Bollen Ngetti apatikana huko Segerea

Bollen Ngetti apatikana huko Segerea

Hivyo vyote ulivyotaja Mkuu mwisho wa siku vinasimama na umma (the voice of the majority ). Siyo vya kutegemea sana kukubakisha madarakani.
Kumbe sababu kubwa ni Membe hivi magufuli zimwo kweli unamuogopa membe ili iweje kwa mfano wakati una kila kitu? wewe ni rais, majeshi polisi TISS yote yako chama pia wewe ni mwenyekiti si umfukuze membe uwanachama?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama vipi amfuate mwenzake ngurumo
HOJA TATU CHANZO CHA KUKAMATWA/KUTEKWA BOLLEN NGETTI.

Bollen Ngetti, Mwanaharakati na Mwandishi wa habari za kiuchunguzi, aliyetekwa tarehe 23/12/2019 siku ya Jumatatu na watu wasiojulikana, kapatikana leo maeneo ya Tabata Segerea baada ya kuachiwa huru na watu hao wasiojulikana.

Bollen Ngetti, amekuwa akitekwa mara kwa mara kwa kipindi hiki cha miaka takribani 4, Mwanaharakati na Mwandishi huyu wa habari za kiuchunguzi ametekwa mara 3 na kutekwa kwake jana ikiwa ni mara ya 4.

KWANINI BOLLEN NGETTI ANATEKWA SANA?


Hizi ni hoja tatu (3) zilizotajwa na Bollen baada ya kutekwa siku ya Jana Tarehe 23 na kuhojiwa hoja hizi tatu ambazo Bollen Ngetti kataja kwamba zimekuwa zikijirudia sana anapotekwa na watu wasiojulikana.

1. Bollen Ngetti kila anapotekwa, amekuwa akiulizwa mahusiano yake ya kikazi na Waziri Mstaafu wa Mambo ya Nje wa Serikali ya awamu ya nne, Ndg. Bernard Kamillus Membe.

2. Bollen Ngetti, anasisitizwa pia kutaja watu anaofanya nao kazi, kazi ambayo watekaji hataki kuiweka wazi!

3. Bollen Ngetti, analazimishwa na watekaji kutaja sehemu ambayo huwa wanafanya vikao, vikao ambavyo Bollen hajui ni kuhusu nini.

Bollen Ngetti anakiri now hayuko sawa kisaikolojia, maana pamoja na kuamua kunyamaza lakini bado amekuwa akiandamwa sana.

Anamalizia kwa kusema "Namuachia Mungu, maana sasa sina amani tena kwenye nchi yangu, naamini ipo siku yatakwisha tu".
 
Huyo jamaa sijui Ngeti inaelekea siyo smart sana kichwani vinginevyo asingechezea maisha yake kijinga hivyo.
Wicked man uloz umetawala kwenye kichwa mpk uone mateso ya wenzio sio kitu kama ambavyo ulifurahia Lissu kupigwa Lissu.
 
Ilitakiwa aamue kuwa liwalo na liwe, unakufa na watano au sita hivi, watanyooka
Rahisi sana kuongea hivyo kama hayajakukuta haya mambo.
Kupambana na wanaume sita wenye silaha na mafunzo maalum sio rahisi kama unavyo ona kwenye filamu za Hollywood au unavyo soma kwenye vitabu vya akina Willy Gamba, Joram Kiango, James Bond, au Jason Bourne.

Hata ukiwa na silaha kama wakikustukiza ghafla watakutuliza tu kabla hujamdhuru yeyote.
Kitu kingine kuwa tayari kufa hakupangwi kabla na mtu mwenye tamaa ya maisha bora bali hupangwa na mtu aliye kata tamaa.
Waandishi kama akina Bollen Ngeti wanaandika sababu ya kutafuta maisha bora kutokana ahadi za wafadhili wa maandishi yao.
 
Smart sana kichwani ni Musiba anaeshinda mitandaoni praising Lawino.
Musiba is very SMART!
Muulize Tundu Lissu hadi leo hajarudi kisa alionywa na MUSIBA mpango uliopangwa na "mwenye uwenyekiti wake" mara atakapotua Airport.
Kinana na Makamba wanajua how SMART Musiba is hadi akatibua mipango yao yote waliyopanga kumvuruga RAIS.
Na Mungu alivyo mkubwa akawathibitishia waliokuwa wakidhani MUSIBA ni mropokaji.
 
Kama katekwa mara 4 na bado anaachwa akiwa hai, basi hii inaleta maswali kadhaa;

1. Kuwa, hivi iweje huyu Mwandishi anatekwa mara 4 na bado anakuwa hajifunzi tu namna ya kujilinda mwenyewe kwa maana ya self defense?

2. Na iweje hawa watekaji wamteke mara 4 na wakiwa na madai yaleyale yasiyo na majibu??

å Yaani wamteka mara ya kwanza kwa madai yaleyale, hawakupata jibu....wakamuachia....!!

å Mara ya pili, madai yaleyale, hawakupata jibu wakamwachia....!!

å Mara ya tatu, madai yaleyale, hawakupata majibu kwa mtu yuleyule, wakamuachia....!!

å Na sasa ni mara ya NNE, madai yaleyale, wakamuachia bila kumdhuru ikiwemo kuuwawa ama kupotezwa kabisa kama kina Ben Sanane ama Kagomba....!!

JAMANI tujiulize hivi ina - make sense kweli juu hiki kinachoitwa utekaji kwa staili hii??

Je, siyo mchezo fulani tu wenye nia na malengo fulani?

Hii maana yake tutegemee huyu jamaa kutekwa kwa mara ya 5 huku watekaji wakiwa na madai yaleyale ambayo huyu mtekwaji hawezi kuwapatia majibu yake....

Na kwanini serikali kupitia vyombo vya ulinzi na usalama hususani jeshi la polisi wameshindwa kukomesha tabia hii ambayo kwa viwango vyote inaipa nchi yetu ya Tanzania taswira mbaya ktk anga za kimataifa?

Ama vyombo vyenyewe hivi ndivyo vinahusika na ujinga huu wa kuteka watu hovyo hovyo??
 
Inasikitisha kwakweli.
Lakini Bollen Ngeti ajuwe akitaka kuingia kwenye siasa iwe kwa uandishi au harakati zozote basi ajiandae na akubaliane na mashambulizi ya kila namna kama vile yeye anavyo washambulia watu kwa namna anayoweza yeye yaani kutumia uandishi.
Vingineyo aandike vitu vingine kama waandishi wenzie wasiokumbana na misukosuko kama yake.

Asishambulie watu kwa uandishi na kutegemea hatashambuliwa kujibiwa mashambulizi, wenzie anao washambulia wao wana njia zingine tofauti na uandishi.
Asitafute huruma toka kwa wananchi, akianzisha vita basi apambane mwenyewe.
Kama ametaka kuwa shujaa ni vizuri sasa aendelee na vita alivyo anzisha na sio kuja kulialia. Akifanikiwa itakuwa faida yake binafsi na familia yake.
Huenda hata ameahidiwa kuwa waziri wa habari au afisa habari wa ofisi kubwa kabisa. Mtaka cha uvunguni lazima ....
Mambo mengne bhana ni kujichosha tu.
Mtu anaondoka nyumban kwake anazima simu zake anaenda kwa mchepuko wake wajinga wanaanza kutangaza ametekwa.

Mashuhuda wakat anatekwa ni akina nani?
Yaani jamaa kaenda kwa mchepuko wake kalala siku moja anaweka defence kwa mke wake kwamba katekwa na mijitu inaamini ametekwa..
Kizazi hiki kina shida kweli

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mambo mengne bhana ni kujichosha tu.
Mtu anaondoka nyumban kwake anazima simu zake anaenda kwa mchepuko wake wajinga wanaanza kutangaza ametekwa.

Mashuhuda wakat anatekwa ni akina nani?
Yaani jamaa kaenda kwa mchepuko wake kalala siku moja anaweka defence kwa mke wake kwamba katekwa na mijitu inaamini ametekwa..
Kizazi hiki kina shida kweli

Sent using Jamii Forums mobile app
Hata Nondo alipotekwa kuna watu kama wewe walisema amejiteka... KASHINDA MARA YA PILI SASA...
 
Back
Top Bottom