Bollen Ngetti apatikana huko Segerea

Bollen Ngetti apatikana huko Segerea

Kwa hiyo kiufupi alitekwa na jeshi la polisi na hawakutaka ndugu na jamaa wajue?
Ki ukweli sheria inakiukwa sana na jeshi la police katika ukamataji washukiwa.
Na utakuta wengi wao wanaishia kuuawa huko na kuzikwa kisirisiri.
Kama hawatobadilika na wao ipo siku yatawageukia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unamwamini boya huyo Ngetti anampa promo Membe Kwi kwi kwi!,jinga sana
Kumbe sababu kubwa ni Membe hivi Magufuli zimwo kweli?

Unamuogopa membe ili iweje kwa mfano wakati una kila kitu?

Wewe ni rais, majeshi polisi TISS yote yako chama pia wewe ni mwenyekiti si umfukuze Membe uwanachama?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
HOJA TATU CHANZO CHA KUKAMATWA/KUTEKWA BOLLEN NGETTI.

Bollen Ngetti, Mwanaharakati na Mwandishi wa habari za kiuchunguzi, aliyetekwa tarehe 23/12/2019 siku ya Jumatatu na watu wasiojulikana, kapatikana leo maeneo ya Tabata Segerea baada ya kuachiwa huru na watu hao wasiojulikana.

Bollen Ngetti, amekuwa akitekwa mara kwa mara kwa kipindi hiki cha miaka takribani 4, Mwanaharakati na Mwandishi huyu wa habari za kiuchunguzi ametekwa mara 3 na kutekwa kwake jana ikiwa ni mara ya 4.

KWANINI BOLLEN NGETTI ANATEKWA SANA?

Hizi ni hoja tatu (3) zilizotajwa na Bollen baada ya kutekwa siku ya Jana Tarehe 23 na kuhojiwa hoja hizi tatu ambazo Bollen Ngetti kataja kwamba zimekuwa zikijirudia sana anapotekwa na watu wasiojulikana.

1. Bollen Ngetti kila anapotekwa, amekuwa akiulizwa mahusiano yake ya kikazi na Waziri Mstaafu wa Mambo ya Nje wa Serikali ya awamu ya nne, Ndg. Bernard Kamillus Membe.

2. Bollen Ngetti, anasisitizwa pia kutaja watu anaofanya nao kazi, kazi ambayo watekaji hataki kuiweka wazi!

3. Bollen Ngetti, analazimishwa na watekaji kutaja sehemu ambayo huwa wanafanya vikao, vikao ambavyo Bollen hajui ni kuhusu nini.

Bollen Ngetti anakiri now hayuko sawa kisaikolojia, maana pamoja na kuamua kunyamaza lakini bado amekuwa akiandamwa sana.

Anamalizia kwa kusema "Namuachia Mungu, maana sasa sina amani tena kwenye nchi yangu, naamini ipo siku yatakwisha tu".
Usiseme unamwachia mungu hakuna kitu kama hicho. Pambana na mungu atakuwa upande wako. Ulisema namwachia mungu ni hatua ya kukata tamaa. Pambana ndani ya nchi yako kwa kusema ukweli hata kama wanakuua kwa kusema. Hapo ndio watakapojua mungu ni nani
 
Tatizo la hawa wanaotekwa ni hiyo kauli yao ya kumwachia Mungu...
Siku zote Mungu yupo bize sana..
Sasa utamuachiaje mambo yanayosababishwa na binadamu (m)wenzako...??
Hivi hii ni theolojia ya wapi??
Aiiseee. Wazo la mwaka hili!
 
Huyo jamaa sijui Ngeti inaelekea siyo smart sana kichwani vinginevyo asingechezea maisha yake kijinga hivyo.
Kwa mara ya kwanza ninakubaliana nawe; lakini kwa maana tofauti kabisa na uliyonayo wewe.

Huyu mwishowe watamuua, lwa lelemama zake hizi kuhusu jambo analotakiwa kulichukulia kwa umakini mkubwa sana.
 
HOJA TATU CHANZO CHA KUKAMATWA/KUTEKWA BOLLEN NGETTI.

Bollen Ngetti, Mwanaharakati na Mwandishi wa habari za kiuchunguzi, aliyetekwa tarehe 23/12/2019 siku ya Jumatatu na watu wasiojulikana, kapatikana leo maeneo ya Tabata Segerea baada ya kuachiwa huru na watu hao wasiojulikana.

Bollen Ngetti, amekuwa akitekwa mara kwa mara kwa kipindi hiki cha miaka takribani 4, Mwanaharakati na Mwandishi huyu wa habari za kiuchunguzi ametekwa mara 3 na kutekwa kwake jana ikiwa ni mara ya 4.

KWANINI BOLLEN NGETTI ANATEKWA SANA?


Hizi ni hoja tatu (3) zilizotajwa na Bollen baada ya kutekwa siku ya Jana Tarehe 23 na kuhojiwa hoja hizi tatu ambazo Bollen Ngetti kataja kwamba zimekuwa zikijirudia sana anapotekwa na watu wasiojulikana.

1. Bollen Ngetti kila anapotekwa, amekuwa akiulizwa mahusiano yake ya kikazi na Waziri Mstaafu wa Mambo ya Nje wa Serikali ya awamu ya nne, Ndg. Bernard Kamillus Membe.

2. Bollen Ngetti, anasisitizwa pia kutaja watu anaofanya nao kazi, kazi ambayo watekaji hataki kuiweka wazi!

3. Bollen Ngetti, analazimishwa na watekaji kutaja sehemu ambayo huwa wanafanya vikao, vikao ambavyo Bollen hajui ni kuhusu nini.

Bollen Ngetti anakiri now hayuko sawa kisaikolojia, maana pamoja na kuamua kunyamaza lakini bado amekuwa akiandamwa sana.

Anamalizia kwa kusema "Namuachia Mungu, maana sasa sina amani tena kwenye nchi yangu, naamini ipo siku yatakwisha tu".
. mmmmh Ni hatari nchi hii hii askari na intelligence YOTE. HII YA. TANZANIA WATEKAJI HAWAJULIKANI??????
 
. mmmmh Ni hatari nchi hii hii askari na intelligence YOTE. HII YA. TANZANIA WATEKAJI HAWAJULIKANI??????

Wanashindwa kufanya Ujasusi wa kiuchumi ili nchi ishindane na nyingine kiuchumi... Wao wanaendekeza kuteka, kupiga na kudhuru wenye akili za kuhoji!!
 
Back
Top Bottom