Baada ya 200 tuliosoma asubuhi, wengine wanane? kwa hiyo jumla ni 208?
Au siyo?
Unakumbuka isue ya kapuya??
MAKOSA YA PROF. JUMA KAPUYA.
Bila kuathiri sharia ya Ubakaji, Prof Kapuya anaonekana na muogopa Binti huyo na kuashiria kuwa ni mzazi mwenzie na yapo mambo mazito ambayo Binti huyo anayajua dhidi ya KAPUYA. Wametajwa watu wengi kuwa wametapeliwa na Bint huyo lakini watu wote hao hakuna hata mmoja anayemouogopa Binti huyo kama anavyofanya Kapuya.Taarifa za Mitandao zinaonyesha kuwa Kapuya ametuma Zaidi ya Tshs 3,000,000 kwa kificho kwa madai kuwa anamsaidia ada mtoto huyo huku yeye Mwenyewe Kapuya anasema kuwa Mtoto huyo ni tapeli .Sasa hapa Kapuya anajichanganya. Ni kwa vipi mtoto huyo Kapuya aseme kuwa Mkubwa na mama mzima kabisa wa miaka 21 ,lakini wakati anatoa msaada wake anasema alikuwa anamulipia ada ya Shule sasa ni lini KAPUYA aligundua kuwa anatapeliwa??Ni lini Kapuya aligundua kuwa huyo ni mtu mzima sasa angesitisha malipo hayo??? Ni kwa nini Kapuya akubali kulipa pesa hiyo kwa Mkono badala ya kulipa moja kwa moja Shuleni ?? Ni kwa vipi waziri wa ulinzi anatapeliwa na Kahaba na kuuza utu na nchi??
(A) USHAHIDI YA MALIPO YA M-PESA KUTOKA SIMU YA KAPUYA(0755993930):
(1)
R93NY448 ImethibitishwaUmepokea Tsh505,000kutoka kwa
JUMA KAPUYATarehe 21/6/13 saa 11:07 AM Salio lako la M-PESA ni Tsh 505,000
(2)
U26UG365. Imethibitishwa Umepokea Tsh 300,000 kutoka kwa JUMA KAPUYA
Tarehe 31/8/13 saa 3:28 PMSalio lako la M-PESA ni Tsh 300,000
(3) V04EU470 Imethibitishwa Umepokea Tsh 400,000kutoka kwa JUMA KAPUYA
Tarehe 24/9/13 saa 2:38 PMSalio lako la M-PESA ni Tsh 400,040
Malipo ya mwisho ya KAPUYA yamefanyika hadi tarehe 24/9/2013 wakati yeye mwenyewe Kapuya anasema kuwa amegundua kuwa Binti huyo ni mtu mzima na tapeli sasa ni kwa nini alikuwa analipa pesa kwa tapeli???
(B) UJUMBE WA VITISHO KUTOKA SIMU YA KAPUYA.
Simu 0784 993930 mali ya JUMA KAPUYA imekuwa ikitoa vitisho hasa baada ya mgogoro huu kufika kwenye media.
(i) Hata hivyo kufikia mwezi Februari mwaka huu2013 , mtu asiyefahamika alienda nyumbani na kutelekeza gari aina ya T.199 BGY Mercedes Benzi ya Blue wakati wanafunzi hao wakiwa shuleni, kisha kuacha ufunguo kwa jirani yao kwa maelekezo kuwa wakifika awapatie.
Na Kapuya aliwapigia simu kuwaarifu kuwa amempa zawadi ya gari kwa ajili ya matumizi ila yeye na dada yake wanaruhusiwa kuuza ili wapate pesa kwa ajili ya mahitaji yake siku zilizosalia, kwani muda sio mrefu baada ya uchguzi mkuu 2015, Kapuya atakuwa Waziri Mkuu, hivyoitakuwa ngumu yeye kumtumia huyo binti pesa kama alivyoelekezwa na jeshi la polisi kituo cha Oysterbay.
Baada ya mwanafunzi huyo na dada yake ambaye ana umri wa miaka 20, kupewa gari walishindwa kulitumia hivyo kutoa taarifa polisi kwani kwa kupokea gari hilo ilikuwa ni kuwatelekeza kwani yeye hana hata hela ya kuweka mafuta ya gari, hivyo walienda polisi ili kesi ipelekwe mahakamani kumshtaki kapuya.
Polisi wa Oysterbay walikubali kulipeleka tatizo hilo kwa Katibu wa Bunge, ambaye alimwita mwanafunzi huyo na mdogo wake waende Dodoma kukutana na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ingawa walipofika Dodoma walikaa na kamati ya hiyo kwa maelezo kuwa Kapuya hakuwepo hadi Bunge lilipoisha walirejeshwa Dar es Salaam.
Mtoto huyo na dada yake alitoka ofisi za CCM lakini akiwa anaelekea kituo cha basi alithadharishwa na mwanafunzi mwingine kwa haraka kuwa akimbie kwa kuwa atamwagiwa tindikali na watu waliokuwa wanamfuata nyuma, alikimbilia katika mtaa wa Hoteli ya Star light kisha aliomba msaada baada ya kupotea njia na hivyo alisaidiwa na mama mmoja kufikishwa chumba cha habari cha Channel Ten. Mmoja wa watoto hao, alidai kuwa miongoni mwa vijana waliokuwa wanawatisha juzi walikuwa katika gari T170 BGY, Benz, Cream Metalic, ambayo inamilikiwa na KAPUYA.
Hapa inajieleza wazi kuwa vyombo vya dola kwa maana ya polisi wanafahamu jambo hili na kwamba sehemu ya polisi hawa wapo katika mfuko wa KAPUYA na hawa uwezo juu ya suala hili.
(ii) Alfajiri saa 11:21 kupitia simu yake ya mkononi yenye namba
0784993930, Profesa Kapuya alituma ujumbe ufuatao kwa mtoto huyo
: chagueni kunisubiri tuje tuongee au mnataka kufa?
Baadaye saa 1:07 asubuhi, alituma ujumbe mwingine kutoka simu hiyo hiyo kwenda kwa mtoto huyo, ukisema
: Mkiuawa, itakuwa nzuri, itawapunguzia gharama za kuishi. Usitake kugombana na serikali, mtoto mdogo kama wewe. Sisi ndo wenye nchi yetu.
Mwambieni Mbowe mwenye hilo gazeti awape nyumba ya kuishi. Si mmemuingizia hela leo? Mnatumika bure watu wanaingiza hela nyingi, mmenitibua lazima niwauwe wiki hiii haitaisha, nitapanga kambi popote.
Jana si wamekuficha? Tuone kama utalindwa milele. Kazi ya kulindwa imeisha, maana wameshatengeneza hela.Lazima mvae sanda. Hilo sio ombi, ni wajibu wenu. Mnajitia mafia watoto sio?Watoto wetu wanauza unga, nani anawakamata?Nani atapigana nasi?Ujumbe mwingine uliotumwa kwa mtoto huyo saa 11:2 3 ulisema:
nimwakosea sana, acha nife mie nakunywa sumu nijiue, na nyie mje mnizike., saa 5:17 usiku wa kuamkia jana alituma ujumbe usemao: Si mpo Bilz? Sasa tupo pamoja na nyie mpaka usiku.Baadaye saa 5:31 alituma ujumbe huu: Hivi hamkubali kushindwa? Leo ulifuata nini ofisi ya CCM?
(iii) Huku akiendeleza vitisho vya kuwaua ikiwa binti huyo hatakubali, katika moja ya ujumbe wake, Kapuya alisema
: Najua kesi ni watu wawili, sasa kwanini hamkubali? Hivi hela nitakayompa mtu akuue si bora nikupe uanze maisha?
Wakili nimempa hela nyingi, magazeti pia nimewapa, naumia jamani, unaweza kukanusha taarifa hii na kufuta ushahidi halafu mimi nikupe hela uende popote, bungeni sifiki na nitafukuzwa, nyie mtapata nini?
Nakupa masaa mpaka saa sita nitakuwa nimeshatuma hela, unachukua passport unasepa na hakuna kurudi, ukikaidi roho itakwenda kupumzika, unataka kufa kibudu?Jiangalie.
Ukienda kwa DPP mwambie kuwa hutaki kesi, mimi niitwe, usipokubali nitakuua, yaani siku si nyingi, na hakuna wa kunifanya lolote, umeshasikia vifo vingapi, unataka kufa wakati huu au kwa ahadi ya Mungu? alimwandikia ujumbe binti huyo.
Kapuya alizidi kumbembeleza binti huyo akimwomba afikirie namna alivyowasaidia kiasi cha kuwapa gari aina ya Benz, na kwamba hata kama amemwambukiza ukimwi, lakini atambue kuwa maisha hayana spea.
Sikiliza nawaambieni, kwanini mnatumiwa, maana yake ni kuwa hao watu wa haki za binadamu hawawezi kuwapa hela
hebu tafakari nimetoa Benz, nimekupa ukimwi sawa, maisha hayana spea, mimi nitafungwa, wewe utapata nini? Mimi nina miaka 69 hata nikifa leo, nakubali kwenda popote hata kwa DPP tukae meza moja, najua nitafungwa tu.
Kwa mujibu wa mawasiliano yaliyonaswa na Tanzania Daima Jumatano, Kapuya hata hivyo ameendelea kutishia kumtoa roho binti huyo hasa baada ya kuona ushauri wake unagonga mwamba. Moja ya ujumbe uliotumwa kutoka katika namba hiyo unasomeka hivi
: Nitakuua tu huwezi kukimbia milele, si hutaki kunisikiliza, kwani kesi ya Mahita ilikuwaje? Mbona anahudumia na hakuna wa kumfanya lolote, kuwa kimya uone, hujachelewa, kama hutaki lazima mimi na Hamis tukuue.
(iv) Uchunguzi wetu umebaini kuwa mara baada ya taarifa ya gazeti hili jana kuandika mwendelezo wa kashfa hiyo, huku likimkariri Waziri wa Ushirikiano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Samuel Sitta, akihoji ukimya wa serikali katika kashfa hiyo, Profesa Kapuya alituma ujumbe mwingine wa kutishia kumuua binti huyo. Ujumbe huo kutoka simu namba 0784993930 inayomilikiwa na Kapuya kwenda kwa namba inayomilikiwa na binti huyo, unasomeka hivi:
Ni lazima nitakuua wewe na ndugu yako na atakaetaka kuwasaidia, huyo Samweli Sitta asijiingize kwenu, yaani nitakuua tena sijui leo mtalala wapi! We unadhani nani atakayenifunga?Ndo nishakupa ukimwi, sasa nakutaka uache mara moja kuongea na mtu, nitakuwinda popote tuone!