Boeing kuwasilisha 787 ya kwanza kabisa

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,246
33,007

Kampuni ya utengenezaji ndege ya Marekani - Boeing - itawasilisha rasmi ndege ya kwanza aina ya 787 Dreamliner kwa shirika la ndege la All Nippon Airways (ANA) la Japan.

101020182857_boeing_dreamliner_386x217_nocredit.jpg
Dreamliner


Awali Dreamliner ilipangwa kuwa tayari mwaka 2008, lakini Boeing imekumbwa na mflulizo wa vikwazo, ambapo hivi karibuni moto uliwaka ndani ya ndege za majaribio mwezi Januari.
Ndege hiyo isiyotumia mafuta mengi imetengenezwa kwa kutumia malighafi nyepesi.
Boeing inapanga kutengeneza ndege 10 kwa mwezi kuanzia mwaka 2013.
Ndege hiyo itakabidhiwa kwa ANA katika kitongoji cha Everett, Washington kabla ya kuruka na kwenda Tokyo ambapo itawasili siku ya Jumatano.
101030105410_boeing_787_dreamliner_226x170_nocredit.jpg
Dreamliner


Boeing imesema ndege hiyo yenye safu mbili na ukubwa wa kati ina madirisha makubwa na hali nzuri ya unyevunyevu ndani ya ndege na hewa safi hali ambayo itaruhusu abiria kuwasili wanapokwenda wakiwa katika njema zaidi.
Lakini matatizo ya Dreamliner yameharibu sifa ya Boeing, na kampuni hiyo ina matumaini kuwa uzinduzi wenye mafanikio utasaidia kufuta ucheleweshwaji uliotokea.
Mashaka

Makamu wa rais wa masuala ya masoko wa Boeing, Randy Tinseth ameiambia BBC: "Huu ni mradi ambao umetoka mbali. Tunaamini itakuwa ndege nzuri.
"Hatimaye tunaona matumaini ya maelfu ya 787 katika siku za mbele."
Alipoulizwa sababu za kuchelewa kutoka kwa ndege ya Boeing 787 Bw Tinseth amesema "kuna mashaka katika kila ndege mpya".
Amesema: "Tumetumia fedha zaidi katika ndege hii kuliko tuliyotarajia, lakini kwa mara nyingine tena bado tupo katika nafasi nzuri, tunaamini mradi huu utaendelea kuwa na faida."
Uzalishaji

Uzalishaji wa Dreamliner kwa sasa unatoa takriban ndege 2.5 kwa mwezi.
Mpaka sasa ndege zipatazo 821 aina ya 787 zinatakiwa kununuliwa kutoka Boeing, ambayo inasema inatumia 20% pungufu ya mafuta yanayotumiwa na ndege za kawaida za ukubwa huo.
110926164458_dreamliner_466x350_bbc_nocredit.jpg
Boeing na Airbus


Ikiwa na uwezo wa kubeba abiria 290 katika ndege yake kubwa ya 787-9, lakini 787 ni ndogo kuliko jumbo jet 747 ya Boeing.
Hata hivyo, Boeing inadhani kuwa 787 itakuwa maarufu katika makampuni ya ndege, kwa kuwa itakuwa na uwezo wa kuruka moja kwa moja kwenda katika viwanja vidogo vya ndege.
Mahasimu

Mahasimu wa Boeing wa Ulaya, Airbus, kwa sasa inatengeneza mshindani wa moja kwa moja wa 787, iitwayo Airbus A350 XWB.
Airbus imepokea maombi ya ununuzi yanayozidi ndege 550 ya A350 XWB, lakini ndege hiyo haitakuwa tayari hadi mwaka 2013.
ANA inatazamia kuanza kutumia ndege ya kwanza aina ya 787 katika safari kutoka Tokyo kwenda Okayama-Hiroshima tarehe 11 Novemba.
Baadaye itaruisha ndege hiyo kimataifa kutoka Tokyo kwenda Frankfurt Ujerumani, mwezi Januari.
"Watu wengi wanasema kuwa ndege hii [787] itakuwa maarufu sana," amesema George Hamlin, rais wa taasisi ya washauri wa usafirishaji ya Hamlin.

Chanzo: BBC Swahili - Habari - Boeing kuwasilisha 787 ya kwanza kabisa
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom