Bodi ya Pamba: Mfano wa kuigwa Duniani

Bodi ya Pamba: Mfano wa kuigwa Duniani

Sisi wakulima wa Pamba kanda ya Ziwa tunajivunia bodi ya Pamba Tanzania kwa kufanya kazi zake kwa WELEDI mkubwa katika kututafutia masoko ndani na nje ya nchi kwa uharaka sana. Wakulima wenzangu wa pamba ni mashahidi kwa hili kwani tunajivunia pamba na jasho letu wengi wetu tumeweza kuwekeza katika miraid mikubwa mikubwa ya maendeleo na kilio cha kisasa kabisa (Teknolojia za kisasa) Kama ingekuwa uwezo wangu ningepandisha hadhi bodi hii na iwe wizara kamili (WIZARA ya MAENDELEO ya PAMBA)
** WEBSITE: www.cotton.or.tz
NB: Wafanyakazi wa bodi hii wanastahili pongezi hasa tukiazimisha siku ya wafanyakazi duniani (Mei Mosi)

TANGIA WENYE GINERY WAKIONGOZWA NA NSAGALI,GUNGU,WALE WA CHAGA WA SHINYANGA KWA KUSHIRIKIANA NA WABUNGE KAMA CHEO,NA YULE WA MASWA WAKAMUONDOA MKURUGENZI MKUU KIJANA MTUNGA BASI BODI HAINA MWELEKEO.MIE NASHAURI MAGUFURI AIPITIE BODI NA AMURUDISHE MTUNGA KAMA MKURUGENZI MKUU BASI BODI ITAFANYA KAZI ILIYOTUKUTA.KWA SASA BODI IPO KAMA HAIPO VILE.
 
Kanda ya ziwa haitaelewa lolote kama hii bodi itaachwa hivi hivi,watarudia mchezo wa kuuza mbegu za hovyo zisizoota na kibarua cha mwigulu kitaota nyasi,mwigulu angalia sana hawa jàmaa,jamaa hawa hovyo kabisa
 
Taza
kukabiliana hili jini ni wakati wakulima wajiundie vyama vya hiari ambavyo watavitumia kujitafutia masoko na mambo mengine.
Tazama huyu mbumbumbu naye, unatakiwa ujue kwamba wadau wakuu wa sekta ya
Pamba ni wakulima wa pamba, wafanya biashara ya pamba pamoja na serikali. Usitegemee composition ya board of directors isiwe na hao wadau waliotajwa. Bodi ya uvuvi kama ipo ni lazima iwe na mjumbe anayewakilisha wanunua samaki kama vile gachuma alivyo tcb. Na after all gachuma hajawahi kuwa mwenyekiti wa tcb zaidi ya ujumbe. Huyu ni chair wa TCA ambacho ni umoja wa wanunuzi kama vile bodaboda walivyo na umoja wao.
 
We jamaa umelipwa,hivi unaujua hata mmea wa pamba unaonekanaje,wakulima wa pamba kanda ya ziwa wanamaisha magumu.pamba inafanyiwa udalali sana na mkulima anamia,ukiwa huna kitu cha kuposti sio lazima kuna na ngongera zisizo na takwimu husika.
 
Mtoa mada naona mnaweweseka kwa
Kwa kotoa hoja mfu kabisa hii bodi ni bodi ambayo haiko kwa ajili ya kusaidia wakulima iko kwa ajili ya masirahi ya matumbo yao
Fikiri mkulima anatumia gharama kubwa ktk kuzarisha pamba kwa makadilio ya chini kabisa ekari moja mkulima hutumia 450000= kuanzi kukodi shamba kulima hadi kuvuna ambapo akivuna anaishia kupata kilo 500 kwa ekari kwa bei ya sh 800 = 400000 kwa mauzo yote ndo maana wakulima wengi wa pamba wamekiacha kilimo hiki na uzarishaji umeshuka wamehamia kwenye mazao mbadara kama Choroko, dengu , alzet hivyo mpo hapo bodi kuneemesha matumbo yenu
Angarizo Magufuri asipo liangalia hili kwa makini atapoteza kura nyingi 2020 kanda ya ziwa
Arafu zao la pamba ndo imekuwa zao kuiibia wanyonge Ndo maana kina Chenge, mbunge wa Itilima Njaru lengo ni kuibia wanyonge
 
We jamaa umelipwa,hivi unaujua hata mmea wa pamba unaonekanaje,wakulima wa pamba kanda ya ziwa wanamaisha magumu.pamba inafanyiwa udalali sana na mkulima anamia,ukiwa huna kitu cha kuposti sio lazima kuna na ngongera zisizo na takwimu husika.
Watu wanashangaza kweli Mkuu,hii bodi ni jipu kubwa sana
 
Siku bodi za mazao ya Kilimo zikianza kutumbuliwa,magufuli atakuwa anaongea moja kwa moja na roho na mioyo za watu wa kawaida kabisa wanaoamka na jembe asubuhi kuandaa Shamba,wanauziwa mbegu za hovyo zisizoota kutokana mitajo yao ya kimasikini,zikiota wanauziwa Dawa ya kuua wadudu ambayo haiui wadudu bali inahamasisha wazaliane,baadae wanaibiwa kwenye bei na mizani,hawa hawa wananchi masikini
 
Taza

Tazama huyu mbumbumbu naye, unatakiwa ujue kwamba wadau wakuu wa sekta ya
Pamba ni wakulima wa pamba, wafanya biashara ya pamba pamoja na serikali. Usitegemee composition ya board of directors isiwe na hao wadau waliotajwa. Bodi ya uvuvi kama ipo ni lazima iwe na mjumbe anayewakilisha wanunua samaki kama vile gachuma alivyo tcb. Na after all gachuma hajawahi kuwa mwenyekiti wa tcb zaidi ya ujumbe. Huyu ni chair wa TCA ambacho ni umoja wa wanunuzi kama vile bodaboda walivyo na umoja wao.
unakumbuka kashfa ya bodi ya kahawa ya Maghembe kuteua wajumbe wa bodi kiupendeleo? ndiyo ujue wakulima hawana sauti kwenye hizi bodi ni serikali kupitia waziri wa kilimo. hata wakoloni wakati wanaanzisha crops boards waliwaambia wananchi ni kwa faida yao.
 
Bodi hizi zinapaswa kuwasaidia wakulima wa zao husika japo sina uhakika wa bodi hii kama imefanya haya anayopamba mtoa mada
 
Hebu acha uongo mchana mchana kama kweli hiyo bodi ya pamba ingekuwa inafanya kazi vizuri kama unsvyongopa hapa uzslishaji wa pamba usingekuwa unashuka kila mwaka!

Usitufanye wote ni wajinga hapa
 
Mtoa mada anaisifu kwamba inapaswa kusifiwa duniani
 
Bodi ya BIA ndio haifai kuigwa kabisa dunia daily bia zinapanda bei.
 
Sisi wakulima wa Pamba kanda ya Ziwa tunajivunia bodi ya Pamba Tanzania kwa kufanya kazi zake kwa WELEDI mkubwa katika kututafutia masoko ndani na nje ya nchi kwa uharaka sana. Wakulima wenzangu wa pamba ni mashahidi kwa hili kwani tunajivunia pamba na jasho letu wengi wetu tumeweza kuwekeza katika miraid mikubwa mikubwa ya maendeleo na kilio cha kisasa kabisa (Teknolojia za kisasa) Kama ingekuwa uwezo wangu ningepandisha hadhi bodi hii na iwe wizara kamili (WIZARA ya MAENDELEO ya PAMBA)
** WEBSITE: www.cotton.or.tz
NB: Wafanyakazi wa bodi hii wanastahili pongezi hasa tukiazimisha siku ya wafanyakazi duniani (Mei Mosi)
CAG kasemaje?
 
Back
Top Bottom