Nafikiri forum hii tuitumie kuelimishana baadhi ya mambo ambayo tuna fununu nayo. Nimesema kwa mwanzisha mada kwamba sifa alizotoa kwa bodi zimetiwa chumvi sana,lakini pia si sawa kuwapa lawana zisizo za kweli. Naomba nisaidie kama ifuatavyo:-
1) Katika nchi yetu bado hatujaweza kuwa na mfumo maalumu wa kuwa na mbegu bora hasa kwa mazao yote makuu, matumizi ya mbegu bora nchini ni chini ya 20%. Bodi siyo wataalamu wa mbegu na wala hawazalishi mbegu na si jukumu lao kwa mjibu wa sheria za pamba. Wanachofanya bodi ni kumtafuta yeyote mwenye mbegu zozote (recycled seeds) awe mzungu, mhindi, mwarabu, mkurya, msukuma, mmakonde ama yeyote apeleke mbegu kwa wakulima. Ni wajibu wa wadau wote kwa pamoja kuhakikisha kwamba mfumo bora wa mbegu unatafutwa.
2) Kuhusu bei: Serikali ya TZ haina power ya kupanga bei, wanaopanga bei ni watumiaji wakuu wa pamba ambao pia ndo wazalisha wakuu wa pamba (market share ya TZ ni below 1% kwenye world market). Serikali inachofanya kwa kushirikiana na wadau wote wakiwamo wawakilishi wa wakulima ni kufanya translation ya bei iliyoko sokoni Newyork na kuibadirisha kwa pesa zetu na ndo anayopewa mkulima baada ya kutoa gharama zinazohusika. Bei inayotangazwa na serikali ni elekezi kwamba hakuna mnunuzi anaruhusiwa kushuka chini ya hapo lakini kupanda juu ni ruksa. Kwamba geita bei iko chini kuliko bariadi hilo pengine siwezi kulisemea lakini naona lingekuwa kosa la bodi kama bei ya geita ni chini ya bei elekezi. Lakini vinginevyo ni masuala ya uhuria.
3) Wakulima kukopwa: Ushirika ulipoanza kuteteleka na hatimaye kufa katika baadhi ya mikoa ulikufa na pesa ya wakulima. Kama hoja zako si za makusudi nakuomba utenge muda kidogo ili ufanye utafiti ili ujue ni nani kakopa wakulima kati ya ushirika na hao binafsi. Kwa uhakika waliokopa wakulima na hawajalipa hadi leo ni ushirika.
4) Bodi kuua ushirika: mie sidhani kama hili ni la kweli, labda tuseme mfumo ndo umeua ushirika (soko huria). Kama zilivyo taasisi zingine za serikali zilizokufa NIC, THB, POSTA, TRC etc, ushirika nao ulikuwa umeanza kuteteleka hata kabla ya soko huria. Bodi kwa mjibu wa sheria ni Regulatory body na kwa hivyo kanuni zinazotumiwa kwa private co. ndo hizo hizo zinatumiwa kwa ushirika. Tatizo liko wapi?
Naweza kuwa siko sahihi sana lakini hizo lawama zako kwa Tcb hazina ukweli wowote.