Bodi ya MCC yainyima Tanzania fedha za msaada

Bodi ya MCC yainyima Tanzania fedha za msaada

Maskini ya Mungu;
Kumbe hata ya Libya huyajui!!
Usije hata siku moja ukategemea demokrasia ya kubambikiziwa na mataifa ya magharibi.
Libya walikuwa poa sana hadi walipolazimishiwa demokrasia ya 'kidhungu' yanayotokea baada ya hapo ni aibu hata kusimulia.
Rejea historia ya Libya tangu mwaka 1990 hadi ulipotokea huu ushenzi wa Arab Spring utajua ninachokiongelea.
Na Arab Spring wajua ilianzishwa na nani na kwa malengo yapi?
Zinduka.

Wazungu ndio walio Leta democracy Tanzania na wakaweka masharti yao,bila ya kufuata masharti hayo hata huyo magufuli hatakanyaga Europe na America tukiwacha na Misaada.
Sisi tupo nyuma ki technology kwa miaka 100 na maendeleo 50 miaka, hivi kweli wa kukataa Misaada?
 
Nafikiri ni vizuri pia kuondoa misamaha yote ya kodi toka kwa wawekezaji wa kutoka nchi za nje sababu sehemu ya faida wanazopata kwa uwekezaji wao Tanzania ndizo huzitumia kutupa misaada.Ajabu sisi tunapowapa nafasi ya uwekezaji nchini kwetu huwa hatuwapi masharti ya kisiasa lakini wao wakishavuna pesa kutoa msaada kidogo toka faida wanayopata wanatupa masharti kibao ya kisiasa.

Bill Gates anauza makomputa na masoftware kibao Tanzania.Anatengeneza pesa nyingi mno na makampuni mengi ya marekani yamewekeza Tanzania bila kupewa masharti ya Kisiasa na watanzania.

Wema wetu ndio wanatulipa kwa kutuingilia mambo ya siasa.

Wawekezaji hawana huruma kwetu naomba serikali iliyopo tufanye biashara nao tu.Wakitaka vitalu vya gesi au madini au ardhi kwanza walipe pesa za kununua na kufidia halafu watoe hisa kwa wenye wenye maeneo zisizopungua 40% wakikataa watuachia vitalu,madini na ardhi yetu.Tuanze kuwa wakali na sisi na kile tulichonacho kama wao wanavyokuwa wakali kwetu kwa vile walivyonavyo.

Bahati mbaya kwako na kwa Taifa,hakuna maliasili iliyogundulika hadi sasa ambayo haina mwekezaji.Maliasili zote zilizogundulika hadi sasa zimeshachukuliwa na wawekezaji,tena kwa mikataba ya siri na sheria haramu zilizopitishwa na wabunge wa CCM- Chama Cha Majipu kwa hati ya dharura.

Si kweli kwamba wawekezaji hawana Huruma,waliokosa huruma ni tuliowapa dhamana ya kusimamia rasilimali zetu,sote tulishuhudia kasi ya mtangulizi wa Magufuli akitiliana sahihi na wawekezaji tena kwa speed ya 4G,mikataba ya uchimbaji wa Gas na Uranium huku akiwa amebakisha muda mfupi kuondoka Ikulu,matokeo yake mrithi wake hana anachoweza kufanya juu ya mikataba hiyo,kwani mikataba hulindwa na sheria za kimataifa.
 
Kihunzi cha kwanza.

Kenya ilinyimwa misaada miaka ya enzi za Moi 1900s lakini ikaendelea kuhimili uchumi wake japo utalii nao ulishuka na kuuwa hoteli nyingi.

Chako ni Chako.

Ni % gani ya pesa za MCC USD 1,2 Bil zingebaki inchini, Najua mabarabara ya Horohoro na Mbinga good development for this country.

Bora kuzuia safari za nje,

Hatua hii itaimarisha Shilingi yetu vs.Dollar?

Dont worry We will emerge out stronger than ever!
 
mnaongea tu nyuma ya keyboard lakini nina shaka kama suala la uongozi mnalijua kwa mapana yake.

Bisha, ongea lakini masharti ya MCC lazima Tanzania watayafuata tu. Wanaojua muda huu wanasugua vichwa wafanyeje ili kujinusuru nyie mnaongea vitu msivyovijua. ETI TRIL 1.3 !!!!!!!!!!!!!!!

kaulize mtu aliyepo Hazina katika hizo 1.3 zimebaki ngapi!!!!!!!

Miradi mingapi ambayo inategemea pesa hapa TZ.

Ni magari mangapi yenye plate number nyekundu DFP unakutana nazo njiani (Hata vijijini utayaona haya magari)

Mnaongea kishabiki usiokuwa na maana, kwa kuwa vidole mali yenu kuandika kila kinachokuja kichwani lakini ubongo hauutumii kuwaza unayoandika!!!!!!!
Tatizo lako unamawazo maskini sana wewe.
 
Tuache kupeana matumaini yasiyo na ukweli. False hope. Gape ni Kubwa sana kati yetu na dunia ya kwanza hivyo kwa utaratibu wa kawaida aliyombele anashika mkono wa chini. Ni ngumu kutoka kwenye simo bila support ya mtu wa juu
 
Hatuna hata vitanda vya hospitali, hatuna madawati kwa watoto hii inasikitisha hiyo pesa ingenunua machine ngapi za CT, barabara kilometa ngapi, vitanda vingapi na ni kwasababu gani hasa ubinafsi!
 
Ni kweli mkuu!

Hatua ya kwanza tuwashukuru wazungu kutunyima pesa yao.

Pia tumshukuru Mungu kutupatia raisi asiye chekea wakwepa kodi na wala rushwa na wazembe.

Tukatae roho ya utegemezi na kutokujiamini. Tunaweza x 1,000,000,000 kujitegemea na kuendelea kama taifa bila kutegemea wazungu!

Mkuu ni bahati mbaya hakuna kitufe cha like. Hii comment yako nimeipenda.
 
Washabikie tu iko siku watakwambia ili upate hiyo hela yako ukubali watu wafanye ngono na mbwa uoe mwanamme na ndoa za waume kwa wake marufuku usipokubal hawakupi misaada ndo unajua yesu yu mlangon

Ni aibu mfano wako hauendani nahali halisi. Ilibidi ulisemee suala la Zanzibar ni hakiam si aki kukamatwa kwa IT wa chama cha Upinznia ni sawa ama la? maana IT wa CM hawajakamatwa. Rudi kwenye hoja suala lashoga na usagaji lina jitegemee na wengi hawaliungi mkono
 
Bahati mbaya kwako na kwa Taifa,hakuna maliasili iliyogundulika hadi sasa ambayo haina mwekezaji.Maliasili zote zilizogundulika hadi sasa zimeshachukuliwa na wawekezaji,tena kwa mikataba ya siri na sheria haramu zilizopitishwa na wabunge wa CCM- Chama Cha Majipu kwa hati ya dharura.

Si kweli kwamba wawekezaji hawana Huruma,waliokosa huruma ni tuliowapa dhamana ya kusimamia rasilimali zetu,sote tulishuhudia kasi ya mtangulizi wa Magufuli akitiliana sahihi na wawekezaji tena kwa speed ya 4G,mikataba ya uchimbaji wa Gas na Uranium huku akiwa amebakisha muda mfupi kuondoka Ikulu,matokeo yake mrithi wake hana anachoweza kufanya juu ya mikataba hiyo,kwani mikataba hulindwa na sheria za kimataifa.

Umempa somo zuri kama ni mwelewa hadi namuonea wivu.
 
Bahati mbaya kwako na kwa Taifa,hakuna maliasili iliyogundulika hadi sasa ambayo haina mwekezaji.Maliasili zote zilizogundulika hadi sasa zimeshachukuliwa na wawekezaji,tena kwa mikataba ya siri na sheria haramu zilizopitishwa na wabunge wa CCM- Chama Cha Majipu kwa hati ya dharura.

Si kweli kwamba wawekezaji hawana Huruma,waliokosa huruma ni tuliowapa dhamana ya kusimamia rasilimali zetu,sote tulishuhudia kasi ya mtangulizi wa Magufuli akitiliana sahihi na wawekezaji tena kwa speed ya 4G,mikataba ya uchimbaji wa Gas na Uranium huku akiwa amebakisha muda mfupi kuondoka Ikulu,matokeo yake mrithi wake hana anachoweza kufanya juu ya mikataba hiyo,kwani mikataba hulindwa na sheria za kimataifa.

Kwenye rushwa hakuna kulindwa kimataifa, zipo sheria za kimataifa zinazopigana na rushwa hata biashara. Kama magufuli anataka kutumbua majipu mikataba aipeleke bungeni
 
Kihunzi cha kwanza.

Kenya ilinyimwa misaada miaka ya enzi za Moi 1900s lakini ikaendelea kuhimili uchumi wake japo utalii nao ulishuka na kuuwa hoteli nyingi.

Chako ni Chako.

Ni % gani ya pesa za MCC USD 1,2 Bil zingebaki inchini, Najua mabarabara ya Horohoro na Mbinga good development for this country.

Bora kuzuia safari za nje,

Hatua hii itaimarisha Shilingi yetu vs.Dollar?

Dont worry We will emerge out stronger than ever!

Baada ya miaka 50 lakini
 
Hata George Bush alimshinda AlGore kimagumashi huko huko marekani....was that what we term as democracy??

Tutajitegemea...!

KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA

Kwanini hukumshitua jembe letu JECHA?
 
Tuzungumzie siasa za visiwani kama watanzania na tuone ni nini tunaweza kufanya kuleta sanity kule. Lakini suala la kulilia misaada halina mantiki; JK kapewa misaada mingapi? Hivi katika miaka yake 10 misaada imetufikisha wapi ukilinganisha na hasara ambazo tumezipata kwa ukwepaji wa kodi uliokuwa umekithiri!! Mbona hawakuwahi kutunyima misaasa kwa sababu ya kuwa na weak revenue collections? - Wanapenda tuendelee na dependency? ... Yes of course. Njia nzuri ya kummiliki mtu ni kumfanya akutegemeee.

That said, siasa za Zanzibar ni tatizo ambalo lazima litafutiwe ufumbuzi wa kudumu. Hii miafaka ya CUF na CCM inaelekea haijawa na maana sana. Tuwe makini.

Suala la kuzungumzia "Cyber crime" - tuelewe kuwa hawa nao walikuwa nyuma ya EL?? Cyber Crime imetumiwa wakati wa uchaguzi tu. Inaonekana hawajakubaliana na matokeo ya Uchaguzi wa bara na wanaamini wale waliokamatwa ndo walikuwa na matokeo sahihi?? .... They got to come out in the open!! Hili hasa naona ndo liko Nyuma. Hizi vurugu zilizokuwepo under JK kuna watu walikuwa wanapenda ziendelee!!

OK, la Zanzibar linaeleweka; ila hayo mengine. Mhh!
 
Nijuavyo hakuna Tanzania bila Zanzibari. Tanzania= Tanganyika+Zanzibari msaada wa MCC ni wa Tanzania. Sasa YEHODAYA hoja zako naona kama zinakinzana.

MCC hawajui kuwa kuna nchi mbili Zinazounda jamhuri ya muungano wa Tanzania? Kwa nini misaada yao wasingeondoa tu kile kipande cha Zanzibar tu? Kwa nini washupalie na TANZANIA bara?
 
Mi naona hawa huwa wana sababu zao za kutotoa msaada. Siwezi amini eti hiyo ndo sababu. Kwani wao sera zao za mambo ya nje zina hata chembe ya demokrasia?

Waacha.waende zao, Magufuli yupo kazini kutafuta hela kwa WANTAANZANI wote.
 
MCC waendelee na msimamo huo, haikubaliki hata kidogo kupokonya ushindi wa wananchi,iwe bara ama visiwani
 
Back
Top Bottom