Bodi ya Maziwa Tanzania ya nini?

Bodi ya Maziwa Tanzania ya nini?

Waongeze ziwe nyingi tuuu,
Bodi ya Mahindi
Bodi ya Karanga
Bodi ya Maharage
Bodi ya Alizeti
Bodi ya Samaki
Bodi ya mchicha
Bodi ya nanasi
Bodi ya ndizi na parachichi
Bodi ya maembe na machungwa
Bodi ya mtama na ulezi
Bodi ya ngano na shayiri
Bodi ya viazi
Bodi ya miwa/sukari
Bodi ya mpunga
Bodi ya tangawizi
Bodi ya viungo vya chai etc.
 
Nimestushwa na kukutana na gari STL pembeni imeandikwa BODI YA MAZIWA daah! hivi kweli tumefikia hatua ya kuunda BODI MAALUM Kwa ajili ya MAZIWA (naamini wanamaanisha haya maziwa ya KUNYWA kupitia mdomoni) hapo hapo tuna TANZANIA FOOD AND NUTRITION CENTRE (TFNC) nao wanapata bajet nenee!!

Mgao wa magari ya kutosha bila kusahau safari za nje ya nchi. Hapo hapo tuna TANZANIA FOOD & DRUGS AUTHORITY (TFDA) nao vile vile tiripu za nje kama kawa, VX za kutosha. Jamani tuoneeni huruma sisi walipa kodi maskini. TUMEROGWA??
Ni sahihi kuwa na bodi ya maziwa nchini. Tatizo kubwa ni kwamba kuna mama moja pale wizara ya mifugo alikuwa anaitwa kwa jina Susan ambaye alikabidhiwa mtoto akashindwa kumlea. Aliishia kuifanya ile Bodi mali yake. Sina uhakika kama bado yupo au keshatumbulia.

Nchi hii tuna maziwa mengi sana lakini wafugaji hawajajengewa uwezo hata kidogo. Maziwa yanakamulia mengi lakini hayana soko. Tunao wawekezaji wazalendo kama Tanga Fresh ambao wanajitahidi kula na wafugaji wa kila sampuli. Bakhresa alitakiwa pia anunuwe maziwa kutoka kwa wafugaji wanavyofanya Tanga fresh na ASAS. Utumiaji wa formula Milk wakati Tanzania kuna ngombe zaidi ya 20 inasikitisha sana.

Bodi ya maziwa izinduke kutoka usingizi wa pono na kuangalia urahisi wa kukabiliana na hizi changamoto katika sekta ya ufugaji na hasa sekta dogo ya mazao yatokanayo na mifugo kwa mfano maziwa. Mazao mengine ni ,....
 
Import maziwa yawe in form of powder, UHT or fresh nchini ndio utawatambua. Wanataka Tshs 2000 per ltr/kg kama ni ada zao ndio upate permit itakayokuruhusu kupata release ya kutowa mzigo bandarini. These guys are insane!
Hayo ni malipo ya wizarani. Wao utalipia 200 kea ltr/kg .wakikupa kibali ndio uandike barua kuomba kibali kingine wizarani kwa malipo ya 2000 .Jumla ni 2200

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahahaha tunayo bodi ya nyuki pia. Ila hii ni hapa kijiji kwetu. Sijui kama ngazi ya serikali kuu ipo.
 
Tupunguze/tuunganishe taasisi zinazofanana na MAJUKUMU jamani ili kubana matumizi & kuongeza ufanisi;
1. BODI YA MAZIWA/TFDA/TANZANIA FOOD & NUTRITION CENTRE
2. TANTRADE/EPZA
3.TIC/BRELA/National Economic Empowerment Council (NEEC)
4.TANAPA/Ngorongoro Conservation Area Authority (NCAA)
5. TACAIDS/ National AIDS Control Programme
6.OSHA/NEMC/ Zimamoto
7. Bodi za Mazao (korosho, chai, PARETO,Sukari, "CHUMVI" )
8.TBC/Habari-Maelezo/Tanzania Standard Newspaper (Daily News)
9. Tanzania Fisheries Research Institute (TAFIRI)+Mbegani Fisheries Development Centre
TANAPA na NCAA?
 
Jaribu kutafuta umuhimu wa maziwa kwa afya ndo utajua kwanin kuna bodi ya mazima!
Kuna watu toka tumeacha kunyonya hatutumii maziwa bodi hio ya nn halafu kama kila kitu chenye umihimu mwilini kinatakiwa kiwe na bodi tutaunda bodi za mayai,nyama,samaki hata maharage but kwa uelewa wangu mdogo hii bodi kama zilivyo bodi za sukari,pamba na korosho ingehusika na upataikanaji wa maziwa maslahi ya wafugaji na vikwazo vya kuuza maziwa nje ya nchi kama ipo na bado uzalishaji wa maziwa sio katika ubora na kiwango cha export ya maziwa bado sio cha kuridhisha means ipo kwaajili ya kuhimiza kunywa maziwa kitu ambacho kingefanywa na taasisi zingine kama wizara na upimaji wa usalama wa maziwa wapo TFDA
 
Back
Top Bottom