Bodi ya Bandari yamuondoa Kipande, Mwakyembe aizuia

Tafuteni nchi nyingine ya kwenda kuibia na sio tanzania tena bandarini chini ya Dr Mwakyembe,la sivyo subirini Dr Mwakyembe aondoke ndio muingine wizi wenu pale kwa sasa mmebugi men,kwanini mmezuia tracking system isifanye kazi kama kweli lengo lenu ni kuisaidia nchi?
Dr Mwakyembe,hakuna muda wa kupoteza,fukuza wote kuanza upya si ujinga,nyie wachache mnavoiba pale bandarini,mnawaumiza waliowengi na hii hakibaliki chini ya uangalizi wa Dr Mwakyembe na mtaondoka tu,no way out
Kinacho endelea hapa ni usanii from both sides they know, the port does not need that tracking system for efficiency purposes. Ndio maana wale waliomwagiwa kitumbua chao mchanga mara ya kwanza kutoka wizarani wanarudisha mashambulizi kwa kuizuia ya sasa kutumia mgongo wa organisation own policies.

Siku hizi ukituma mzigo wako kutoka UK kwenye bill of reading unapewa hiyo tracking namba na wewe, kwa hivyo mtumaji unaona meli ilipo mpaka mzigo unaposhuswa kwa hivyo for what purposes does TPA need the system.

Issue hapa ni kukomoana ulaji tu ambao ulikuwa auna faida, kibaya zaidi it is at tax payers expenses. Kama suala la upotevu wa mizigo hapo bandarini ni poor human supervisions suala ambalo clearly huyo DG bado ajalipatia ufumbuzi. Lakini tracking system is a service already provided by the shipper these days, well atleast from UK.
 
............semeni/tajeni ufisadi wa Mwakyembe ni upi?.......mijitu mingine aisee....msianze kupoteza lengo....labda mpige fitina Mwakyembe aondolewe.....lakini huyo jamaa atawashughulikia tu as long as yuko pale......

.....akina Lowassa & Co. naona wanatumia nguvu nyingi kweli.......inabidi mtumie akili kidogo.....maana mnajianika kiwazi wazi kabisa jinsi mnavyohangaika kwa kuwa madili yenu yanakutana na vigingi.......
 
Nakumbuka wakati wa uteuzi wa Kipande kulikuwa na tuhuma za uhusiano kati ya white hse na huyu Kipande, labda ndio maana Mwakyembe imebidi atafute consultancy ya white hse popote ilipo kabla ya kuchukua maamuzi.

Kipande,Kawambwa na Kikwete ni kitu moja! Mwenye akili jiulize nini kinaendelea na mahusiano ya hao watatu!
 
inaonekana wewe umetumwa na mgawe hapa jamvini au we ni kijana mtoto wake ada uliyokuwa ukilipia nje ya nchi imeisha na hakuna pa kuiba tena.....acha mwakyembe afanye kazi sisi ndio wananchi tunaona anafanya kazi akikosea tutamwambia na sio wewe kibaraka
 
Tina,
Asante kwa nondo hizi, zinairusha jf enzi zile tulipoikuta na kujiunga nayo!. Za moto moto kutoka jikoni!.

Mwaki ni "sensetionalist!".
Tangu CCJ ilipoasisiwa kuna kitu niliwaambia humu!.
Alipotishia kuwa anawindwa kuuwawa kuna kitu niliwaambia humu!.
Alipodai amenusurika kwenye ajali ya kuchonga kuna kitu niliwaambia humu!.
Alipotia ripoti nusu ya Richmond na kuuficha ukweli mkubwa zaidi, kuna kitu niliwaambia humu!.
Zitto aliposhauri tuinunue mitambo ile au tuitaifishe, yeye alipinga na kuna niliwaambia humu!.
Alipoteuliwa Naibu Waziri kuna kitu niliwaambia humu!
Alipodaiwa kuwekewa sumu, kuna kitu niliwaambia humu!.
Manumba alipoitoa ile medical report yake ya Apollo kuna kitu niliwaambia humu!.
Dr. Mwaki alipoibuka kudai ile sio medical report kuna kitu niliwaambia humu!.
Alipojidai atasema kila kitu kuna kitu niliwaambia humu!.
Aliporipoti na Sitta pale Kawe kwenye kanisa la Gwajima (mchungaji wa msafara wa Hammer 3!) na kutangaza amemwachia Mungu, kuna kitu niliwaambia humu!.
Tatizo la baadhi yetu humu, ni uwezo wa kutunza kumbukumbu na connecting the dots!.
Ukweli ni kuwa "he is not real!" so do Sitta!. Hata Magufuli ni action oriented but not real!. Membe ni boya!.
Mtu peke ambaye ni very genuine, very real!, na mtu wa vitendo vya ukweli, ni yule yule, "the one and only..."!
Naomba nisimtaje nisije kuharibu thread yako!.
Pasco.

Tatizo kubwa ya wabongo wengi ni kumbukumbu fupi kama Nyumbu! Na kwa kosa hilo CCM itatawala kwa kipindi kirefu hapa! Unazungumzia mambo ambayo mtu/watu makini wangekwisha mfuta Mwakyembe ktk list ya watu makini na wazalendo.

Huko nyuma nimewahi kupendekeza kwamba pengine ifike wkt kama unataka kugombea Urais na wewe ni waziri ktk serikali,basi ujiuzulu miaka 2 kabla ya uchaguzi ukajipange nje. Kuwaachia hawa jamaa ndiyo hivi tunashuhudia mambo ya hovyo kama haya,akina Membe wanachafua ujirani mwema na Nchimbi wanashindwa kuwaongoza Mapolisi!
 
Mafisadi waliokosa ulaji tangu mwakiembe aingie madarakani..alikuta bandari inaingiza sh.bil 3 kwa mwezi akaanza kwa kuwaondoa mkurugenzi mkuu na genge lake,kisha akasambaratisha bodi na kutafuta watanzania wanaotafuta kazi na ambao wako tayari kuitumikia tanzania.
tangu alipofika TPA mkurugenzi mpya aliwabana sana watendaji na baada ya miezi miwili pato la bandari lilipanda mara dufu toka bil 3 hadi bil.9,kwa mwezi.hakuishia hapo akawaweka watendaji wote karibu ili kurahisisha utoaji wa mzigo na kupelekea kupandisha pato la bandari toka bil 9 hadi 21 na hivi karibuni kafuta utaratibu wa kulipia pesa bandarini kwenye chumba maalum( strong room) na sasa pesa inalipiwa BOT na Bank M,bandari mteja anaenda ba pay in slip.kubadilika kwa mfumo huu kumeongeza pato la bandari toka bil.21 hadi bil 40 kwa mwezi. hivyo tangu mwakiembe ameshika wizara hii na kumweka huyo mkurugenzi mpya ambae mafisadi wanajitahidi kumchafua ,pato la bandari limeoanda toka bil 3 hadi bil 40 kwa mwezi.
Hii inamaana zaidi ya bil 37 ziliishia kwenye account za mafisadi huko uswiss kwa kila mwezi.ukali na ufuatiliaji wa mwakiembe ni threat(tishio) kwa wachumia tumbo.hali umekuwa ngumu bandarini.wizi wa vipuli vya magari unedhibitiwa na sasa kila kona ya mafisadi ni vilio.
My take:waandishi wa habari hususan magazeti naamini wite watanunuliwa ili waanze kumpaka matope mwakyembe kwa maslagi ya wezi .hata lowasa aliweza kuvinunua vyombo vyote vya habari kuanzia Uhuru,Tazama,mzalendo,Tanzania Daima,mawio,mwanahakisi na kila gazeti unalolijua wewe huta sikia tena likimwandika lowasa katika mtazamo hasi.
"the great weapon of the oppressor is the mind of oppressed"by late steven Bicco.
Tina, mleta mada tuthibitishie ukweli wa maelezo haya kama ndivyo hali ilivyokuwa na ilivyo kwa sasa
cc Pasco
 
Last edited by a moderator:
Tina taarifa hii inadhihirisha wewe ni mpenda majungu na ni mrongo mkubwa unaposema bodi ilitaka kumuondoa Kipande je wana bodi wote walikuwa na msimamo huo? bora mngejiuzulu mapema muwaache wenzenu wafanye kazi sio nyie kila kukicha majungu majungu. Kipande na timu yake wamefanya kazi kubwa na kuleta sifa kubwa kwa muda mchache waliokaa leo utwambie hafai kwa lipi? huyu mleta taarifa anayejiita Tina ameshagundulika wizarani ni mmoja wa wajumbe wa bodi jina lake kamili ni Hilderbrand Shayo anayejigamba ni afisa usalama wa taifa na anaripoti taarifa zake kwa bosi wake EMILIAN MWAGA!!!?huyu Shayo ndie anayeandika taarifa mbaya katika magazeti menge hasa gazeti la Kulikoni akimchafua Mwakyembe na Kipande.
 
Wangejiuzulu tu ili tujue kuwa wana uchungu na nchi yao na wala siyo wachumia tumbo;

Kipande ninayemfahamu toka enzi za rrm huko mbeya ni mtu ambaye yuko juu juu sana;
ana tabia ya kuanzisha jambo halafu halimalizii; linabaki likielea hewana na ananzisha lingine.
 
My take:waandishi wa habari hususan magazeti naamini wite watanunuliwa ili waanze kumpaka matope mwakyembe kwa maslagi ya wezi .hata lowasa aliweza kuvinunua vyombo vyote vya habari kuanzia Uhuru,Tazama,mzalendo,Tanzania Daima,mawio,mwanahakisi na kila gazeti unalolijua wewe huta sikia tena likimwandika lowasa katika mtazamo hasi.
Mkuu Mwobho, sio kweli kuwa yamenunuliwa ndio maana hayamripoti katika mtazamo hasi, bali sasa yameutambua ukweli halisi!. EL was framed kwenye Richmond and then condemed without being heard!. Kabla ya baraza jipya, Six ndie ilibidi awe PM ili JK akimaliza term yake, Six ampokee!. Kitendo cha JK kumteua EL, kilimaanisha baada ya JK ni EL na sio Six!. Richmond ilipoibuka Six akamtumia Mwaki kama nyundo kummaliza EL!. Ukumbuke Mwaki anajua fika Richmond ni ya nani, who was behind and the benefisiaries ni kina nani!, lakini walifanya scheme yao, na kumframe EL the final motive kumfuta kwenye sura za 2015 na mwanzo walifanikiwa!. The rest hata humu jf, were too blind to see including the media!, as times goes by, true visions zimeanza kuibuka, ukweli umeanza ku surface na media imelijua hili ndio maana sasa media zote ziko very positive kuhusu EL, kambi ya Six na scheme zao, imesambaratika kwa sababu kuna watu hawakujua it was a scheme!. Baada ya kushtukiwa, wakaandaa plan B (CCJ), nayo ikashtukiwa!.

Ndani ya CCM, kuna some few ambao ni "the wise ones!", licha ya kuwajua ndio the team behind CCJ, kazi ya kwanza ilikuwa ni lazima Six ang'olewe uspika. Kwa vile he is powerful na Mwaki ni very influential, don't let them loose!, they'll spit vernon!, kwa ile principle ya "keep your friends close, "your anemies closer!". Huo uwaziri Six na Mwaki kina Nape na Mwigulu kupewa vyeo CCM, wamepewa ili kuwa "contained!". Almost all CCJ team ukimuondoa Mpendazoe aliyejitoa kabla, wamepewa ulaji ili wawe watched very closely!.

Njia ya "The one and only" ni nyeupe!, he is as clean as water, the way is as clear as the the sky tatizo ni "afya tuu" kama kweli sio mgogoro!, siku za Mwaki, Six na wahaini wote ndani ya CCM ambao ni "chui" wakipose kama "kondoo" zinahesabika!.
Pasco.
 
Hiyo bodi siku zote ilikuwa wapi kusafisha madudu ya bandarini hadi waziri aingilie kati? Mi naona ni wasanii tu hao.
 
Tina taarifa hii inadhihirisha wewe ni mpenda majungu na ni mrongo mkubwa huyu mleta taarifa anayejiita.... ameshagundulika wizarani ni mmoja wa wajumbe wa bodi jina lake kamili ni ... anayejigamba ni afisa usalama wa taifa na anaripoti taarifa zake kwa bosi wake ....!!!?huyu .... ndie anayeandika taarifa mbaya katika magazeti menge hasa gazeti la Kulikoni akimchafua Mwakyembe na Kipande.
Mkuu Sabato Masalia, kwa sheria zetu humu jf, huruhusiwi kumtaja member yoyote ni nani, hii ni kosa la name calling na adhabu yake ni ban!. Nimekuhurumia sijakuripoti kwa kuamini hujui kuwa ni kosa!, edit bandiko lako kama nilivyoedit kwa kuficha majina ujumbe wako umeishatufikia!.
Pasco.
 
Bora hata Mrema, Mwakyembe ni zaidi ya Mrema Enzi za Unaibu Waziri Mkuu... Tutakuja kujua baadae.
Sisi ambao ni "trend readers" hili tumeishaliona siku nyingi!. Baada ya ripoti ya ile ile tume yake kutoka, nilitoa angalizo kuwa kanuni kuu ya kwanza ya haki na utawala wa sheria ni "no one is condemned unheard!". Nikauliza iweje mwanasheria huyu tena aliyebobea kuamua kutomhoji mtuhumiwa mkuu wa Richmond, ba badala yake kumcondem moja kwa moja?!. Kwa hili la bandari sasa wengi zaidi mtamwelewa vizuri, la TAZARA limeishamshinda!, akimaliza la bandari, ATCL na TRC vinamsubiri!, kuna mambo hayahitaji "sensionalism!", soon he'll prove failure!. Time will tell!.
Pasco.
 
Huyu Tina anadhihirisha chuki yake dhidi ya Mwakyembe na Kipande inamtia upofu, mwenye macho haambiwe tazama Watanzani mpaka wateja wa nchi za jirani ambao walikuwa wanaikimbia bandari yetu Dar kutokana na wizi uliokithiri enzi ya aki a Mgawe lakini kwa wanakubali kweli mabadiliko yaliyofanywa na Mwakyembe yameleta tija kubwa.

hongera sana Mwakyembe na Kipande endeleeni kuchapa mzigo hao wajumbe wachache wa bodi wanaolalama ni bora wangejiuzulu ingekuwa aula zaidi kuliko kuendelea kuwepo kwao kutaharibu utendaji na siri za vikao zitaendelea kuvuja.
 
Hii hoteli ni ya nani?

Ni Mwakyembe aliyeunda Kamati ya kuchunguza TPA ikilipwa fedha na TPA na kamati hiyo Mwenyekiti alilipwa 930,000 kwa siku, wajumbe 7+1 katibu kila mmoja 630,000 kwa siku na walilala na kupata huduma zote Hoteli Sourthen Sun USD 200 kwa siku (kulala tu) na walikaa kwa zaidi ya siku 60 na kuomba kuongezewa zaidi. Hadi leo ripoti ni siri maana imejaa majungu.
 
Pasco, wangelitaka kuinunua mitambo, nani angeliwazuia? Kaulize Mtwara na Gas yao.

Zitto aliposhauri tuinunue mitambo ile au tuitaifishe, yeye alipinga na kuna niliwaambia humu!.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom