Bodaboda mnawahi wapi?

Kalamu Nzito

JF-Expert Member
Aug 13, 2015
318
662
Leo kwa mara ya kwanza nimeshuhudia mtu anakata roho.

Ajali ya bodaboda na gari ndogo imetokea maeneo ya Kange kituoni mkoani Tanga majira ya saa tisa alasiri.

Bodaboda ame-overtake upande wa kushoto wakati gari ndogo ilikua inakunja kutoka barabara kuu kuelekea barabara ya vumbi huku dereva wa gari dogo akiwa amechukua tahadhari zote ikiwemo kuwasha indicator.

Bodaboda katoka na speed zote upande wa kushoto bila kujua kuna gari tayari inakunja kona mbele yake. Kijana akalivaa gari ubavuni upande wa mbele, akatupwa mbali na boda yake na kutua mzimamzima pembezoni mwa barabara.

Kwakua niilikua nyuma ya gari hilo dogo wakati ajali inatokea eneo, nilisogea mbele na kupaki pembeni kisha nikashuka kwenda kumtazama muhanga wa ajali ile. Damu zilikua zinamtoka kwa nyingi sana puani, mdomoni na masikioni.

Alikua katika mwendo wa kasi mno (takribani 80-100km/her) na mbaya zaidi hakua na helmet kichwani.

Shukrani zimuendee msamalia mwema mwenye gari zenye namba T*** EBN ambaye alijitolea kumkimbiza hospitali. Lakini kwa hali ilivyokua ni wazi kijana alikua amekwishakata roho.

Chondechonde vijana wa Bodaboda kuweni makini tafadhali.
 
Bila shaka gari ilikuwa inatokea Tanga Mjini na ilikunja kuelekea njia ya vumbi iendayo Kange Kasera na boda alikuwa ananyoosha kwenda Kange Stendi, Kituo Kikuu cha Mabasi, Tanga.

Hawa vijana wa bodaboda walishashindikana. Pikipiki mpya washaondoa side mirrors na kutoboa exhost ili ipige kelele.

Vijana wameshindikana nchi nzima hakuna wa kuwagusa.

Kwenye taa nyekundu wanapita, hawakai foleni.

Boda boda ni laana
 
Mimi siku hizi nawaogopa,maana nimeshawagonga sana,naona wanachonitafutia sasa ni kesi tu.Sasa hivi wamefikia mahali wanatoa taa kubwa ile ya original mbele wanaweka kitaa kimoja kidogo kina mwanga hafifu,yaani hata haijulikani wanataka nini...
 
Mimi siku hizi nawaogopa,maana nimeshawagonga sana,naona wanachonitafutia sasa ni kesi tu.Sasa hivi wamefikia mahali wanatoa taa kubwa ile ya original mbele wanaweka kitaa kimoja kidogo kina mwanga hafifu,yaani hata haijulikani wanataka nini...
Pia taa ya nyuma wanatoa wanaweka kidogo.

Usukani wanaupindisha unakua kama koleo la kung'olea meno.

Bure kabisa!
 
Leo kwa mara ya kwanza nimeshuhudia mtu anakata roho.

Ajali ya bodaboda na gari ndogo imetokea maeneo ya Kange kituoni mkoani Tanga majira ya saa tisa alasiri.

Bodaboda ame-overtake upande wa kushoto wakati gari ndogo ilikua inakunja kutoka barabara kuu kuelekea barabara ya vumbi huku dereva wa gari dogo akiwa amechukua tahadhari zote ikiwemo kuwasha indicator.

Bodaboda katoka na speed zote upande wa kushoto bila kujua kuna gari tayari inakunja kona mbele yake. Kijana akalivaa gari ubavuni upande wa mbele, akatupwa mbali na boda yake na kutua mzimamzima pembezoni mwa barabara.

Kwakua niilikua nyuma ya gari hilo dogo wakati ajali inatokea eneo, nilisogea mbele na kupaki pembeni kisha nikashuka kwenda kumtazama muhanga wa ajali ile. Damu zilikua zinamtoka kwa nyingi sana puani, mdomoni na masikioni.

Alikua katika mwendo wa kasi mno (takribani 80-100km/her) na mbaya zaidi hakua na helmet kichwani.

Shukrani zimuendee msamalia mwema mwenye gari zenye namba T*** EBN ambaye alijitolea kumkimbiza hospitali. Lakini kwa hali ilivyokua ni wazi kijana alikua amekwishakata roho.

Chondechonde vijana wa Bodaboda kuweni makini tafadhali.
Wanawahi kaburini
 
Leo kwa mara ya kwanza nimeshuhudia mtu anakata roho.

Ajali ya bodaboda na gari ndogo imetokea maeneo ya Kange kituoni mkoani Tanga majira ya saa tisa alasiri.

Bodaboda ame-overtake upande wa kushoto wakati gari ndogo ilikua inakunja kutoka barabara kuu kuelekea barabara ya vumbi huku dereva wa gari dogo akiwa amechukua tahadhari zote ikiwemo kuwasha indicator.

Bodaboda katoka na speed zote upande wa kushoto bila kujua kuna gari tayari inakunja kona mbele yake. Kijana akalivaa gari ubavuni upande wa mbele, akatupwa mbali na boda yake na kutua mzimamzima pembezoni mwa barabara.

Kwakua niilikua nyuma ya gari hilo dogo wakati ajali inatokea eneo, nilisogea mbele na kupaki pembeni kisha nikashuka kwenda kumtazama muhanga wa ajali ile. Damu zilikua zinamtoka kwa nyingi sana puani, mdomoni na masikioni.

Alikua katika mwendo wa kasi mno (takribani 80-100km/her) na mbaya zaidi hakua na helmet kichwani.

Shukrani zimuendee msamalia mwema mwenye gari zenye namba T*** EBN ambaye alijitolea kumkimbiza hospitali. Lakini kwa hali ilivyokua ni wazi kijana alikua amekwishakata roho.

Chondechonde vijana wa Bodaboda kuweni makini tafadhali.
Kwa mweli sie bodaboda inabidi tuwe makini sana maana mwili bodi. Asante kwa kutukumbusha tutachukia tahadhari zote
 
Back
Top Bottom