Bodaboda mnawahi wapi?

Bodaboda mnawahi wapi?

Wewe kazi gani hulipwi mpaka upumuliwe kisogoni.Lema alikuwa sahihi bodaboda ni LAANA.
 
Hawa watoto wengi wao bangi haziwapendi kabisa. Mtaa ninaoishi wanasumbua mpaka basi. Yaani muda wote ni kelele, na kupita kwa mwendo kasi!!
Na wanakufa kweli kutokana na huu ujinga wao!! Lakini hata hawajali.

Kiukweli kuna bodaboda wachache sana wenye akili timamu.
Ni hatari kwa Taifa. Mimi ninadhani pikipiki zipandishiwe ushuru mara nne ili ziwe ghali kama bajaji au zaidi ili kupunguza madhara kwa jamii.

Kabla ya Mchina kumwaga pikipiki nchini Mjapani ndiye alikuwa anaongoza kwa kuuza Yamaha kwa bei sawa na gari ndogo na kipindi hicho usafiri wa pikipiki uliheshimika kama wa gari.
 
Ni hatari kwa Taifa. Mimi ninadhani pikipiki zipandishiwe ushuru mara nne ili ziwe ghali kama bajaji au zaidi ili kupunguza madhara kwa jamii.

Kabla ya Mchina kumwaga pikipiki nchini Mjapani ndiye alikuwa anaongoza kwa kuuza Yamaha kwa bei sawa na gari ndogo na kipindi hicho usafiri wa pikipiki uliheshimika kama wa gari.
Tatizo na serikali yenyewe ndiyo inapata unafuu kwa kiasi fulani. Maana hawa watoto wasingekuwa na shughuli za kufanya, wengi wao wangekuwa ni vibaka na wezi mtaani.

Mimi nashauri wangepewa semina za mara kwa mara ili wajitambue. Maana wengi wao wakishapata tu hesabu yao ya siku; basi kinachofuatia kuanzia hapo ni kuchezea tu mafuta, kunywa pombe na kuvuta bangi.

Ni bodaboda wachache sana ndiyo wana malengo. The rest ni vurugu tu mtaani.
 
Tatizo na serikali yenyewe ndiyo inapata unafuu kwa kiasi fulani. Maana hawa watoto wasingekuwa na shughuli za kufanya, wengi wao wangekuwa ni vibaka na wezi mtaani.

Mimi nashauri wangepewa semina za mara kwa mara ili wajitambue. Maana wengi wao wakishapata tu hesabu yao ya siku; basi kinachofuatia kuanzia hapo ni kuchezea tu mafuta, kunywa pombe na kuvuta bangi.

Ni bodaboda wachache sana ndiyo wana malengo. The rest ni vurugu tu mtaani.

Hiyo semina hawawezi kuelewa kwa sababu kitendo cha kuendesha pikipiki muda mrefu ni ulevi tosha.

Petroli inavuja kupitia mfuniko wa tenki na kuingia puani kisha kichwani na kuwalewesha ndiyo maana wengi wana wenge. Muda mwingi wamekaa kwenye pikipiki hata kama wamepaki.
 
Kuna mmoja kagonga mtoto juzi kwa speed za kipumbavu kwenye barabara ya vumbi ni mbovu lakini ana pita speed, tume piga makofi hadi akawa mwekundu nazani ali hadithia wenzake.

Na wana penda kupita njia za waenda kwa mguu wana acha lami. Hawa sha sema nki mfuma ana nipigia honi kwa nyuma ni makofi tu ..pale ubungo Riverside sha piga makofi mmoja ali nipigia honi kidogo moyo uchomoke
Mr Devil 😂
 
Kuna mmoja kagonga mtoto juzi kwa speed za kipumbavu kwenye barabara ya vumbi ni mbovu lakini ana pita speed, tume piga makofi hadi akawa mwekundu nazani ali hadithia wenzake.

Na wana penda kupita njia za waenda kwa mguu wana acha lami. Hawa sha sema nki mfuma ana nipigia honi kwa nyuma ni makofi tu ..pale ubungo Riverside sha piga makofi mmoja ali nipigia honi kidogo moyo uchomoke
Haha
 
Hv hawa jamaa kwa nini huwa wanang'oa hizo side mirrors? Cha ajabu na polisi wa usalama barabarani wanawatazama tu
Lakini kwenye gari Hata kama side mirror ina kreki ndogo tu faini
 
Unajuaje labda huyo msamaria mwema ni yeye ila hakupenda kujianika utambulisho wake?
Umeona kaficha namba ya gari?
Kwaiyo wewe huna usamaria wema uongo? Uliona kupakia huo mzoga kwenye hicho ki rahum chako kwamba kingeisha mafuta au unakuja kueleza unoko hapa,hata picha hujaweka....
 
Bodaboda wengi mama zao ni vijana.
Wao wakifa mama zao watapata mimba nyingine(replacement)
 
Serikali haiwezi fanya chochote kuhusu bodaboda, kwasababu haya yanayotokea ndio hasa serikali inachotaka.

Boda boda priority zao ni ;
1. Kupata hesabu
2. Kubeti
3. Pombe
4. Ulevi mwingine kama bangi
5. Mademu
6. Matumizi yasiyo ya msingi.

Hawafikirii maendeleo ya maisha yao au maisha yao ya baadae.

Mwisho kabisa, hawafikirii maendeleo ya taifa lao maana muda huo hawana na pia sio priority yao. Total mind distraction.

Hebu fikiria hawa boda boda wote wangekuwa hawana ajira, wako mitaani wanapigwa na njaa kali ya maisha, katiba mpya ingekua haijapatikana mpaka leo? njaa zingewafungua akili wangedai haki zao, hata mapinduzi wangefanya amini nakwambia, maana asilimia kubwa ya idadi ya watu Tanzania, ambao ni wapiga kura ni vijana.

Kwaiyo hapo serikali haitafanya lolote, na wataendelea kupagawa na kupoteza maisha tu, kwasababu hicho ndicho serikali inataka.

Huo ndio ukweli wenyewe.
 
Nabwanawake ndio wateja wao wakubwa, unakuta kidada kiko kwenye bodaboda kimetulia wala hakina habari, kinachart na simu mda wote kikiwa na uhakika kiko salama!! Boda ni usafiri hatarishi mda wote
 
Leo kwa mara ya kwanza nimeshuhudia mtu anakata roho.

Ajali ya bodaboda na gari ndogo imetokea maeneo ya Kange kituoni mkoani Tanga majira ya saa tisa alasiri.

Bodaboda ame-overtake upande wa kushoto wakati gari ndogo ilikua inakunja kutoka barabara kuu kuelekea barabara ya vumbi huku dereva wa gari dogo akiwa amechukua tahadhari zote ikiwemo kuwasha indicator.

Bodaboda katoka na speed zote upande wa kushoto bila kujua kuna gari tayari inakunja kona mbele yake. Kijana akalivaa gari ubavuni upande wa mbele, akatupwa mbali na boda yake na kutua mzimamzima pembezoni mwa barabara.

Kwakua niilikua nyuma ya gari hilo dogo wakati ajali inatokea eneo, nilisogea mbele na kupaki pembeni kisha nikashuka kwenda kumtazama muhanga wa ajali ile. Damu zilikua zinamtoka kwa nyingi sana puani, mdomoni na masikioni.

Alikua katika mwendo wa kasi mno (takribani 80-100km/her) na mbaya zaidi hakua na helmet kichwani.

Shukrani zimuendee msamalia mwema mwenye gari zenye namba T*** EBN ambaye alijitolea kumkimbiza hospitali. Lakini kwa hali ilivyokua ni wazi kijana alikua amekwishakata roho.

Chondechonde vijana wa Bodaboda kuweni makini tafadhali.
Tatizo la bodaboda kule kupatia mara moja wanafikiri mara zote wataendelea kupatia
 
Unajuaje labda huyo msamaria mwema ni yeye ila hakupenda kujianika utambulisho wake?
Umeona kaficha namba ya gari?
Sie tunamfahamu huyo mwamba kwa post za majigambo na spika alizonazo,hawezi kukusaidia asijitangaze/asikutangaze
 
Back
Top Bottom