Mwendesha Bodaboda, kama unapenda kuishi, pitia hapa!

Mparee2

JF-Expert Member
Sep 2, 2012
2,639
4,387
Kutokana na changamoto za waendesha Pikipiki, nimeona niwakumbushe tena kwani wengi hufanya mzaha barabarani bila kujua kuwa Mwili wao ndio bodi ya pikipiki!

1. Usikae ubavuni mwa gari, kwa kuwa hutajua maamuzi dereva wa gari anayotaka kufanya. Gari inaweza kupinda kushoto au Kulia bila wewe kufaham - Utagongwa!
2. Usiendeshe katikati ya Barabara kwa kuwa magari yanakimbia sana hivyo unayazuia kuovertake - utagongwa
3. Usiovertake gari na kukaa mbele yake huku ukipunguza mwendo; utagongwa. Ukiovertake gari, ongeza mwendo au sogea kushoto kabisa mwa barabara
4. Usiendeshe bila vioo vya pembeni (side mirror mjini) kwani hutaona gari linalokuja nyuma- utagongwa!
5. Usiendeshe kwa kupanga msitari (moja nyuma ya nyingine) katikati ya Barabara. Mnaweza kuendesha hivyo ila iwe kushoto kabisa mwa barabara.
6. Usichomekee gari ukitegemea lisimame/lipunguze mwendo, sio magari yote yenye break za karibu kama pikipiki. Majuzi hapa mmoja kafa pale Msamvu/Moro kwa ujinga wake
7. Ukiona gari limesimama, usipite kabla ya kujua kwa nini limesimama; unaweza kuta limesimama kupisha gari jingine liingie barabarani...utagongwa!
8. Usibebe mzigo unaopita sana pembeni mwa pikipiki (mbao, mabati, bomba nk) ukiguswa tu kidogo, utasokotwa kama pia, ukipona shukuru Mungu.

Muhimu:
1. Endeshea kushoto (pembeni kabisa mwa Barabara) muda wote, kumbuka magari yanakimbia sana kuliko Pikipiki hivyo ukiwa kushoto/pembeni, yataweza kukupita/kukukwepa bila shida.
2. Narudia tena - endeshea kushoto kabisa mwa Barabara... Pikipiki inaweza tu kuyapita magari kwenye msongamano, au Barabara mbovu za vumbi ila sio highway (Barabara kuu)
 
Na kapicha kakusindikizia uzi
1000049777.jpg
 
Kutokana na changamoto za waendesha Pikipiki, nimeona niwakumbushe tena kwani wengi hufanya mzaha barabarani bila kujua kuwa Mwili wao ndio bodi ya pikipiki!

1. Usikae ubavuni mwa gari, kwa kuwa hutajua maamuzi dereva wa gari anayotaka kufanya
2. Usiendeshe katikati ya Barabara kwa kuwa magari yanakimbia sana hivyo unayazuia kuovertake - utagongwa
3. Usiovertake gari na kukaa mbele yake huku ukipunguza mwendo; utagongwa
4. Usiendeshe bila vioo vya pembeni (side mirror mjini) kwani hutaona gari linalokuja nyuma- utagongwa!
5. Usiendeshe kwa kupanga msitari (moja nyuma ya nyingine) katikati ya Barabara. Mnaweza kuendesha hivyo ila iwe kushoto kabisa mwa barabara.
6. Usichomekee gari ukitegemea lisimame/lipunguze mwendo, sio magari yote yenye break za karibu kama pikipiki. Majuzi hapa mmoja kafa pale Msamvu/Moro kwa ujinga wake
7. Ukiona gari imesimama, usipite kabla ya kujua kwa nini imesimama; unaweza kuta imepisha gari nyingine iingie barabarani...utagongwa!
8. Usibebe mzigo unaopita sana pembeni mwa pikipiki (mbao, mabati, bomba nk) ukiguswa tu kidogo, utasokotwa kama pia, ukipona shukuru Mungu.

Muhimu:
1. Endeshea kushoto (pembeni kabisa) mwa Barabara muda wote, kumbuka magari yanakimbia sana kuliko Pikipiki hivyo ukiwa kushoto/pembeni, yataweza kukupita/kukukwepa bila shida.
2. Narudia tena - endeshea kushoto kabisa mwa Barabara... Pikipiki inaweza tu kuyapita magari kwenye msongamano, au Barabara mbovu za vumbi ila sio highway (Barabara kuu)
usitumie honi hovyo hovyo au kama ndio break yako wengi wakigonga gari, bajaji au guta wanakua kwenye honi 🐒

kuna kale kamchezo hatari ka kwenye mataa 🐒

magari ya upande fulani yamesima kuheshimu taa za kuongoza magari, ya upande mwingine yameruhusiwa na yanapita kwa kasi sana.

sasa unakuta makomandoo, maafisa usafirishaji na bodaboda yanakatisha kwa kukadiria, eti aah lile gari linalo kuja kwa kasi sana, liko mbali nitaliwahi nikivuka kwa kasi🐒

ule mchezo pia ni hatari, waache mara moja 🐒
 
Hawa watu wanakufa sana,kama traffic wangekuwa wanatoa takwim ya nchi nzima ya kila wiki,watu wangeogopa hata kupanda hzi bodaboda,cjui tumekosea wapi kama taifa kwenye huu usafiri,unasaidia sana na sometimes hata ukiwa na gari unakusave pale unapokuwa na haraka.hawa vijana wanaoendesha hzi boda wamulikwe kwa jicho kali.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom