Bob Marley aliamini Mungu kweli?


Nakubaliana nawe mkuu, get up stand up ni kama aliona namna watu wanavoingia mkenge na kuvizwa fikra kwa sababu ya dini (kumbuka kama Tosh alikuwa mwimba kwaya).Dini hapa ilionekana wazi kutumika (tunaona hata Africa,,ujaji wa missionaries and the spread of"word of God"),Ndiyo maana wanasema "You preacher man....", "Most people think that God will come from the sky......" ni mafundisho wahubiri walikuwa wakiyatoa wakiaminisha watu kuna siku ya mwisho ambapo atashuka na mawingu(Bwana) na kutwaa watu,,matokeo yake watu walikuwa wanaelekea zaidi ktk mentally slavery ya hatari!!
 
Ila watu..! Kwa hiyo we kiranga unataka kila mtu aamini unachoamin? Track ni ya ukwel. Nadhani ulitaka usikie unayowaza but tafakari. The man was an african spiritually. Na hata mimi naponda dini zenu
 
Everybody belive in GOD in different manner that why other call him,ALLAH,JAH,JESUS GOD,BUDHA,INDUS E.TC.We Africans we have been planted by the image of JESUS GOD Philosophies of which made us think other belives are devor philosophies which is not true that why whoever go beyond Jesus philosophy must be...............and should be.....
Lastly every man have right to decide on his/her destiny regards everything on earth without distubing others.
 
Kiranga katika maisha ya kiujumla ya Bob Marley ni wapi pengine ama alitamka au aliimba kuonyesha hamuamini Mungu?
Unataka kutuaminisha kuwa kwa mashairi hayo tu ya Peter Tosh basi ni ushahidi kuwa Bob alikuwa hamuamini Mungu?
Maana umejaribu kutengeneza picha ionekane alichoimba Peter Tosh ndio masimamo wa Bob kitu ambacho si cha kweli kabisa, kila mtu ana uhuru wa kuimba kile anataka na si mkuu wa bendi anaamua uimbe nini

Kimsingi maisha ya Bob kiujumla yalitawala kuonyesha atambua na kuamini uwepo wa mungu kupitia dini zake, na ndio maana hata katika maongezi yake alimtaja sana, alitembea kila mahali na Bibilia na ana nyimbo zaidi ya 20 zinazo mtaja Mungu ama zina tumia mistari ya kitabu hicho kitakatifu cha Bibilia..............je haya yote yamefutwa na mistari ya Peter Tosh. I DONT THINK SO

Anyway maswali ya msingi ni tujiulize je Bob Marley alikuwa anafuata imani gani?............
Alianza kuwa mkristo kwa kuzaliwa
Kisha akafuata imani ya Rastafarian
Na mwishoni kabisa akabatizwa kuwa mkristo siku chacha kabla ya kifo

Kimsingi imani zote alizopitia zinatambua na kuamini katika Mungu kwa njia tofauti(hata wasabato,waroma, jehova witness wanaamini katika Mungu na kitabu kimoja lakini katika misingi tofauti)
Rastafarian wanaamini katika Mungu kupitia zaidi kwenye Agano la kale na wanamisingi yao

Nadhani si sahihi ku conclude ati Bob alikuwa haamini katika Mungu kwa msatari huo wa Peter Tosh badala ya kuangalia historia nzima ya maisha yake na kile alicho kiamini na namna hicho alicho kiamini kilivyo effect maisha yake hadi kwenye nyimbo zake, matendo yake nk
 
Last edited by a moderator:

"Everybody" is such a sweeping generalization, wewe umejuaje hili? Una ushahidi gani kwamba kila mtu anaamini mungu?

Mbona mimi siamini katika kuwako kwa mungu?
 
paulss

Kuna watu wanaamini katika mungu kimila zaidi. Huwezi kutaka kuwa rais wa Marekani, au Papa au muimbaji mkubwa wa Reggae, halafu ukasema huamini mungu. Utakuwa unanyea kambi. Ndo maana utakuta katika mi chant ya "Jah Rastafari" unapenyezewa lyrics kwamba habari za mungu ni geresha za wachungaji tu, mwenye masikio na asikie. Sasa hayo makanisa yote unayoyasema kuanzia hilo la Ethiopian Orthodox alilobatizwa mpaka Rome huko, wote ndo hao preachers aliowalambast.

Mtu anayeamini katika mungu "per excellence" hawezi kuweka mistari kama hiyo katika wimbo wake, na wala hawezi kubatizwa kiharakaharaka kwenye deathbed ili kusudi hata watakaohoji uratsa wake baadaye wambiwe "yule alikuwa Rasta mpaka kubatizwa kabatizwa Ethiopian Orthodox". Kama aliamini mungu maisha yake yote kwa nini aende kubatizwa kwenye deathbed?
 
Last edited by a moderator:

Kwa sababu Ethiopian Orthodox ni kanisa la H.I.M HAILE SELASSIE ambaye bob alimuona kama ni Mesiah King. Na utambua kuwa Bob alisema. Kubatizwa E.O.T.C haimaanishi he is not a rasta. ALL rastas believe in God as Jah/YHWH/JAHOVIA the God of Iesraeli. Rastas wanaposema 'personal God' wanamaanisha falsafa ya ''I and I''. Kwamba spirit of God is Inside me, thats why nikikutendea ubaya nimemtendea na Jah kibaya kwa kuwa roho yake ipo ndani ya kila mwanadamu. Thats why All people are equar, regardless religion or race. Boa Alikuwa anaamini Mungu yupo, na alikuwa msomi mzuri wa bible na mistari yake mingi alikopi kwenye bible. Hii topic tulishaimaliza, someni comments za kale kwa ufahamu.

Most of Rastas wanabatizwa Katika Ethiopian Tewahedo kwa kuwa ni kanisa la H.I.M. Mfano Peter Tosh na mimi, but sio lazima kubatizwa huko, ni uamuzi wa mtu.
 
Last edited by a moderator:

Falsafa ya "I and I" na "the spirit of god is inside me" ukiiangalia kwa jicho la tatu utagundua inakataa kumuamini mungu aliyeko mbinguni, na inakuambia kwamba man is as close as you can get to god, hence "I and I" I moja ni mungu, na nyingine ni mimi, na mimi ndiye mungu (kwa maana mwenye mamlaka juu ya mazingira kwa kiwango cha akili yangu) kwani hakuna mungu wa mbinguni.

Kwa hiyo inamtaka mtu achukue personal responsibility, atafute uzuri hapahapa duniani badala ya kusubiri ahera ambayo haipo.

Kuna wasomi wa theology wanasema hata Yesu alipojiita "mwana wa mungu" hakumaaanisha kwamba uana wa mungu wake ni special in any case, na kwamba binadamu wote ni "wana wa mungu". Fumbo kubwa, kwa sababu kama hakuna mungu, na mungu kasemwa ontologically na Anselm kwamba ni the idea of the greatest good, basi duniani the epitomy of that wonder is found in man's ability to reason, hence "mwana wa mungu". Wewe na mimi. I and I.

Ukishamkataa mungu anayekaa mbinguni na kumpitisha mungu aliye ndani yako, kusema "spirit of god" ni humility tu, what you really mean is man's reason is supreme among the known and empirically falsifiable processes.

But if you know what life is worth,
You will look for yours on earth:

Anayeamini mungu wa ukristo anaukana ulimwengu huu na kufikiri uzima wa milele mbinguni, Bob anaenda kinyume na kanisa anasema sahau habari ya mbingu, anza hapahapa duniani kula good time na kuishi vizuri.

Na kuwa msomi mzuri wa Bible hakumaanishi kwamba unaiamini sana kama vile kuwa msomi mzuri wa riwaya za Shakespeare hakumaanishi kwamba unaziamini sana.

Kwa hiyo wewe rasta unaamini Haile Selassie mungu?
 

Nimekusoma na nimekuelewa kwa umakini mkuu.

Kasome vizuri falsafa ya I'nI utaelewa maana hujaitambua bado. Kwa kifupi, Roho wa Mungu yupo ndani ya kila kitu, unapoambiwa ure the image of God, haina maana una kichwa, miguu au sura kama ya Mungu, bali Tunatambua Mungu ni Roho, hana sura, hana mwili wala haonekani, hivyo u have the image/roho wa Mungu ndani yako na wakristu wanatambua maana ya Roho Mtakatifu, ni roho wa Mungu ambaye anakaa ndani Yetu, sema tunatofautiana kumtambua na kumtumia. Kama huamini uwepo wa Roho wa Mungu ndani ya mwanadamu is up to you, hujalazimishwa, unaweza kuendelea kuamini Mungu yupo tu angani/mawinguni.

Kusoma Biblia sio njia ya kuokoka, i know that, unaweza ukaisoma mwanzo mpaka mwisho ukapata Negative thoughts, kama hujakubali Roho wa Mungu ndani yako akuongoze.

Kwa kukujibu simple, Im a Nazarite, who follows laws of Judaism.
I believe in YHWH, i believe in YAHSHUA. Also I RESPECT the root of king DAVID, God alishasema ''He will sit on the throne of David'' kuwatetea watu wake mpaka mwisho wa dunia.
I Respect Ethiopian Monarch which came from Solomon and Queen Makheda. I honour Ethiopia as a blessed place with the Ark Of Covenant and the origin of Mankind (Im Archaeologist, i understand that) and Much respect also to Lalibela.
I respect humanity, mother Earth, Africa, My body as first temple, with Love and being Natural.
That is my spiritual lifestyle

ONLY YHWH CAN JUDGE ME, NOT ANY HUMAN BEING.

Respect!
 

Hapo umeongea vema watu wanamchukulia mungu kwa uwezo wao wa kufikiri, Mungu ametumba na ubongo na uhuru wa kutumia bongo zetu ilitujiandalie better life na kama angetuumba akaweka kila kitu sawa kwa au kama robot hata tusingefurahia maisha.
 

Kwanza, kuiita expression ya "I n I" falsafa ni kuipaza.

"Roho" ni lugha ya ushairi zaidi kuliko uhalisi. Ndiyo maana yenyewe na dini/ falsafa inayotokana nayo inaweza kuwa kitu chochote kwa mtu yoyote.

Kwa mujibu wako mungu hajulikani na binadamu, lakini hapo hapo binadamu wameweza kujua kwamba wao ni mfano wa mungu, wamejuaje? Wakijua kwamba wanafanana na mungu basi maana yake mungu anajulikanika, mungu akiwa hajulikaniki ki hivyo maana yake hata wanadamu wanaosema wameumbwa kwa mfano wa mungu ni wazushi tu.

Roho wa mungu utamjuaje wakati roho hajulikani kibinadamu?
 

Maisha ya Bob Marley ndiyo yaliyozaa mashairi yake. Akiwa upande wa mtu mweusi daima aliumizwa na namna maisha ya mtu mweusi yalivyokuwa mabaya kutokana na mfumo gandamizi uliojengwa kwa miongo na miongo. Katika wimbo huu ana wa hamasisha Watu weusi kupigania haki zao pasipo kujali ni ghiriba gani wanayoletewa na wahubiri wa uongo. Kutokana na kuwa dini ilitumiwa na Mzungu kama chombo cha kuendeleza mfumo gandamizi, Bob Marley hakusita kuwashambulia wahusika kwa wimbo huu.
Kwa hiyo suala la Bob Marley kuamini katika Mungu binafsi silioni kupitia wimbo huu mmoja ambao nimeutolea mantiki yake hapo juu. Kuna nyimbo zake nyingi sana zenye kuonesha alivyokuwa karibu na Mungu kiasi cha Mungu kutomtupa na kumfanya icon kwa kumshushia mashairi yenye hekima, na mafunzo ya kupendana kama wanadamu. Mfano wa baadhi ya nyimbo zake nyingi kuhusu Mungu ni kama Give thanks and Praise, Jah Live, Thank you Lord, Positive Vibration,One Love, God of all Ages, n.k.

Nadhani ni vyema kutomuhukumu Bob kwa wimbo huo mmoja na badala yake fikiria nyimbo nyingine makumi kwa makumi (kama sio nyimbo basi katika moja ya nyimbo zinginezo utakuta mistari yenye kuonesha hofu yake na ukaribu wake pia na Mungu).
Aksante, Amani na Upendo na viwe nawe.
 

Shukuran mkuu,

Unajua wasanii wakubwa wana namna yao ya kutoa jumbe zilizojificha ndani ya jumbe. Ndo maana unaweza kuangalia mchoro wa Da Vinci kwa juu juu usipate maana, baadaye ukatafsiriwa ukaambiwa hapa kuna maana ndani ya maana.

Ukiamini kwamba Bob Marley anaamini katika mungu kwa sababu ya nyimbo zake hizo nyingine, basi ni lazima utatizwe na Get Up Stand Up. Unless useme Bob alikuwa ana appease the religious massive in Jamaica, alipochoka akajionyesha makucha yake halisi katika "Get Up Stand Up".
 

Either god is infinitely unknowable due to being infinitely perfect or knowable.

If god is infinitely unknowable, any notion you may have of god is wrong.

If god is knowable at all, by virtue of being knowable and comprehensible by the human mind, he cannot be the pinnacle of perfection (infinitely perfect) and therefore he cannot be god.

Either way, your notion of god is wrong.

And of course there is the argument for the non existence of god.
 
Ila watu..! Kwa hiyo we kiranga unataka kila mtu aamini unachoamin? Track ni ya ukwel. Nadhani ulitaka usikie unayowaza but tafakari. The man was an african spiritually. Na hata mimi naponda dini zenu

To the contrary, mie sitaki mtu yeyote aamini at all.
 
For all we know Bob was using "God" as an euphemism for "Good" "Justice" "Truth"....

Na ndiyo maana alikataa habari za kusubiri uzima wa milele mbinguni.
 

Nadhani hapa mkuu umeongea Point. Badala ya mtu kukaa na kumuhuku Bob na kusahau mengine mengi ni kama kupoteza tu muda. Nakumbuka kuna nyimbo kama

Thank you Lord,
Jah Live,
Exodus,
Rat Race,
Sun is shinning,
Afrika unite,
One Love,
Give Thanks And Praise,
Forever Loving JAH,e.t.c

Kama mtu unamsikiliza Tuff Gong na msikilizaji wa nyimbo zake huwezi kusema Bob hakumuamini Mungu (Jah).
 
For all we know Bob was using "God" as an euphemism for "Good" "Justice" "Truth"....

Na ndiyo maana alikataa habari za kusubiri uzima wa milele mbinguni.

Hahahahahaaa. Mkuu now ndio nimekuelewa. Kumbe unalazimisha kuwa Tuff Gong alikuwa anaamini unachokiamini wewe? Angekuwa anaamini hivyo Asingeitwa Rasta, NEVER!
 
Hahahahahaaa. Mkuu now ndio nimekuelewa. Kumbe unalazimisha kuwa Tuff Gong alikuwa anaamini unachokiamini wewe? Angekuwa anaamini hivyo Asingeitwa Rasta, NEVER!

Ukisema nalazimisha wakati ushaambiwa "for all we know" unatulazimisha tu doubt intelligence yako.

Halafu Tuff Gong hawezi kuamini ninachoamini mimi kwa sababu mimi siamini.

Asingeitwa Rasta? Rasta ni nini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…