Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 16,987
- 20,271
Uandishi wa Kitabu cha Marehemu Regia Mtema (Biography)
Kamati Teule iliyochaguliwa kuanzisha Taasisi ya Regia Mtema Foundation imedhamiria kufuatilia kuandikwa kwa kitabu cha Marehemu Regia Mtema kufuatia azimio lililoafikiwa katika kikao cha kwanza cha Marafiki wa Regia pale British Council na baadaye kuwekewa uzito katika kikao cha Kamati Teule.
Kamati Teule sasa inapenda kutoa fursa ya kualika mtu au kampuni yeyote ambayo inaweza kuifanya kazi hiyo ya uandishi kwa uharaka, ustadi na ubora wa hali ya juu. Itahitajika kujua mchanganuo wa gharama zote za zoezi zima.
Kazi hii inatarajiwa itahusisha kuweka kumbukumbu ya historia ya Regia, Kazi mbalimbali alizofanya, picha nk. nk.
Kama wewe ni mojawapo wa waandishi wa Biography au unamfahamu yeyote, tafadhali naomba tuwasiliane moja kwa moja kwa PM au kupitia barua pepe sam@danimex.com.
Mkuu asante sana, sasa mwangaza wa taasisi ya ndugu yetu kipenzi Regia naona inatimia! Umoja tulionao uendelee hivyohivyo!