Aisee pole sana ila watu tuko tofauti mno. Mie sikulelewa na baba na hata alipojitokeza nikiwa chuo kikuu sikumshobokea wala mpaka leo sina muda nae ila naamini nitamsamehe siku moja. Sijawahi kujiskia upungufu kwa kutokua na baba. Najiona mtu wa kawaida, nimekamilika. Nilipendwa sana, sana na babu na bibi, wajomba na mama wadogo. Babu alikuwa ndo babangu, bibi mama yangu, mama mlezi wangu. Shukrani za pekee ziwaendee hawa watu, ila mama namshukuru zaidi. Upendo wake siwezi kuufananisha na kitu. Alijinyima vingi mno kunifurahisha na kuhakikisha nakuwa na "future" nzuri. Wakati wewe unawaasa watu (baba na mama) walee watoto kwa pamoja mi nawaasa wababa na wamama wanaojikuta peke yao kwa kutelekezwa, kutalikiwa au kufiwa au kwa sababu nyingine yoyote wafunge mkanda wawape watoto wao malezi mema.
Acha kuhuzunika kwa vitu ambavyo huwezi kuvidhibiti. Si ajabu ungelelewa na huyo baba hapa ungetoa maoni ya kuwaonea wivu wanaopendwa na baba zao kwa sababu baba yako ni kimeo (analewa, anampiga mama yako, hakukupeleka shule, kakunajisi, kakulaza njaa, yuko busy na kazi hamuonani n.k). Na si ajabu baba yako yuko hivyo ndo maana hujui aliko wala hajui uliko - hana sense ya kuwajibika (nimesema labda). Kakuambia nani baba yako angekuwa kama wa Kichunafk? We una mama unalalamika huna mtu wa kumwambia shkamoo baba. Hilo tu linakukosesha raha ya maisha wakati kuna mayatima wamepigana katika uyatima wao wameyashinda maisha na sasa ni watu wenye furaha kuliko wenye wazazi wote wawili. Kwa kuwa hayuko najua utasema baba ni baba tu hata kama zembwela. Kila kitu ni namna unavyokichukulia. Unaweza kabisa kuacha kulia. Pole tena.