Uhusiano wangu na baba yangu ulikuwa wa kipekee, Mimi ndo binti pekee katika familia yetu basi Mzee alinidekeza hadi basi, full kubebwa hadi jitu zima, alinifundisha kusoma na kuandika manake huko vidudu nilikuwa sielewi, Hadi kidato cha tatu nilikuwa nafuliwa uniform na Mzee.
Yani nilikuwa namjua akifurahi au akikasirika, na kuna kipindi ulitokea mgogoro kati yake na mama so akawa anachelewa kurudi ( ilikuwa sio kawaida yake kuchelewa kurudi home) Niliogopa, nikaanza kumpa huduma za kifalme ili asipachukie nyumbani kwake, nikawa nampikia vizuri( alikuwa anapenda kula vizuri) nahakikisha nyumba safi kabla hajarudi, namuandalia maji ya kuoga, nampigisha story za mpira( alikuwa shabiki wa simba), basi akaanza kuwahi kurudi nyumbani na akirudi yupo sebuleni na mimi. Mama akaanza kunimind, akawa ananambia yani angekuwa mama wa kambo angehisi kuna kitu kinaendelea kati yangu na Mzee.
na nadhani huu uhusiano wangu na baba umeniathiri katika kuanzisha mahusiano ya kimapenz, ili uuteke moyo wangu lazima uwe na sifa walau moja kama ya baba yangu. hapo najifeel secure mtoto wa baba mie.
Mola mlaze mahali pema peponi baba yangu mpenzi.