manuu
JF-Expert Member
- Apr 23, 2009
- 4,064
- 10,723
Ni ukweli uliyo wazi baadhi ya viongozi wa chadema ni waropokaji sana bila hata kufikiria,Kwa nini nasema hivyo;
- Chadema wakiwa kwenye mkutano wao miezi kadhaa iliyopita katika eneo la Unga Limited Mh Nassary katika hotuba yake alipandwa na mori na kujikuta anatoa matamshi ya kuigawa nchi katika majimbo na kuacha baadhi ya sehemu.
Kitendo ambacho Mbowe alikikanusha haraka sana kwa kujua madhara ya kauli hiyo ya Nassary kwa wananchi haitapokelewa vizuri na Kamanda Mbowe akasema hii si kauli ya chama ni kauli ya Nassary mwenyewe.Na baada ya muda kauli ile ya Nassary iliibua sintofahamu nyingi sana.
-Jana nikiwa naangalia zoezi zima la M4C wakati watu wanaanza kutoa michango yao ya pesa kupitia M-PESA,mitandao ikawa slow inawezekana ni kwa sababu ya user walikuwa wengi online ghafla bila kutafakari sababu zingine zinazoweza kusababisha jam kwenye network,LEMA akasimama na kuanza kusema nyie makampuni ya simu nawaamuru muachie line la sivyo nitaamuru wananchi wote kesho watupe line zenu chooni.
Kamanda Mbowe akagundua jamaa kachemka kwa kutoa kauli kama hiyo akasimama akasema ndugu wananchi nawasii muendelee kujaribu kutuma kwani nahisi mtandao unajam sababu ya watumiaji kuwa wengi so endeleeni kutuma michango na network itatengemaa.Na hii ni kuonyesha maturity zaidi ya Lema.
Big up Kamanda.
Ki ukweli nilimkubali sana Mbowe kwani alihisi kauli kama zile si za busara na akaamua kui-neutralize na mwisho akamaliza kwa kusema nawashukuru sana makampuni ya simu na tutaendelea kushirikiana bila shida.
USHAURI WANGU KWA VIONGOZI WENGINE WA CHADEMA,Hasa Lema na Nassary aka Dogo janja.
Mjaribu kutafakari kabla ya kuongea kwani iko siku kauli zenu zitawa-cost sana na hata mnaweza kupoteza imani ya wanachama kwa ajili ya kauli zenu hizi.
WATCH YOUR TALK.
- Chadema wakiwa kwenye mkutano wao miezi kadhaa iliyopita katika eneo la Unga Limited Mh Nassary katika hotuba yake alipandwa na mori na kujikuta anatoa matamshi ya kuigawa nchi katika majimbo na kuacha baadhi ya sehemu.
Kitendo ambacho Mbowe alikikanusha haraka sana kwa kujua madhara ya kauli hiyo ya Nassary kwa wananchi haitapokelewa vizuri na Kamanda Mbowe akasema hii si kauli ya chama ni kauli ya Nassary mwenyewe.Na baada ya muda kauli ile ya Nassary iliibua sintofahamu nyingi sana.
-Jana nikiwa naangalia zoezi zima la M4C wakati watu wanaanza kutoa michango yao ya pesa kupitia M-PESA,mitandao ikawa slow inawezekana ni kwa sababu ya user walikuwa wengi online ghafla bila kutafakari sababu zingine zinazoweza kusababisha jam kwenye network,LEMA akasimama na kuanza kusema nyie makampuni ya simu nawaamuru muachie line la sivyo nitaamuru wananchi wote kesho watupe line zenu chooni.
Kamanda Mbowe akagundua jamaa kachemka kwa kutoa kauli kama hiyo akasimama akasema ndugu wananchi nawasii muendelee kujaribu kutuma kwani nahisi mtandao unajam sababu ya watumiaji kuwa wengi so endeleeni kutuma michango na network itatengemaa.Na hii ni kuonyesha maturity zaidi ya Lema.
Big up Kamanda.
Ki ukweli nilimkubali sana Mbowe kwani alihisi kauli kama zile si za busara na akaamua kui-neutralize na mwisho akamaliza kwa kusema nawashukuru sana makampuni ya simu na tutaendelea kushirikiana bila shida.
USHAURI WANGU KWA VIONGOZI WENGINE WA CHADEMA,Hasa Lema na Nassary aka Dogo janja.
Mjaribu kutafakari kabla ya kuongea kwani iko siku kauli zenu zitawa-cost sana na hata mnaweza kupoteza imani ya wanachama kwa ajili ya kauli zenu hizi.
WATCH YOUR TALK.