Bila Mbowe CHADEMA kwisha...

manuu

JF-Expert Member
Apr 23, 2009
4,064
10,723
Ni ukweli uliyo wazi baadhi ya viongozi wa chadema ni waropokaji sana bila hata kufikiria,Kwa nini nasema hivyo;
- Chadema wakiwa kwenye mkutano wao miezi kadhaa iliyopita katika eneo la Unga Limited Mh Nassary katika hotuba yake alipandwa na mori na kujikuta anatoa matamshi ya kuigawa nchi katika majimbo na kuacha baadhi ya sehemu.
Kitendo ambacho Mbowe alikikanusha haraka sana kwa kujua madhara ya kauli hiyo ya Nassary kwa wananchi haitapokelewa vizuri na Kamanda Mbowe akasema hii si kauli ya chama ni kauli ya Nassary mwenyewe.Na baada ya muda kauli ile ya Nassary iliibua sintofahamu nyingi sana.

-Jana nikiwa naangalia zoezi zima la M4C wakati watu wanaanza kutoa michango yao ya pesa kupitia M-PESA,mitandao ikawa slow inawezekana ni kwa sababu ya user walikuwa wengi online ghafla bila kutafakari sababu zingine zinazoweza kusababisha jam kwenye network,LEMA akasimama na kuanza kusema nyie makampuni ya simu nawaamuru muachie line la sivyo nitaamuru wananchi wote kesho watupe line zenu chooni.


Kamanda Mbowe akagundua jamaa kachemka kwa kutoa kauli kama hiyo akasimama akasema ndugu wananchi nawasii muendelee kujaribu kutuma kwani nahisi mtandao unajam sababu ya watumiaji kuwa wengi so endeleeni kutuma michango na network itatengemaa.Na hii ni kuonyesha maturity zaidi ya Lema.
Big up Kamanda.

Ki ukweli nilimkubali sana Mbowe kwani alihisi kauli kama zile si za busara na akaamua kui-neutralize na mwisho akamaliza kwa kusema nawashukuru sana makampuni ya simu na tutaendelea kushirikiana bila shida.
USHAURI WANGU KWA VIONGOZI WENGINE WA CHADEMA,Hasa Lema na Nassary aka Dogo janja.
Mjaribu kutafakari kabla ya kuongea kwani iko siku kauli zenu zitawa-cost sana na hata mnaweza kupoteza imani ya wanachama kwa ajili ya kauli zenu hizi.

WATCH YOUR TALK.
 
Mods mbona mmelala au mpo kwenye swaum? amisheni hii thread kwenye ile nyingine ya M4C dar kwani zimekuwa nyingi sana........!
 
Mkuu nakubaliana na wewe kwa 90%, ila tu heading yako, kwa heading yako ni sawa na kusema kama siyo Kaseja Yanga ingeifunga Simba, Kaseja yuko pale kuzuia Simba isifungwe, vivyo hivyo Mbowe ni mwenyekiti wa Chadema na wajibu wake ni kuona kuwa Chadema inafanya vizuri.
 
Mi mwenyewe lema jana alinichefua, lakini nauhakika alikuwa anatuma the right message.
 
hapo kwenye kuamuru wateja wa mitandao ya simu kutupa line alikurupuka sio kidogo. Maana najua mitandao mingi kama sio yote ilihusika kwenye hiyo harambee. Kwa maana hiyo tutupe line zote tulizonazo tutawasilia vipi.? au turudi enzi za kuandikiana barau kama zamani.. Hata kama ni kiongozi wangu mimi nisingekubaliana naye kamwe.!
 
welll, jamaa kajitahidi ona ila kuna kitu hajaona vizuri.Huwa kuna staili ya kuongoza n akukaripia watu muhimu. Yaani wanaongea watu nini cha kufanya na jinsi gani ya kueliminate damage.

Mfano. una jamaa lets say mhasibu mkuu ambaye kashikilia doc muhimu za kampuni na kaifanya office kama yake(halafu ana arrogance na irresponsible kama mtaka urais,yaani yupo tayari blackmail kila mtu ), huwa uongozi huandaa mtu mmoja wa kufikisha ujembe sahihi kwa upana sahihi.Baada ya hapo basi Kiongozi wa juu huja na kauli bogus ya kuwa pande ya aliyepewa ujumbe huku kijenga misingi ya kutomwondoa msemaji/mtendaji kwa kuleta suluhu zaidi(kumpa confort zote ya kuikubali hiyo hali).Kwa mtu mwenye akili akiambiwa mbele ya bosi wake na mtu kuwa aache tembea na mke wa bosi wake, boss aseme hakuna mtu anayeweza tembea na mkewe, halafu akaongeza ila siku mtu akikutwa basi kifo kitakuwa naye.Huyo mzizi atajitetea msemaji ni kichaa ila atajua kuwa suala lake si siri sana na kunfikia bosi ni rahisi na hatari yake ni wazi kabisa.

Kuna sehemu niliwasem aushindi wa ccm kuhusu malawi, kwali aliyesema kusuru utayari wa jeshi, tukibanwa anaweza appologize aua hata kuambiwa si msimamo wa nchi, ila kwa wamalawi wanaujua kuwa habari si mzuri.

Hizo ni njia za kufikisha ujumbe kwa kuwafanya waliopo gizani wachukulie serious wakijua kuwa kuna viherehere wanaweza haribu upepo.Kweli tunajua kuwa matandao unaweza kuwa umezidiwa ila pia huwezi jua kuwa kisingizio hichoo hicho kinaweza tumika kupunguza kasi.Vodacom walikuwa na matatizo ya mawasilino kwa siku mbili mfululizo, hat simu za kawaida hazikuwa zikienda, huwezi jua walianza mapema ili siku ya siku wawe na cha kujitetea.Ila Lema ni mtu sahihi wa kuufikisha huo ujumbe, na wanamjua kuwa ni mhamasishaji mkubwa, na huwa acheleweshi.Ila mbowe aka neutralize .Ujumbe umefika,tena kwa vitisho huku chama kikinyenyekea kuwa bila voda M4C itayumba.Ukweli ni kwamba voda nao wanahitaji kujenga mahusiano kupitia watu wasionekana kuwa karibu na CCM kwani kibao kikigeuka basi wasiangamie,ingawa nao wana wana ccm katika umiliki wao.

Alichosema Nassari kiliwatisha CCM na ujinga wao wa kusingizia watu kuwa ni wakanda huku wakidhulumi na kubagua baadhi ya kanda kwa kila kitu(kuanzia rasilimali, utawala wa nchi etc), so kauli ya Nassari ni kuwaonyesh akuwa ikibidi kuwa na kanda pia ianweza fanyika vizuri zaidi na kupata ukanda wenye mazingira mazuri geographically na economically.
Kuanzia hapo CCM kam wana akili watajua kuwa alichoongea Nassari hata kama hakikuwa official ni wazi kuwa siasa za maji chafu za CCM za kutumia udini na ukanda, watu wanawez abadili kuwa suggestion pia.

So Lema ahjakosea, Mbowe hajakosea, na mitandao haijakosea ila Check and balance imefanyika.Ila ni wazi wameona kuwa visingizio ama kujificha nyuma ya fact huku wakiwa na nia ovu si salama.By the way na wao pia wanapata hela kwa yanayotokea, na Tanesco kama wahajui kuwa atumizi ya umeme siku hiyo ni hela, na kuzima umeme siku hiyo na saa hiyo hakuna wanachosave au mmbadala wa customer
 
Ushauri mzuri ila badilisha heading hiyo, wahusika wataufanyia kazi huo ushaui wako.
 
Back
Top Bottom