Lakini Anita, tusiangalie upande mmoja tu bwana, let’s be fair. Bikira ina umuhimu wake wa kisaikolojia na kijamii. Mwanamke anayeingia kwenye ndoa akiwa bikira anakuwa hana emotional baggage, hii huwa inaleta amani fulani na heshima ya kipekee kwa sisi wanaume kwa sababu unakuwa unajua kuwa wewe ndio wa kwanza kwenye maisha yake ya mahusiano.
Ni vile kwa sasa imekuwa ni ngumu sana kama sio muujiza kwa kila mwanaume kukutana na mwanamke bikira. Hali ya maisha na jamii imebadilika sana kiasi kwamba hiki kigezo kimekuwa adimu mno kwa sababu ukiangalia mtandao na simu janja zimefika hadi vijijini, na kuondoa ule usiri au ushamba uliokuwepo zamani.
Umri wa mabinti kuolewa kwa sasa ni kama umesogea mbele, kiuchumi na kielimu, sasa hivi wasichana wengi wanaolewa wakiwa na miaka 25 hadi 30+, umri ambao kibaolojia na kijamii ni ngumu sana kwa huyo binti kuwa bado hajakutana na vishawishi vya kimapenzi.
So mwisho wa siku, kila mtu anabaki na vipaumbele vyake, kuna watakaoona tabia na utangamano ndio kila kitu, na kuna wanaoona misingi ya kujitunza tangu mwanzo ndio msingi wa uaminifu.