Biggest slums in africa

Tanzania slums hatuna isipokuwa hatuna usimamiz wa mipango miji baadhi ya maeneo hayakutakiwa kukaliwa na watu lkn yanakaliwa na watu kama huko bonde la mto msimbazi najua wanaobisha wangeenda hata kibera wakaone slum ni nini au huko india
Shida mkuu watu hata maana ya slums hawajui.
Bongo kuna unplanned settlements hakuna slums.
Sasa wao wanashindwa kutofautisha hayo.
 
Kwa vigezo vya slum hizo hazijafikia kuitwa slums.
Zitabaki kuwa informal settlements tu.
Hakuna hata sehemu moja hapo unaweza ukaifananisha na Kibera.
Kibera hata mnyama hawezi ishi.
 
Unajua maana ya slum kijana!?
Dar Kuna unplanned towns sio slums.
Embu enda usome maana ya slums halafu urejee.
Inamaana wewe na jumuiya za kimataifa zilizofanya tafiti wewe una akili zaidi?
Acha ujuaji dogo, yawezekana haujafika dar slum
Yaani Tandale,keko,jangwani sio slums? Yaani unatafsiri slum kwa tafsiri yako wewe? Punguza ujuaji dogo
 
Usidanganyike na upya wa eneo. Hakikisha kumepimwa. Mji utaonekana mzuri mwanzoni kwa nyumba mpya. Ila baada ya muda unageuka slum kwa mbanano na ukosefu wa utaratibu.
 
Acha ujuaji dogo, yawezekana haujafika dar slum
Yaani Tandale,keko,jangwani sio slums? Yaani unatafsiri slum kwa tafsiri yako wewe? Punguza ujuaji dogo
Aiseeee Tandale ipi unaiseme wewe?
Kwa tumbo,mto wa ng'ombe,Kwa mtogole au Tandale ipi!?
Keko machungwa nyuma ya Kurasini Mivinjeni huko kote mimi nimelelewa.
Mie mtoto wa Temeke Kwa Azizi Ally sheli.
Hakuna kiunga ambacho cha Dar sijakanyaga.
Hiyo keko ndio usiseme,tena tulikua tunatembea Kwa miguu kutoka Kwa Azizi Ally tunaibukia makaburi ya Chang'ombe tunatokea Kibasila sekondari tunanyoosha maduka mawili Kwa nyuma tunakatia shule ya Yemeni kwenda keko Machungwa.
Kote huko Kuna makazi ya zamani sio slums.Makazi ambayo unaweza kuyaboresha pasi na kuyavunja.
Msimbazi inavunjwa au wewe hilo hulijui!?
Halafu acha kuniita dogo.
 
Usidanganyike na upya wa eneo. Hakikisha kumepimwa. Mji utaonekana mzuri mwanzoni kwa nyumba mpya. Ila baada ya muda unageuka slum kwa mbanano na ukosefu wa utaratibu.
Nina hati ya kiwanja na eneo limepiwa; slums zimejaa kwenye kwenye maeneo yaliyokuwa yamekusudiwa yawe wazi kwa sababu ni kwenye milima halafu hakuna udhibiti watu wanajijengea hovyo hovyo tu.
 
Dogo fika kwanza dar slum ndio tujadiliane naona wahadithiwa tu huko kwenu mpitimbi,kwa shemeji unaanf
 
Dogo fika kwanza dar slum ndio tujadiliane naona wahadithiwa tu huko kwenu mpitimbi,kwa shemeji unaanf
Umerogwa wewe.
Labda kama unakaa mpitimbi ni wewe.Hizo direction nilizokwambia sidhani kama hata unazijua.
Unajifanya unakaa Dar hata hujui kama Msimbazi inabomolewa doooh.
Nakukaribisha karibu Kigamboni polisi njia panda ya Mwasonga.
Halafu mie sio msukuma mwenzio.
 
Unaijua manzese wewe?hii inayochipua Kila siku hotels na vitega uchumi vya Kila aina?
Labda vile vijumba vya zamani vya urithi ndo umeona kigezo..haina sifa ya kuitwa slum
Manzese wewe hupajui ingia humo ndan ndan ujionee mwenyewe aisee utashangaa
 
Unaongelea Tanzania gani wewe mwehu ? ,Umefika Lindi ,Dodoma ,Singida huko ndani ndani ,Shinyanga nk ?
 
Vipi tandale ya kwatumbo,vipi mwananyamala kwa mtogore
Mwananyamala somehow inabadilika.
Zile barabara za mitaa kidogo zinastua watu wabadili mji.
Ila yote yale ni majumba chakavu ya zamani yaliyojengwa bila mipango miji.
 
Unaongelea Tanzania gani wewe mwehu ? ,Umefika Lindi ,Dodoma ,Singida huko ndani ndani ,Shinyanga nk ?
Hiyo mikoa uliyotaja umewahi kuona nyumba za mabati tupu mkuu!??
Tena hiyo mikoa ni masikini wa kipato ila Kenya ni masikini Hadi wa chakula.
Hivi unajua kaka kuwa Kenya ipo kwenye orodha ya mataifa yanayopokea misaada ya vyakula toka WFP?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…