Wakati fulani nikipita kwenda kwenye channel ninazozitaka huwa najikuta nimepitia channel zinazoonesha wanachoita Big Brother Afrika. Humo huwa naona vijana wa kiume na kike wakilala pamoja, wakioga pamoja, wakihojiwa, wakicheza, wakipika, wakiimba, na mengine mengi ambayo katika utamaduni wa kiafrika yasingekuwa ya kawaida tena hadharani. Sasa mimi huwa sielewi ni nini kinachokusudiwa na hicho kinachoitwa shindano la BBA. Ni kwaajili ya kujifunza au kufundisha nini? Je hao vijana wakitoka hapo wanakuwa watu wa aina na wenye manufaa gani kwa jamii. Mwanzoni nikifikiri kwa jina lake itakuwa ni wavulana watupu, kumbe na wasichana wamo yaani ni kama kusema Big Brothers and Sisters Afrika. Yaani sielewi hata nikiangalia sijui lolote na sioni la kujifunza au vijana wa Tanganyika kujifunza ingawa nasikia kuna mmoja aliwahi kuibuka na Mil 100 hata sijui aliishia wapi na ana manufaa gani kwa jamii.