Bifu kubwa kati ya mwanaspoti na championi

Bifu kubwa kati ya mwanaspoti na championi

Tatizo Eddo ni kujifanya anajua kila kitu kuhusu mpira...asijue kuwa wanaoujua mpira na uchambuzi wake ni wengi na hasa ktk ulimwengu huu wa mitandao...na ajue yeye anafanya kama kazi wengine wanajua na kuchambua mpira kama hobby tu,so asifikiri yeye anajua yote ktk soka!!!Eddo mashauzi mengi..hataki kukosolewa kana kwamba anajua kila kitu...ni mtu wa majungu hata wafanyakazi wenzake wanalalamika anajidai much knower na mjuaji wa kila kitu.
Naye Salehe aache maneno ya vijembe afanye kazi,kuonyesha maneno kama hayo anathibitisha kuwa anaiogopa mwanaspoti...huwezi kupata hofu kwa kitu usichokiogopa...Champion kwa Mwanaspot ijipange

Hoja hapa si Edo, ni Mwanaspoti vs Champion
 
Tanzania hakuna wachambuzi wa soka, kuna watoa maelezo ya nini kinafanyika... wanafanya kitu kama hiki "Sunday na mpira, Sunday na mpira, kashoot Gooooooooo"
 
Mwanaspoti limesheheni, hayo mambo ya edo na saleh tuwaachieni wenyewe.
 
Wananchi tunataka Habari tu,hayo mengine tunawaachia
 
Edo kumwembe n jembe kwenye 7chambuz wa soka soooo mwanaspot wako juu zaid ya champion jammnn au hmjui hlooo
 
Ninachokiona hapa
kulikua na bifu ya chini chni kati ya edo na salehe ila sasa inaota
mizizi. Salehe alimponda edo kwa kumwambia kuwa ni mtu ambaye anaziba
nafasi anazoziacha kwa maana alipoacha kazi dimba edo akaenda kuziba
pengo afu pia salehe alipotoka mwanaspoti edo akaenda kuziba
pengo

kama yeye salehe alikuwa anaondoka kwa kufuata maslahi bora, kuna ubaya gani kwa eddo kuziba hizo nafasi kwa maslahi bora?
Salehe aache hizo, mwanasport kutoka mfululizo inajulikana sababu ilkuwa nn.
champion page zao za kwanza na mwisho ni kopy kutoka mwanasport.
 
Mimi naona ni ile wanayoiita kwa Kiingereza, chungu kuliita birika ni jeusi (a pot calling a kettle black). Sioni kati yao wala magazeti yao mwenye uwezo wa kujifanya yeye kuwa legend na gazeti lake kuwa brand. Waandishi wetu wengi hupima uwezo wa wachezaji wetu kicheza ligi za Ulaya. Lakini hawajipimi wao kwa uwezo wa makala zao na wao wenyewe kukubalika huko wanakoyaka wachezaji wetu wakibalike. Wanabaki kuwa ni wakalimani wa mitandao ya nje, wakosoaji wa kila jambo la michezo linaloganyika Tanzania, na watetezi wa maslahi yao kupitia tawala za vilabu vyenye uwezo wa kuwatiizia. Tujiulize, lini magazeti haya yatanukuliwa na vyombo vya habari vya kimataifa kwa makala zao asilia (original) kama wao wanavyonukulu makala za wenzao?
 
MwanaSpoti sikosi nakala nakala yake ya Jumanne na Jumamosi. Kifupi jamaa wanajua
 
Mimi naona ni ile wanayoiita kwa Kiingereza, chungu kuliita birika ni jeusi (a pot calling a kettle black). Sioni kati yao wala magazeti yao mwenye uwezo wa kujifanya yeye kuwa legend na gazeti lake kuwa brand. Waandishi wetu wengi hupima uwezo wa wachezaji wetu kicheza ligi za Ulaya. Lakini hawajipimi wao kwa uwezo wa makala zao na wao wenyewe kukubalika huko wanakoyaka wachezaji wetu wakibalike. Wanabaki kuwa ni wakalimani wa mitandao ya nje, wakosoaji wa kila jambo la michezo linaloganyika Tanzania, na watetezi wa maslahi yao kupitia tawala za vilabu vyenye uwezo wa kuwatiizia. Tujiulize, lini magazeti haya yatanukuliwa na vyombo vya habari vya kimataifa kwa makala zao asilia (original) kama wao wanavyonukulu makala za wenzao?
Magazeti yetu ni kwa ajili ya wasiosoma mitandao. 90% ya taarifa ni tafsiri kutoka The Sun, Daily Mail na Goal.Com. Unashindwa kuelewa waandishi wanasomea nini vyuoni? Waandishi wetu wanaenda vyuoni kujifunza kutafsiri kazi za watu?
Hofu yangu kubwa ni kizazi chetu kama kweli tunapiga hatua intellectually, iweje magazeti yenye kubeba habari za copy and paste kwa 90% na kutafsiri habari kwa lugha tunayoitumia shuleni na vyuoni yaongozee kwa mauzo...Kuna shida hapa. Wingi wa vyuo na shule unatusaidia vipi?
 
Magazeti yetu ni kwa ajili ya wasiosoma mitandao. 90% ya taarifa ni tafsiri kutoka The Sun, Daily Mail na Goal.Com. Unashindwa kuelewa waandishi wanasomea nini vyuoni? Waandishi wetu wanaenda vyuoni kujifunza kutafsiri kazi za watu?
Hofu yangu kubwa ni kizazi chetu kama kweli tunapiga hatua intellectually, iweje magazeti yenye kubeba habari za copy and paste kwa 90% na kutafsiri habari kwa lugha tunayoitumia shuleni na vyuoni yaongozee kwa mauzo...Kuna shida hapa. Wingi wa vyuo na shule unatusaidia vipi?
Nashawishika kuamini kwamba siku hizi biashara ndio kila kitu. Taaluma, sanaa, siasa, dini, kila kitu kipo kwa ajili ya biashara kwanza, mengine baadaye. Ndio maana dansi asilia zinatoweka kwa muziki wa kizazi kipya, taarabu asili imeuliwa na modern taarab, makanisa ya mtu mmojammoja yanachipua kila siku, waislamu wanachezesha bakora misikitini kugombea uongozi, vyama vyetu haviongozwi kwa kufuata itikadi fulani (ideology), wachezaji mpira wanasaini mikataba zaidi ya mmoja ndani ya msimu mmoja. Kwa mtindo huu, huenda siku moja hata Katiba ikaruhusu watu kuuza nchi iwapo kutakuwa na kura za kutosha kuunga mkono hilo. E Mungu, tusaidie!
 
mimi nina mitazamo miwili tokana na hii habari na wachangiaji
mosi, salehe ally anatakiwa awe na busara afahamu mwanaspoti ipo juu ya championi na pili yeye ameajiriwa tu na global kesho wanaweza filisika akarudi mwanaspoti kuomba kazi, so beef na wenzie hazipendezi
 
Back
Top Bottom