Rockcity native
JF-Expert Member
- Dec 31, 2012
- 2,174
- 1,462
Kwa kile kinachoonekana gazeti la mwanaspoti kuongeza matoleo katika wiki na kua mara 4 kwa wiki, kitendo hicho kimezua hasira kwa mwandishi nguli na mhariri wa championi bw salehe ally ambaye katika akaunti yake ya facebook aliandika "joto wameshalipata na jumatatu wataikimbia wenyewe" maneno hayo yaliashiria kitendo cha mwanaspoti kutoa toleo jumatatu ni kujipalia mkaa.. Hiyo si mara ya kwanza kwa salehe ally kulumbana na watu wa mwanaspoti kwani ikumbukwe mwezi mmoja uliopita alimshambulia kwa maneno machafu mchambuzi wa mwanaspot bw. Edo kumwembwe kwa madai ya kuingilia taarifa ambayo ilimuhusu bondia wiliam aliepigana na fransis cheka kuwa ni kinyozi huko kwao marekani