Biden atashinda, Trump is done

Hazi-determine ila lazima ushughulike kupata hizo kila jimbo ndipo ushinde hizo za electrol college. Kwa hiyo si sahihi kusema poular votes siyo determinant. Kila state bila kushinda popular votes huwezi pata zile special. Main determinant ni popular votes

Sent from my SM-J530F using JamiiForums mobile app
 
Duh!

Hata tahajia nyepesi nyepesi zinakushinda?

Ndo maana hata hujaelewa kinachozungumziwa hapo.

Kinachozungumziwa hapo ni national popular votes.

National popular votes hazi determine mshindi wa urais.

Unabisha?
 
Huu ndio ukweli mwenyewe.
Sioni namna ambavyo Trump anaweza kutoboa mwaka huu.

Kwenye kura za maoni kaachwa nyuma, kwenye uchambuzi wa midahalo yote mitatu kaachwa nyuma na kwenye agenda muhimu zinazowagusa wamerekani wengi (Ubaguzi, Corona, Ajira) kaachwa nyuma. Sioni mahali ambapo Trump anaweza kusimamia ili kuweza kushinda.
 
Duh!

Hata tahajia nyepesi nyepesi zinakushinda?

Ndo maana hata hujaelewa kinachozungumziwa hap

Kinachozungumziwa hapo ni national popular votes.

National popular votes hazi determine mshindi wa urais.

Unabisha?
We una ubishi usio na tija. Unavosema hau-determine sijui una maana gani. Sema siyo determinant pekee. Mgombea lazima atafute popular votes kwanza kwa kila state then ndiyo zimpe special votes. Na ni mara chache imetokea kwa Rais kushinda kura maalumu bila kushinda overall popular votes.

Sent from my SM-J530F using JamiiForums mobile app
 
Kwanini 2016 Trump aliweza kushinda?

-Wamarekani wengi walimpigia kura Clinton lakini sheria za kumpata mshindi zikamuwezesha Trump kushinda. Hiyo ni technical winning. Yaani wingi sio issue issue ni ubora.

-Hillary Clinton alikuwa anapendwa zaidi lakini bado wamarekani wengi walikuwa hawamwamini kama ni mtu imara kuweza kushika madaraka makubwa kama yale. (Kuwa mwanamke? Skendo za propaganda kuhusu uzembe uliopelekea kupoteza maisha kwa maafisa wa ubalozi marekani kule Banghazi).

-Siasa za kifadhihina za wababe wa Republican zilitawala mchuano mzima kiasi cha kumpa umaarufu usio stahili Trump. (Wengi hawajui kuwa, kitendo cha Democratic kuongoza vipindi viwili mfululizo tena chini ya Rais Obama kilikuwa ni tusi kubwa kwa wamarekani wenye mrengo mkali, siasa ngumu na wabaguzi. Hao jamaa hawakupenda kabisa waendelee kuwa chini ya Democratic kwa gharama yoyote, na Trump alikuwa mtu sahihi kwao. Sasa walichokivuna chini ya utawala wa Trump sina uhakika kama watatamani Trump aendelee tena)
 
National popular vote hai determine mshindi wa urais Marekani.

Unabisha au unakubali?
 
SirChief, New York Times inaheshimika na ni gazeti (Newspaper) na New York Post ni kijarida cha udaku (tabloid). I rest my case!
Kwa akili yako unafkiri sijui tofauti ya NYT na NYP,nilikuuliza unaposema NYT inaheshimika,inaheshimika na kina nani??
 
Trump yupo nyuma sana katika kura za maoni
Msiamini sana opinion polls nyingi zinakuwa manipulated na main stream media kutokana na wamiliki wa makampuni hayo hawaungi mkonoTrump, kumbukeni walivyo kuwa wanampigia debe Hillary Clinton kwamba angeshinda kinyanganyilo cha Urais, sasa nini kilitokea eventually? Trump alimshinda Clinton.
 

Msikilizeni vizuri anacho kisema "Nyani Ngabu" mbona amefafanua vizuri tu - tatizo liko wapi?
 
LISSU anashinda asubuhi na mapema,Trump anashinda tena hakuna ubishi
 
Trump anashinda kwa kishindo, ni kichaa pekee anaeamini kwamba biden anashinda,, Tatizo lenu mnaangalia sana cnn
 
Mkuu hilo linajulikana tangu awali trumpet hana chake. Tulisema hata ile awamu ya kwanza, huwzi kuwa rais wa nchi hasa USA wakati hakuweza hata kuonyesha alikuwa anachangia kiasi gani cha kodi kwenye uhai wake wa kufanya kazi. Trumpet ni jambazi mbobezi, na wananchi wa USA waliingia choo cha kike.
 
Nyani Ngabu,

..Nasikia Biden atapata ushindi wa kishindo / landslide.

..eti Biden atashinda electoral college vote 290 huku Trump akiambulia 163.

..hizo habari ni kweli?
 
Nyani Ngabu,

..kwa hiyo unadhani Trump atashinda?

..unajua uchaguzi mzuri ni ule ambao mshindi hajulikani mpaka dakika za majeruhi.

..napenda zile chaguzi ambao waandishi husema ni " too close to call. "

..natamani siku moja na sisi Watanzania tufike huko, tuwe na chaguzi za namna hiyo.
 
Honestly speaking, I don’t know who’s gonna win.

Mimi siku zote huwa nasema kura zinazo matter ni zile kura za kweli zinazopigwa siku ya uchaguzi.

Opinion polls don’t count...
 
Honestly speaking, I don’t know who’s gonna win.

Mimi siku zote huwa nasema kura zinazo matter ni zile kura za kweli zinazopigwa siku ya uchaguzi.

Opinion polls don’t count...

..hivi ni kweli kwamba wakati wa uchaguzi huko kwenu huwa hakuna mapolisi wanaoranda-randa kwenye vituo vya kura na mitaani?

..au polisi, fbi, na marines, siku ya uchaguzi hutoka kwenye makambi yao kuimarisha ulinzi kwa hofu ya kutokea machafuko?
 
Biden hashindi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…