Uzalendo wa Kitanzania
JF-Expert Member
- Mar 8, 2020
- 4,205
- 9,196
Kura za maoni ( Opinion polls) & kura za wengi ( Popular vote) hazina maana yeyote kwenye kuamua nani awe Rais zaidi ya kuonyesha maoni ya wapiga kura!
Uamuzi wa nani awe Rais wa Marekani unafanywa na Wajumbe wa Baraza la Uchaguzi ( Electrol College) na si vinginevyo.
Kusema Trump atashindwa eti kwa sababu ya maoni ya Wamarekani ni kichekesho kikubwa.
Mfumo huo uliwekwa mahsusi kubalance Matokeo ya Uchaguzi ili Kuzuia baadhi ya majimbo yenye wapiga kura wengi au Jamii ya Watu walio wengi au Chama chenye wafuasi wengi kuamua nani awe Rais! Pia unazuia kura za MIHEMUKO Kwenye kuamua nani awe Rais wa Taifa hilo kubwa Duniani.
Wajumbe wa Baraza ndiyo wamepewa majukumu Kisheria na kwa mujibu wa Katiba kuchagua Rais wa Marekani kwa niaba ya Wamarekani Wote!
Kuna Kampeni zimeshika Kasi kufuta Mfumo huo wa kuchagua Rais kwa kutumia Baraza la Uchaguzi ila utahitaji upitishwe na Baraza la Wawakilishi, Seneti na Kupigiwa kura na Wamarekani Wote
Uamuzi wa nani awe Rais wa Marekani unafanywa na Wajumbe wa Baraza la Uchaguzi ( Electrol College) na si vinginevyo.
Kusema Trump atashindwa eti kwa sababu ya maoni ya Wamarekani ni kichekesho kikubwa.
Mfumo huo uliwekwa mahsusi kubalance Matokeo ya Uchaguzi ili Kuzuia baadhi ya majimbo yenye wapiga kura wengi au Jamii ya Watu walio wengi au Chama chenye wafuasi wengi kuamua nani awe Rais! Pia unazuia kura za MIHEMUKO Kwenye kuamua nani awe Rais wa Taifa hilo kubwa Duniani.
Wajumbe wa Baraza ndiyo wamepewa majukumu Kisheria na kwa mujibu wa Katiba kuchagua Rais wa Marekani kwa niaba ya Wamarekani Wote!
Kuna Kampeni zimeshika Kasi kufuta Mfumo huo wa kuchagua Rais kwa kutumia Baraza la Uchaguzi ila utahitaji upitishwe na Baraza la Wawakilishi, Seneti na Kupigiwa kura na Wamarekani Wote