Jaguar
JF-Expert Member
- Mar 6, 2011
- 3,440
- 1,029
Tukiwa msibani kijijini eneo la makaburi,bibi mmoja akiwa kambeba mjukuu wake mgongoni alisikika akilia kwa uchungu;'jamani huyu kijana kafa bado mdogo kabisa,inatia uchungu sana,bora ningekufa mimi mzee nimeyafaidi maisha kiasi cha kutosha'.Akiwa katikati ya kilio chake,mara ghafla nyoka toka mtini akamdondokea mtoto mgongoni kwa bibi.Bibi alimfungua mtoto fasta na kumtupa chini,akatoka mbio kama caster semenya huku akipiga mayowe.