Anaweza kuwa ni mwaminifu ila ana makosa kwenye kutoa chenji ama kutuma hela. Jaribu kumfanyia test, unamtajia kiasi ye akiandike kwa tarakimu chap chap. Taja kiasi kama laki moja na elfu tano, milioni moja na elfu nane mia tano nk nk.
Kwa uzoefu wangu, mawakala wengi sana wanakwama hapo na wateja 'wajanja' wakishamjua, ndio wanampiga kihivyo.
Anampa laki na elfu tano mia tano (105,500/=) binti anamtumia laki na hamsini na tano (155,000/=).
Kuna mdau pale juu kashauri urekodi transactions zote, unaweza pia kuweka vile vikaratasi kila mteja anajaza namba, jina na kiasi then vitunze ili kukiwa na mapungufu unavipitia upya jioni.
Mbali na hayo, issue za pesa zina ushirikina mwingi sana, hivyo ushauri wangu muhusishe sana Mungu kwenye biashara yako na pia weka mfanyakazi ambaye yuko active sana (mjanja) anayeweza kustudy matapeli kirahisi.
Zuia matumizi yasiyo ya lazima ya simu akiwa ofisini kwa kuwa inamuondolea umakini na piga marufuku vijana kuzoeana naye hapo na kumpa viofa vya soda kwani wakishajenga mazoea ndio 'wanampiga' kirahisi sana.
Mlipe vizuri kama kuna faida ya kutosha ili aithamini kazi yake, kama hapo kuna vifursa kama kuuza vinywaji, bites nk muwekee uwe mradi wake ili kuongeza uaminifu wake na kithamini kazi. Nina ofisi ya hivyo na inafanya vema na anayeisimamia ni binti tu me niko mbali.