Biashara ya Uwakala na upotevu wa pesa

Biashara ya Uwakala na upotevu wa pesa

Kwa miamala ya kibank wateja huwa nawajazia fomu za bank husika nabaki na copy na miamala ya simu huwa siandikishi ....nakua makini kwa kila hatua ya kufanya muamala napesa cash mtu anapotoa lakini nikipiga hesabu jioni hasara inakuwa ipo
Kuna trend ya kutumiwa meseji hewa unaweza ukadhani kweli umepokea pesa kumbe ni hoax
 
Biashara ya pesa inahitaji umakini sana, hata kuzidisha pesa kwa wateja ni kawaida..
Ndio lakini sio kila siku mpendwa najitahidi kihesabu vizuri pesa na kufanya muamala kwa umakini lakini bado hali ni hiyo hiyo
 
Itakuwa wazee wa "Ndele" wanapita na mashuka ya Mmasai! Muda wa kufanya kazi na wazee wa Bagamoyo umewadia. Biashara ni ngumu sana kibongobongo maana kanuni za vitabuni pekee hazitoshi. Lazma uende nje ya box kistaili. Wanasema vipande vya mkaa kwenye droo ya pesa husaidia.
Hahahaha umenikumbusha kuna jamaa yangu mmoja hivi anaamini sana katika chuma ulete. pesa ikionekana ku miss moja kwa moja jamaa anajua wazee wa street wamepita nayo

Huyo jamaa alikua hana masihara kwenye swala la hela nakumbuka alimfata mzee mmoja hivi anauza madawa ya asili Kuomba ushauri kudhibiti hiyo kero ya upotevu wa hela

Mzee akamuambia weka mikaa kwenye droo yako ya pesa kisha ukipokea hela kwa mteja iweke chini kisha ikanyage na mguu ndio uiweke kwenye droo ikapigwe msasa na mkaa.

Mzee akamuambia ila kuna njia nyingine ambayo ni bora zaidi na iko very secure kukulinda na chuma ulete ila tatizo moja tu inapingana na itikadi zako

Jamaa akauliza ipi hiyo, yule docta akamwambia ni kuweka mifupa ya nguruwe kwenye droo unapo hifazia pesa zako. Ukiweka mifupa hata mamluki waje na magnetic ya kichawi hawanasi kitu

Jamaa hakumjibu mzee ila kesho yake nilimuona yuko around kwenye bucha la nguruwe
 
Habari wanajamvi ..naomba mnisaidie jambo moja kwa watu wenye uelewa na hili swala la mambo ya wakala wa huduma za kifedha katika mitandao ya simu na huduma za Kibank.Mimi nafanya huduma hizi jambo linalonisumbua wanajamvi ni upotevu wa pesa .kwamfano nina mtaji wa M20 nazungushia pesa hizo katika wakala huduma za kibenk na mitandao ya simu .kutoa na kuweka pesa sasa kila ninapofunga hesabu lazima nikute pesa pungufu Mara elf 20,18,30,40,juzi nimepata loss ya laki 3 .wanajamvi nashindwa kuelewa shida inakua ni nini najitahidi kuwa makini kwa kila muamala lakini. Bado hali ni hiyo hiyo naomba mnisadie hata mbinu au mawazo maana sijui tatizo linakua wap kwa wenye uelewa nipeni mbinu yakutokupata hasara za mara kwa mara
Inaonekana huwa huhesabu vizuri pesa unazopewa na wateja.

Au ukishahesabu, unamrudishia mteja tena halafu akikupa tena huhesabu kwa kuwa ukishahesabu mwanzo.

Pili, labda kuna mtu wa karibu unaefanya naye kazi ANAJIONGEZA kidogo kidogo
 
Juzi hapa mtaani kuna dada alifumwa katoa pesa kwa wakala kwa meseji hewa

Yule dada alikua mrembo sana lakini wahuni walivyokua wanamgombea kumpiga ni kama vile wananpiga jombi
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Wanaume wa siku hizi hawana 'mahaba' na wanawake ndio maana ukipita kwenye 'vikao' vyao wako hata kumi na hakuna mdada hata mmoja na story zao ni siasa, mpira na mambo mengine ya maisha.
 
Hahahaha umenikumbusha kuna jamaa yangu mmoja hivi anaamini sana katika chuma ulete. pesa ikionekana ku miss moja kwa moja jamaa anajua wazee wa street wamepita nayo

Huyo jamaa alikua hana masihara kwenye swala la hela nakumbuka alimfata mzee mmoja hivi anauza madawa ya asili Kuomba ushauri kudhibiti hiyo kero ya upotevu wa hela

Mzee akamuambia weka mikaa kwenye droo yako ya pesa kisha ukipokea hela kwa mteja iweke chini kisha ikanyage na mguu ndio uiweke kwenye droo ikapigwe msasa na mkaa.

Mzee akamuambia ila kuna njia nyingine ambayo ni bora zaidi na iko very secure kukulinda na chuma ulete ila tatizo moja tu inapingana na itikadi zako

Jamaa akauliza ipi hiyo, yule docta akamwambia ni kuweka mifupa ya nguruwe kwenye droo unapo hifazia pesa zako. Ukiweka mifupa hata mamluki waje na magnetic ya kichawi hawanasi kitu

Jamaa hakumjibu mzee ila kesho yake nilimuona yuko around kwenye bucha la nguruwe
[emoji3][emoji3][emoji3] jamaa kiboko..maadam hakula hiyo nyama haina shida
..unajua inaumiza kufanya biashara kwa umakini lakini bado mambo yanaenda mrama
 
Back
Top Bottom