Biashara ya Solar

Game Theory

Platinum Member
Sep 5, 2006
8,545
835
Jamani naona hili tatizo la umeme tutaendelea kuwa nalo kwa miaka takriban 20 ijayo

sasa nauliza je kama nataka kufanya biashara ya solar kama wale jamaa wa REX mnanishaurije?

Naweza kuingia ubia na watu ambao wanaweza kukusanya investment capital ya kiasi cha 2-3 million usd

Je soko lipo Tanzania?

Je solar ni zero tax kama nchi zingine?

Je REX ni ya nani na wanaendeleaje?

Kutokana na tatizo la umeme naona ni ngumu hata kuweka assembly Tanzania je tukiingiza ambazo zishafungwa toka nje je?

Je naweza ku incorporate na umeme wa upepo pia au?
 
Mkuu uko nchi gani?

Kuhusu soko la solar kwa Tanzania ninavyo jua si kubwa sana na sana sana wazungu wanao ishi huku ndo watumiaji wazuri sana wa solar kuliko wabongo.

- Watanzania wengi wanapendelea genereta kuliko solar na ndo maana kipindi cha migao ya umeme utakutana na Genereta nyingi zi iungulruma.

- Ila kwa maeneo ambayo umeme hujafika soko si baya, ila unatakiwa kuwalenga watu wa vijijini make kule ndo kuna shida sana

- Kwa mijini watu wengi wanaishi kwenye nyumba za kupanga na kama unavyo jua zilivyo na mashariti mengi, so metu anaona kuliko kupandisha solar kwenye paa la nyumba ambayo si yake bora anunua kajenereta kake.

ILA MKUU FANYA RESEARCH ZAIDI, HAO REX MIMI C WAJUI NAWAONAGA TU, NI VIZURI UKAFANYA ANALYSISI YAKO MWENYEWE KATIKA MIKOA MBALIMBALI NA UKAONA UKUBWA WA MAHITAJI YA HIYO PRODUCT.

- KUHUSU KODI LABDA CHEKI KWENYE WEBSITE YA TRA UTAKUTANA NA HAYO MAMBO YA USHURU WA SOLAR
 
kaka nashkuru sana
Mimi niko Denmark na hawa jamaa kwenye masuala ya renewable energy ndio wenyewe

REX ni the only player wa maana Tanzania as we speak

Genereta tatizo ni kwanza ghali na pili bei ya mafuta inawaadhibu sana watu NA kama zina kodi then its more economical watu wakawa na solar kuliko generator

Kuhusu kodi poa ntacheki kwenye website ya TRA

watu wa vijijini si wengi ambao wataweza kununua solar kwa bei za juu lakini nijuavyo NGO na 1% ya wa Tanzania ni soko tosha kabisa then kuna soko la middle class pia
 
Soko la solar lipo, watu wanakimbilia generator kwa kuwa kwa haraka haraka inaonekana kama ndio rahisi kuliko solar kwa sasa. Nashangaa kwa nini Rex wana bei hivyo, mfano mimi niliwahi wasiliana nao ili kujua kama nataka kuwasha taa zangu zote na labda tv nitahitaji kiasi gani. Tulipopiga hesabu ikaja karibu 5mil, wakati nawazapata generator chini ya 1mil shida itakuja kwenye mafuta.
Mkuu nakuhakikishia ukija na solar na bei ikawa resoanable wateja tupo tena wengi, binafsi ningetamani kuachana na tanesco kabisa ila si kwa gharama kama za rex.
 
Tanzania ina watu milioni 45

Nadhani REX kwa sababu wako peke yao wana milk as much as possible na nadhani wanaweka profit margin kubwa mno

hii issue mimi nataka niighulikie kiundani zaidi

imagine 5% ya population wakipata solar tutakuwa wapi?

Anyway nadhani kuna umuhimu wa ku explore zaidi lakini naamini hiii kitu inawezekana sana tuuu

Lakini pia TRA nao inawezekana wanakata kod kubwa zaidi

Nimetazama website yao hakuna sehemu yenye list ya viwango vya kodi
 
Nakuhakikishia mkuu kuwa soko lipo tena kubwa na la kibiashara, wewe jipange tu. Tatizo linaweza kuwa TRA, maana huwa hawako wazi hivyo unaweza ukakuta kodi ya ajabu huko. Unasema Rex wako peke yao, hapana hawako peke yao kuna kampuni nyingine tena ila jina lake limenitoka nikumbuka nitakutajia. Ila inaonekana nao pia hawajajipanga vizuri kufanya biashara ya solar, wewe jipange tu soko lipo tena zaidi ya 5% nakuhakikishia.
 
Mkuu, nimependa sana, kuhusu solar power, Mungu akutangulie kusupply hapa Tanzania. Pia sisi sote tunatakiwa kufahamu, mabadiliko ya hali ya hewa, yanapelekea sana kuongezeka kwa joto na kukauka kwa vyanzo vya maji kwa matumizi ya Hdyro Power kama Pangani falls. Solar Power ndiye mkombozi wa Tanzania na tatizo la umeme.
 
House_SolarSmart.jpg

The main way that a conventional gas "combination boiler" continually wastes energy is by replenishing stored water as soon as the volume or temperature decreases.With solar powered boilers, this is instead fuelled by the solar power collected through panels on the roof of your home.The power collected through the solar tiles is used to fuel and therefore heat a separate water cylinder, thus saving energy throughout the course of every day.Another smaller tank, still powered by gas, is provided with most solar boiler installations as a backup.
 
boxbanner3.png
boxbanner1.png
bells%20bend%20002%20small.jpg
1290200487_BEST%20(Small).JPG
photo_1%20small.jpg

blueblob.jpg
Solar energy isn't always about generating electricity:
For example, photoluminescent products store light energy and release it later. They're also called "self-luminous" and are a useful source of emergency lighting in the event of a sudden power outage.

blueblob.jpg
Advantages

  • Solar energy is free - it needs no fuel and produces no waste or pollution.
  • In sunny countries, solar power can be used where there is no easy way to get electricity to a remote place.
  • Handy for low-power uses such as solar powered garden lights and battery chargers, or for helping your home energy bills.
blueblob.jpg
Disadvantages

  • Doesn't work at night.
  • Very expensive to build solar power stations, although the cost is coming down as technology improves. In the meantime, solar cells cost a great deal compared to the amount of electricity they'll produce in their lifetime.
  • Can be unreliable unless you're in a very sunny climate. In the United Kingdom, solar power isn't much use for high-power applications, as you need a large area of solar panels to get a decent amount of power. However, technology has now reached the point where it can make a big difference to your home fuel bills.
blueblob.jpg
Is it renewable?
Solar power is renewable. The Sun will keep on shining anyway, so it makes sense to use it.​

 
Nakuhakikishia mkuu kuwa soko lipo tena kubwa na la kibiashara, wewe jipange tu. Tatizo linaweza kuwa TRA, maana huwa hawako wazi hivyo unaweza ukakuta kodi ya ajabu huko. Unasema Rex wako peke yao, hapana hawako peke yao kuna kampuni nyingine tena ila jina lake limenitoka nikumbuka nitakutajia. Ila inaonekana nao pia hawajajipanga vizuri kufanya biashara ya solar, wewe jipange tu soko lipo tena zaidi ya 5% nakuhakikishia.

Soko la Solar linaweza kuwepo lakini si kwa ufanisi. Kama kuanzisha solar kwa malengo ya kufanya biashara nisingeshauri kwa vile hata mataifa yaliyoendela bado biashara hii haina nguvu isipokuwa eneo ambalo hakuna upatikanaji wa umeme. Na pia huduma ambayo haihitaji mtu wa kuangalia kuwepo mara kwa mara kama solar zinazowekwa kwenye highway ambazo hupita porini mbali na makazi ya watu kuweka digital information na mengineyo.

Kwa vyo vyote unahitaji kwanza kuwaelimisha watu umuhimu wa faida ya kutumia solar, na pengine ugumu na kutokuwa na uhakika wa kupata nguvu yake ndio tatizo, kama usiku, na siku mawingu yakitanda kuwa nusu usiku hapo hakuna upatikanaji wa energy.

Mtu anaona bora kutumia kajenereta kake kwa vile ana uhakika ingawa atagharimia mafuta. Ningekushauri kama alivyopendekeza mdau hapo juu fanya utafiti wa kutosha usije poteza mtaji wako kwa huduma na mradi ambao hauna uhakika sana kwani makampuni mengi yameanzisha miradi hiyo lakini inasuasua.
 
Back
Top Bottom