Biashara ya Chakula (mama wa biashara zote)

Hata Kujitolea.

TRUE STORY


Siku moja nilienda mahali kula chipsi,nikaagiza wakaniletea huwa nikienda kula mahali kiepe nawambiaga waweke kila kitu kasoro mayonaize zao tu.

Basi nikaletewa kiepe kwakweli zile chipsi zilikua safi sana sana zinang'aa lakini zaidi pilipili yao ilikua inawasha haswaaa na ni tamu sio kitoto yani unakula pilipili makamasi yanashuka ila bado unailamba.

tukija kwenye kachumbari ndio usiseme sijui ile kachumbari ilikua inatengenezwaje,kusema ukweli zile chipsi sikuwahi kuzila mahali popote tangu nizaliwe.

Kumbuka hapo nina goli la kuuza chipsi namimi sio kwamba sina

ila chipsi zangu si tamu na nzuri kama zile,nikawa nimetamani kweli zile chips na kila kitu cha pale nikawa najiuliza moyoni namimi nifanyeje ili niweze kutoa chipsi za namna hii?

basi next time nikarudi tena nikaagiza vile vile kiepe ila safari hii nilienda kwa lengo la kukagua zile chipsi na pilipili na kila kitu chao ili namm nikatengeneze kwangu,sikwenda kwasababu nilikua na njaa Hapana.

Nlipofika nikaagiza wakaniletea,nikanawa mikono nikainua kipande cha chipsi nikakisogeza machoni kbsa nikawa nakikagua,hiki n kiazi kweli au kuna uziada uliofanyika hadi kiepe kikang'aa vile? kwenye viazi nikagundua kuwa kuna kitu imeongezwa ambayo n rangi,swali n kwamba Je n rangi gani? (hapo nikapaacha)

nikaja kwenye kwenye pilipili nikatia mdomoni nikawa naskilizia kung'amua viungo vilivyotumika ila Nikatoka kapa,Nikaja kwenye kachumbari napo nikatoka kapa sikuweza gundua chochote.

Nikajiuliza sasa nafanyaje? nikienda kule kwangu nikimtuma mfanyakazi wangu mmoja aje ajitolee hapa kwenye hii ofisi atakubaliwa ataingia ila je Huyu mfanyakazi wangu Nitakua nae miaka yote? Jibu hapana.

Nilichoamua n mimi mwenyewe kwenda kuomba kazi ya kujitolea kwenye ile ofisi,Basi SIKU 1 nikadamka saa 10 usiku nikaenda pale nikaomba kazi japo sikumkuta boss nikawa naomba tu kusaidia nikawa nasaidia,mida mida ikafika boss akaja akanikuta akauliza taarifa zangu akaambiwa najitolea tu kufanya kazi.

hakukataa basi nikawa nafanya kazi,ikafika muda wa kachumbari wakawa wanaandalia ndani mimi nipo nnje namenyeshwa viazi,Lengo langu likawa halijatimia,Day 1 ikaisha sikujua chchte kuhusu pilipili wala kachumbari,Ikaja day 2 nikatoka kapa,Day 3 ndio nikaambiiwa niandae pilipili nikaelekezwa jinsi yakuandaa mpk ikakamilika.

Day 4 nikaandaa tena pilipili kweli ikatoka kama ile niliyokua naila,day 5 nikahamia kwenye kachumbari kiufupi nilifanya kazi ile ofisi kama wiki (siku 7) nikaongeza siku nyingine kama 3 mbele maana nakumbuka nilisingizia naumwa ilikua j4 sikwenda kbsa HAPO n baada ya ku master kila kitu.

Wakawa wananipgia sana simu nirudi kazini boss akasema nirudi atakua ananilipa ila nilisingizia nimesafiri nikirudi ntaenda,walisumbua sana ila mwisho wakanipotezea.

Nikarudi kwenye magoli yangu nikawa nawaandalia mimi kachumbari na pilipili,wateja wakapenda nikafundsha wafanyakazi jinsi ya kuandaa,nikazunguka ofisi zote nikatoa somo likaeleweka basi saivi usijiloge ukaja kula kiepe eneo langu maana ndio utakua umenasa hiyo.

Lengo la kusimulia hii kitu refu hivi ni nini?


wakati mwingine tunapaswa kuingia gharama/kupoteza muda ili kupata kitu kizuri Pesa si kitu kama huna akili za kujua uitumie vipi hiyo pesa.

pesa haiwezi kukupikia chakula kitamu,pesa haiwezi kukutengenezea kachumbari nzuri,pesa si kila kitu linapokuja swala la ubunifu ktk biashara unayofanya ili uweze kufikia malengo yako.

na ktk biashara zinazotaka uwe m'bunifu kila siku iendayo leo n biashara ya chakula maana ukizoesha wateja taste flani kila siku wakiizoea wataaanza kuona chakula chako kibaya wakat chakula n kile kile cha siku zote.

ukizoesha wateja aina flani ya kachumbari ukawa unaiandaa hyo hyo kila siku wakiichoka wataanza iona mbaya wakat kachumbari n ile ile,ndio mana biashara ya chakula inataka ubunifu wa hali ya juu Mfano leo ukipika wali wa nazi,kesho unawapikia wali wa kitunguu,kesho kutwa unawapikia wali wa maua Yani haina kukariri chakula cha ofisi yako kiko vipi.

ukipka chai ya rangi leo unapika unaweka viungo hivi,kesho unaweka viungo vile kesho kutwa unawapkia na mchai chai peke yake,nk nk yani hamna kukaririr taste ya chai wala chochote kinachopikwa ktk ofisi yako.

ila ukisema upike chakula kile kile wali aina ile ile,pilau lile lile,chai ile ile,kachumbari,nk nknk aseee utapata wateja ila hutodumu na hao wateja maana wateja n watu wapenda kubadilisha ladha,na hiyo ipo kwa kila mtu duniani.

Kwahyo tunarudi pale pale kuwa ubunifu ktk biashara ya chakula unahitajika sana na ubunifu huu huwezi kuupata kama huzungki ofisi za wengine,hutembelei wenzako,Ukijiona umekua boss ukiamini huwezi tena kuajiriwa wala kushuka chini basi Biashara haikufai na siku 1 isiyo na jina utaanguka na utaanza singizia biashara bila ndumba haiendi wakati si kweli.
 
Unamlipa 8000 kwa startup business na tena watendaji ni wote mbona naona faida ya 2000 ulikuwa unampa yeye ungemlipa 5000-6000 kwa Startup kwanza hii inaonesha na sehemu nyengine umefeli kimahesabu.

mimi ningempa 3000 tu maana kula anakula kazini

na kazi tunafanya wote tunasaidiana,na hii 3000

nampa basi tu ila ki ukweli mtaji wa ndoo 1 siajiri mtu mimi.
 
Sivan hii millioni 1 iliyokushtua ni mauzo tu wala usishtuke sana

Unamaanisha million 1 au labda ngoja nimsubiri Controla.


Nilikujibu hivi ila sikuonyesha kuchanganua hyo millioni n kitu gani

Mkuu 1M ni hela ndogo sana kwenye biashara ya chakula kama

ikitokea ukalenga sehemu sahihi inayoteremsha wateja 24hrs

Biashara ya chakula ikikukubalia nakwambia utaona wafanya biashara

wengine kama wanapoteza tu muda wao kwenye biashara zao acha tu mkuu.

Kuna raia nachat nae pm anadhani hii 1m ni FAIDA aisee hii 1M sio faida hayo n mauzo tu ambayo yaweza kuzidi hata hiyo 1m per day.

lakini tukirudi kwenye faida kama faida unayoweza ipata kufinya 1M kama faida asee hizo ngekewa zipo ila n kwa wafanyabiashara wakubwa kbsa sio wa chipsi,wafanyabiashara wakubwa naongelea kwenye mafestival kama NYAMA CHOMA au matamasha matamasha ya namna hyo.

ila biashara za kitaa kitaa sjui bar,pub,hotel aaah wapi hamna anaekunja faida 1M hayupo na haiwezekani labda awe anaongezea hela zngine huko alikotoa atudanganye n faida.

huko kwenye mitamasha na wenzao wanaweza kukusanya faida hiyo kwasababu hata nyama tu hachinjwi ng'ombe 1 wanaangushwa ng'ombe hata wa tano,mbuzi wanaangushwa wakutosha,na hata kama wanauza chipsi wanakuuzia chipsi kavu sahani 2000 mpk 3000 hiyo n chips kavu tu.

na kipimo cha chips n kile kile cha mtaani ila bei wanapandsha kwasababu pia wanamatumizi mengi,so hiyo 1M aliyokutajia ndugu yako hadi ukashtuka n ya mauzo na si Faida.

Faida
kimtaani mtaani sinza huko boss anaekimbiza kweli kweli faida anachezea kwenye 100k - 300k hiyo n baada ya kulipa wafanyakazi wote kutoa matumizi yote nk nk ndio yeye kama boss anaweza kubaki na faida hyo 100k - 300k ambapo pia hyo nayo haipo constant leo anaweza pata na kesho asipate.Faida ya 1M kimtaa mtaa nakataaa.
 
Nikikumbuka jamaa aliwekeza Bonge la biashara la kisasa BBQ anauza chips na vikorombwezo vyote na wali supu MENU imekamilika location inavutia wafanyakazi Tshirt Marketing mpaka group la whatsApp na Agent jamaa alifanya ubunifu wa Deliver maana wateja wanachuo sasa kule wanapopita sana wanachuo akaweka kibanda ambacho Mobile wanakipeleka na kukirudisha eti baadae akashindwa biashara hakuna faida aisee.
Biashara kila mtu anaweza kuianza kwa ubora na viwango ila ni wachache sana ktk wafanyabiashara wanaoweza kuwa wabunifu kila iitwayo leo ktk hizo biashara wanazozianzisha,

wengi wa wafanyabiashara ni wazee wakuiga wengine yani wana copy na ku paste,biashara uki copy n paste lazima itakubumia tu yani,mfano mwepesi tu ni ;

Huu mtindo wa kuwawekea charger wateja kwenye bar/pub/hotel/ma bus,nk

Jaribu kujiuliza n nani aliyeanzisha utamaduni wa kuweka usb port charger kwenye sehemu ya kukaa wateja? tafuta mtu aliyeweka kwake muulize kwann kaweka hizo usb

Jibu atakalokupa ni "Siku hizi ndio style" au "bar na pub kubwa nyingi na wao wanaweka" yani wengi hawajui hata kwann kamuwekea mteja wake usb port charge ndio maana anaweka

halafu sasa kwa mbwembwe Kila meza yani,wakati haitakiwi ziwekwe hivyo Na hajui hilo kwasababu wazo la usb port charger sio lake yeye n mzee wa copy n paste,

kwa hyo anahisi akizdsha idadi ndio atakua mtoa huduma bora kuliko mwenzake,huyu mtu wa hivi hana muda mrefu kwenye game hafiki hata half time lazima sub ifanyike.

Ndio mana sishtukagi kbsa na wafanyabiashara wakubwa wakubwa wa biashara za mtaani maana najua wengi wanafikiri PESA NDIO KILA KITU na mimi nawaangaliaga tu na pesa zao ila nawahesabia saa tu.
 
Biashara ya chakula ni moja ya biashara nzuri na yenye faida na inayoweza kukutoa from zero to hero ndani ya mwaka wako mmoja tu ukikomaa ipasavyo kazini kwako,lakini ili ikutoe kama inavyotoa wengine ni lazima biashara yako iguse wateja wote bila kubagua.

Biashara nyingi sana hapa mjini zinafeli kwasababu 1 kuuu ambayo ni ubaguzi wa wateja,Acha niwape mfano 1 : Zamani kidogo nilitamani kufanya biashara flani hivi,baaada ya kufanya research zangu za ile biashara ninayotaka kuifanya nikagundua kuwa wauzaji wengine wengi wanauza vitu feki ambavyo si original,nikajisemea moyoni mimi nitakua tofauti na wao nitauza vitu OG tuu.

Basi nikafungua ofisi,nikaipendezesha kimuonekano,Weka mabango ya kisasa kbsa biashara ikaanza kweli nilikua nauza vitu OG OG kama mbele mzee,na bei ya vitu OG nadhani mnazijua jamani Kitu ya bei chee pale ilikua ni ya 25k ila vingine vyote bei zake N za moto.

Picha linaanza Day 1 nimeuza hakuna,Day 2 nkauza Desh,Day 3 nkauza Empty mpk kukatika wiki ya kwanza nilikua nauza maneno na kusifia product zangu,nikawa najipa moyo labda sababu ofisi bado mpya ila wapi ikakatka miezi,nikaona hali inazd kua mbaya nikasema Huu ungedere HAPANA siuwezi.

Nikaagiza mzigo ule ule niliokua nauza ORIGINAL nikaagiza FEKI zake sasa,kisha nika brand duka tena upya,matangazo nikaweka upya Kazi ikaanza tena,yani Mauzo yake siwezi andika hapa ila amini amini nawambia Sikuamini macho yangu kwa hesabu niliyofunga Day 1 tu.

Hii maana yake nini? sio kwamba wateja hawakuepo? wala si kwamba nilikosea eneo la kufungua hyo biashara ila kosa langu kubwa lilikua ni KUTENGA WATEJA (ubaguzi) niliwabagua wateja nikawa nime egemea upande mmoja wa wateja wenye nazo nikawasahau hawa wenzangu namimi wenye uwezo wa kati na wachini kbsa ambao kiuhalisia ndio wengi wengi wengi kuliko hawa wengine.

Turudi kwenye Mada yetu ya Biashara ya chakula ;

Nimesema biashara ya chakula ili ikupe faida na matokeo chanya n lazima iguse wateja wote (usiwe m'baguzi) maana jamii tunayoishi imejaa wateja wa aina zote na ni lazima tuwaguse wote.

Leo nataka kumshauri mtu anaetaka kufanya biashara ya chakula kwa kufata IDEA yangu nitakayoichambua hapa chini mwanzo mpk mwisho wa thread hii.

KUUZA CHIPS

Hii ni biashara ya chakula tofauti na vyakula vingine ambayo naipenda kwasababu ni biashara unayoweza ifanya kuanzia asubuhi saa 1 kamili na ukaenda nayo 24hrs watu wakala bila kuchoka,

Chipsi ni chakula kinacholika na kupendwa na rika zote,chipsi ni chakula kisicho na muda maalum kulika ndio maana ukiingia k.koo asubuhi saa 1 utakuta raia wanagonga chai maziwa na chips zege hii n kwasababu chipsi inasimama kote kote yani kama kitafunwa,kama mlo mkuu,kama Bites,NK yani kama n chakula kisicho na jinsia basi ni CHIPSI.

Sasa hii chips unauzaje ili uguse wateja wote? kipimo cha chipsi kavu kwa wakazi wa dar sio chini ya 1500 na sehemu chache chache sana huko ndan ndani ndio unaweza ukaomba ukapimiwa hata za 1000 ila hapo n uombe sana au uwe member unaejulikana na umkute muuzaji yupo kwenye mood hiyo siku.

Sasa basi ktk biashara yetu hii ya chipsi tukisema twende kwa bei kipimo 1500/1000 bado tutasurvive kwa muda mchache sana lakni mwisho tutaanguka kabisa kwasababu kiuhalisia buku au buku jero bado n pesa wachache sana wanaimudu (ukweli ndio huu) anaweza imudu kwa leo lakini hatoweza imudu kwa kesho,kesho kutwa,ijumaa,jmos na kuendelea.

Sasa kwann tufanye biashara ambayo uhakika n mpk mteja mfuko uwe vzuri ndio aje? Hamna sababu hiyo,Tufanyeje sasa? Katika biashara yetu ya chipsi ambayo muda wakufungua n saa 1 kamili asubuhi kabati limeshapendeza tutakua tunauza

  • chips
  • mihogo/viazi vitamu (utachagua uweke kipi)
  • ndizi mzuzu (za jero na za 200)
  • mishkaki (ya buku,ya jero, ya 200 na ya 100)
  • Kuku (firigisi/shingo/miguu/vichwa)
  • soseji
  • viazii vya kacholi

Katika vitu vyetu hivyo hapo juu sio lazima ununue gunia la viazi kwasababu ndio tunaanza unaweza ukaaanza na ndoo mbili tu kubwa za viazi au hata 1 kutegemea na uwezo wako,

kwenye mihogo hapa napo muhimu chukua mihogo ya 15,000 au hata 20,000 kutegemea na eneo ulipo,ndizi mzuzu hizi nazo unaweza ukafata mkungu wenye ndizi ndogo ndogo kbsa au

ukaenda kununua zile za mafungu ndogo ndogo utakazouza 200 na ukanunua na zle mzuzu kubwa utakazoweza uza 500.

Mishkaki nunua kulingana na mfuko wako muhimu uweze kujua kuikata kwa kipimo finyango za buku,za jero,200 na 100 na vitu vingine upendavyo kama hizo kacholi kama unaweza tengeneza usiache hakikisha unaziweka hata kama huwezi tafuta mtu anaeweza Muajiri atengeneze kachori utakazouza sh.100 kwa moja.

Hivi vitu nilivyotaja vinaweza kuonekana ni vingi na kweli n vingi kwasababu nataka tuwe tofauti na wauza chipsi wengine wote eneo tutakalofungua na lengo la kuweka vitu vingi hivi ni ili kuweza pata watu aina zote,

Nilisema hapo awali kwamba Hapa Dar na sehemu nyingi sana ili weze kupata mlo wa mchana au usiku n lazima kila mlo usiwe na chini ya 1000 maana yake n kwamba mchana 1000 usiku 1000,sasa kwenye hiii ofisi yetu nataka Wale wenye jero jero zao nao wakitaka kula wale washibe.

mteja akija na jero akataka mihogo ambayo sisi tunauza sh.200 tutampa mihogo miwili,ile sh 100 tutampa kacholi 1 na tutamuwekea chpsi chombeza ile sahani yake ukiweka na kachumbari zetu atapokea sahani ina mlima atakula atashushia na maji yetu ya kandoro ya bure ya mezani Ataondoka kashiba vizuri kabisa,

huyu mteja kurudi tena kwetu sio ombi n lazima tU Maana hamna mahali pengine popote atakapoenda na jero akala akashiba tofauti na kwetu.

View attachment 1526858

wakija wateja V.I.P wale wanaotaka mshkaki wa buku,kidari cha 2500 soseji mayai nao tunaenda nao sawa vile vile hii biashara yetu haina uchawi hta uwe uchochoro gani biashara lazima utusue na ufanye vizuri tu.

Mihogo sio asubuhi tu mihogo kazin kwetu itapatkana muda wote ofisi itakapokua wazi,ndizi kadhalika,kacholi kadhalika hatuanzi na nguvu ya soda speed hii hii tutaenda nayo hadi mwisho.

Mtaji wa hii biashara yetu kwa makadirio ya chini kbsa kwa mtu mwenye vyombo vyote ni kama 300,000 na kwa mtu aasie na vyombo maana yake gharama itapanda zaidi lakini Ukiwa na 500,000 - 600,000 unaweza ukaianza hii biashara kibishi bishi mpk utakapoimarika kabisa.

Faida utakayoipata kwenye biashara hii kama upo sehemu nzuri umelenga na ukaiweka biashara kama mimi ninavyoipigia picha huku kichwani kwangu kukunja faida ya 100,000k per day ni jambo la kawaida kbsa,ambapo ukitoa matumizi ukalipa wafanyakazi wako wewe kubaki na 40,000 - 50,000 ni jambo la kawaida sanaaaaaaaa.View attachment 1526867

Kuna watu wanasemaga hizi ni theory hazina uhalisia SAWA SAWA kbsa acha sisi wazee wa theory tuthiorike ila mfano wa biashara hii ya chips ipo Magomeni usalama na nyingine ipo K.koo Aggrey na likoma opposite na POSTAL BANK kuna chaliii ya R chuga iko pale inajua biashara mpk inaboa,akikupmia chipsi ya buku unaweza sema kateleza mkono jinsi anavyomwagia kwenye hiyo sahani.

Hela haweki kwenye epron Hela anatupia kwenye ndoo kubwa Jioni hesabu anayofunga,wewe na duka lako unaweza ukaipata kwa wiki nzima ila mtu anaikunja kwa siku 1.

Kama upo Dar na una mtaji Nakuhakikishia hii biashara ipo siku 1 utakuja toa ushuhuda.Usiache ifanya.Funga macho ifanye Hutojutia nakuhakikishia.

I dedicate this thread kwa watafutaji wote wasiochoka na wenye malengo na wasioridhika na biashara moja kiufupi kwa wapiganaji wote waliopo ndani ya JF amu MAMA nakuaminia sana sana,najua huchokagi wala hujawahi kuchoka,ongezea na hiii.
Shukurani sana
 
TRUE STORY


Siku moja nilienda mahali kula chipsi,nikaagiza wakaniletea huwa nikienda kula mahali kiepe nawambiaga waweke kila kitu kasoro mayonaize zao tu.

Basi nikaletewa kiepe kwakweli zile chipsi zilikua safi sana sana zinang'aa lakini zaidi pilipili yao ilikua inawasha haswaaa na ni tamu sio kitoto yani unakula pilipili makamasi yanashuka ila bado unailamba.

tukija kwenye kachumbari ndio usiseme sijui ile kachumbari ilikua inatengenezwaje,kusema ukweli zile chipsi sikuwahi kuzila mahali popote tangu nizaliwe.

Kumbuka hapo nina goli la kuuza chipsi namimi sio kwamba sina

ila chipsi zangu si tamu na nzuri kama zile,nikawa nimetamani kweli zile chips na kila kitu cha pale nikawa najiuliza moyoni namimi nifanyeje ili niweze kutoa chipsi za namna hii?

basi next time nikarudi tena nikaagiza vile vile kiepe ila safari hii nilienda kwa lengo la kukagua zile chipsi na pilipili na kila kitu chao ili namm nikatengeneze kwangu,sikwenda kwasababu nilikua na njaa Hapana.

Nlipofika nikaagiza wakaniletea,nikanawa mikono nikainua kipande cha chipsi nikakisogeza machoni kbsa nikawa nakikagua,hiki n kiazi kweli au kuna uziada uliofanyika hadi kiepe kikang'aa vile? kwenye viazi nikagundua kuwa kuna kitu imeongezwa ambayo n rangi,swali n kwamba Je n rangi gani? (hapo nikapaacha)

nikaja kwenye kwenye pilipili nikatia mdomoni nikawa naskilizia kung'amua viungo vilivyotumika ila Nikatoka kapa,Nikaja kwenye kachumbari napo nikatoka kapa sikuweza gundua chochote.

Nikajiuliza sasa nafanyaje? nikienda kule kwangu nikimtuma mfanyakazi wangu mmoja aje ajitolee hapa kwenye hii ofisi atakubaliwa ataingia ila je Huyu mfanyakazi wangu Nitakua nae miaka yote? Jibu hapana.

Nilichoamua n mimi mwenyewe kwenda kuomba kazi ya kujitolea kwenye ile ofisi,Basi SIKU 1 nikadamka saa 10 usiku nikaenda pale nikaomba kazi japo sikumkuta boss nikawa naomba tu kusaidia nikawa nasaidia,mida mida ikafika boss akaja akanikuta akauliza taarifa zangu akaambiwa najitolea tu kufanya kazi.

hakukataa basi nikawa nafanya kazi,ikafika muda wa kachumbari wakawa wanaandalia ndani mimi nipo nnje namenyeshwa viazi,Lengo langu likawa halijatimia,Day 1 ikaisha sikujua chchte kuhusu pilipili wala kachumbari,Ikaja day 2 nikatoka kapa,Day 3 ndio nikaambiiwa niandae pilipili nikaelekezwa jinsi yakuandaa mpk ikakamilika.

Day 4 nikaandaa tena pilipili kweli ikatoka kama ile niliyokua naila,day 5 nikahamia kwenye kachumbari kiufupi nilifanya kazi ile ofisi kama wiki (siku 7) nikaongeza siku nyingine kama 3 mbele maana nakumbuka nilisingizia naumwa ilikua j4 sikwenda kbsa HAPO n baada ya ku master kila kitu.

Wakawa wananipgia sana simu nirudi kazini boss akasema nirudi atakua ananilipa ila nilisingizia nimesafiri nikirudi ntaenda,walisumbua sana ila mwisho wakanipotezea.

Nikarudi kwenye magoli yangu nikawa nawaandalia mimi kachumbari na pilipili,wateja wakapenda nikafundsha wafanyakazi jinsi ya kuandaa,nikazunguka ofisi zote nikatoa somo likaeleweka basi saivi usijiloge ukaja kula kiepe eneo langu maana ndio utakua umenasa hiyo.

Lengo la kusimulia hii kitu refu hivi ni nini?


wakati mwingine tunapaswa kuingia gharama/kupoteza muda ili kupata kitu kizuri Pesa si kitu kama huna akili za kujua uitumie vipi hiyo pesa.

pesa haiwezi kukupikia chakula kitamu,pesa haiwezi kukutengenezea kachumbari nzuri,pesa si kila kitu linapokuja swala la ubunifu ktk biashara unayofanya ili uweze kufikia malengo yako.

na ktk biashara zinazotaka uwe m'bunifu kila siku iendayo leo n biashara ya chakula maana ukizoesha wateja taste flani kila siku wakiizoea wataaanza kuona chakula chako kibaya wakat chakula n kile kile cha siku zote.

ukizoesha wateja aina flani ya kachumbari ukawa unaiandaa hyo hyo kila siku wakiichoka wataanza iona mbaya wakat kachumbari n ile ile,ndio mana biashara ya chakula inataka ubunifu wa hali ya juu Mfano leo ukipika wali wa nazi,kesho unawapikia wali wa kitunguu,kesho kutwa unawapikia wali wa maua Yani haina kukariri chakula cha ofisi yako kiko vipi.

ukipka chai ya rangi leo unapika unaweka viungo hivi,kesho unaweka viungo vile kesho kutwa unawapkia na mchai chai peke yake,nk nk yani hamna kukaririr taste ya chai wala chochote kinachopikwa ktk ofisi yako.

ila ukisema upike chakula kile kile wali aina ile ile,pilau lile lile,chai ile ile,kachumbari,nk nknk aseee utapata wateja ila hutodumu na hao wateja maana wateja n watu wapenda kubadilisha ladha,na hiyo ipo kwa kila mtu duniani.

Kwahyo tunarudi pale pale kuwa ubunifu ktk biashara ya chakula unahitajika sana na ubunifu huu huwezi kuupata kama huzungki ofisi za wengine,hutembelei wenzako,Ukijiona umekua boss ukiamini huwezi tena kuajiriwa wala kushuka chini basi Biashara haikufai na siku 1 isiyo na jina utaanguka na utaanza singizia biashara bila ndumba haiendi wakati si kweli.
Nakukubali sana mkuu.
 
Ubarikiwe sana... Thread zako zimenibadilisha sana...
Kwakweli mimi nilikuwa ni yule jamaa anaye-plan kufungua biashara ila daily naghairisha kwa visingizio lukuki eti mtaji ninaodhamiria haujatimia,
Mara location ninayoitaka bado sijaipata yaani nadharia mwanzo mwisho...

Ila thread zako zimenifanya niwe na uthubutu mkubwa mno..

Mpaka sasa umechangia pakubwa kwa mimi kuanzisha miradi yangu mipya bila kuwaza na kilakitu kinasonga poa...

Sikuhizi sighairishi vitu...
Nikilala na idea basi nikiamka tu nafanya action... No delay...

Shukran.

Sent from my kitochi using JamiiForums mobile app
Nafarijika sana nikisoma shuhuda za namna hii

Asante kwa moyo wa shukurani chief,ubarikiwe!
 
Biashara ya chakula ni moja ya biashara nzuri na yenye faida na inayoweza kukutoa from zero to hero ndani ya mwaka wako mmoja tu ukikomaa ipasavyo kazini kwako,lakini ili ikutoe kama inavyotoa wengine ni lazima biashara yako iguse wateja wote bila kubagua.

Biashara nyingi sana hapa mjini zinafeli kwasababu 1 kuuu ambayo ni ubaguzi wa wateja,Acha niwape mfano 1 : Zamani kidogo nilitamani kufanya biashara flani hivi,baaada ya kufanya research zangu za ile biashara ninayotaka kuifanya nikagundua kuwa wauzaji wengine wengi wanauza vitu feki ambavyo si original,nikajisemea moyoni mimi nitakua tofauti na wao nitauza vitu OG tuu.

Basi nikafungua ofisi,nikaipendezesha kimuonekano,Weka mabango ya kisasa kbsa biashara ikaanza kweli nilikua nauza vitu OG OG kama mbele mzee,na bei ya vitu OG nadhani mnazijua jamani Kitu ya bei chee pale ilikua ni ya 25k ila vingine vyote bei zake N za moto.

Picha linaanza Day 1 nimeuza hakuna,Day 2 nkauza Desh,Day 3 nkauza Empty mpk kukatika wiki ya kwanza nilikua nauza maneno na kusifia product zangu,nikawa najipa moyo labda sababu ofisi bado mpya ila wapi ikakatka miezi,nikaona hali inazd kua mbaya nikasema Huu ungedere HAPANA siuwezi.

Nikaagiza mzigo ule ule niliokua nauza ORIGINAL nikaagiza FEKI zake sasa,kisha nika brand duka tena upya,matangazo nikaweka upya Kazi ikaanza tena,yani Mauzo yake siwezi andika hapa ila amini amini nawambia Sikuamini macho yangu kwa hesabu niliyofunga Day 1 tu.

Hii maana yake nini? sio kwamba wateja hawakuepo? wala si kwamba nilikosea eneo la kufungua hyo biashara ila kosa langu kubwa lilikua ni KUTENGA WATEJA (ubaguzi) niliwabagua wateja nikawa nime egemea upande mmoja wa wateja wenye nazo nikawasahau hawa wenzangu namimi wenye uwezo wa kati na wachini kbsa ambao kiuhalisia ndio wengi wengi wengi kuliko hawa wengine.

Turudi kwenye Mada yetu ya Biashara ya chakula ;

Nimesema biashara ya chakula ili ikupe faida na matokeo chanya n lazima iguse wateja wote (usiwe m'baguzi) maana jamii tunayoishi imejaa wateja wa aina zote na ni lazima tuwaguse wote.

Leo nataka kumshauri mtu anaetaka kufanya biashara ya chakula kwa kufata IDEA yangu nitakayoichambua hapa chini mwanzo mpk mwisho wa thread hii.

KUUZA CHIPS

Hii ni biashara ya chakula tofauti na vyakula vingine ambayo naipenda kwasababu ni biashara unayoweza ifanya kuanzia asubuhi saa 1 kamili na ukaenda nayo 24hrs watu wakala bila kuchoka,

Chipsi ni chakula kinacholika na kupendwa na rika zote,chipsi ni chakula kisicho na muda maalum kulika ndio maana ukiingia k.koo asubuhi saa 1 utakuta raia wanagonga chai maziwa na chips zege hii n kwasababu chipsi inasimama kote kote yani kama kitafunwa,kama mlo mkuu,kama Bites,NK yani kama n chakula kisicho na jinsia basi ni CHIPSI.

Sasa hii chips unauzaje ili uguse wateja wote? kipimo cha chipsi kavu kwa wakazi wa dar sio chini ya 1500 na sehemu chache chache sana huko ndan ndani ndio unaweza ukaomba ukapimiwa hata za 1000 ila hapo n uombe sana au uwe member unaejulikana na umkute muuzaji yupo kwenye mood hiyo siku.

Sasa basi ktk biashara yetu hii ya chipsi tukisema twende kwa bei kipimo 1500/1000 bado tutasurvive kwa muda mchache sana lakni mwisho tutaanguka kabisa kwasababu kiuhalisia buku au buku jero bado n pesa wachache sana wanaimudu (ukweli ndio huu) anaweza imudu kwa leo lakini hatoweza imudu kwa kesho,kesho kutwa,ijumaa,jmos na kuendelea.

Sasa kwann tufanye biashara ambayo uhakika n mpk mteja mfuko uwe vzuri ndio aje? Hamna sababu hiyo,Tufanyeje sasa? Katika biashara yetu ya chipsi ambayo muda wakufungua n saa 1 kamili asubuhi kabati limeshapendeza tutakua tunauza

  • chips
  • mihogo/viazi vitamu (utachagua uweke kipi)
  • ndizi mzuzu (za jero na za 200)
  • mishkaki (ya buku,ya jero, ya 200 na ya 100)
  • Kuku (firigisi/shingo/miguu/vichwa)
  • soseji
  • viazii vya kacholi

Katika vitu vyetu hivyo hapo juu sio lazima ununue gunia la viazi kwasababu ndio tunaanza unaweza ukaaanza na ndoo mbili tu kubwa za viazi au hata 1 kutegemea na uwezo wako,

kwenye mihogo hapa napo muhimu chukua mihogo ya 15,000 au hata 20,000 kutegemea na eneo ulipo,ndizi mzuzu hizi nazo unaweza ukafata mkungu wenye ndizi ndogo ndogo kbsa au

ukaenda kununua zile za mafungu ndogo ndogo utakazouza 200 na ukanunua na zle mzuzu kubwa utakazoweza uza 500.

Mishkaki nunua kulingana na mfuko wako muhimu uweze kujua kuikata kwa kipimo finyango za buku,za jero,200 na 100 na vitu vingine upendavyo kama hizo kacholi kama unaweza tengeneza usiache hakikisha unaziweka hata kama huwezi tafuta mtu anaeweza Muajiri atengeneze kachori utakazouza sh.100 kwa moja.

Hivi vitu nilivyotaja vinaweza kuonekana ni vingi na kweli n vingi kwasababu nataka tuwe tofauti na wauza chipsi wengine wote eneo tutakalofungua na lengo la kuweka vitu vingi hivi ni ili kuweza pata watu aina zote,

Nilisema hapo awali kwamba Hapa Dar na sehemu nyingi sana ili weze kupata mlo wa mchana au usiku n lazima kila mlo usiwe na chini ya 1000 maana yake n kwamba mchana 1000 usiku 1000,sasa kwenye hiii ofisi yetu nataka Wale wenye jero jero zao nao wakitaka kula wale washibe.

mteja akija na jero akataka mihogo ambayo sisi tunauza sh.200 tutampa mihogo miwili,ile sh 100 tutampa kacholi 1 na tutamuwekea chpsi chombeza ile sahani yake ukiweka na kachumbari zetu atapokea sahani ina mlima atakula atashushia na maji yetu ya kandoro ya bure ya mezani Ataondoka kashiba vizuri kabisa,

huyu mteja kurudi tena kwetu sio ombi n lazima tU Maana hamna mahali pengine popote atakapoenda na jero akala akashiba tofauti na kwetu.

View attachment 1526858

wakija wateja V.I.P wale wanaotaka mshkaki wa buku,kidari cha 2500 soseji mayai nao tunaenda nao sawa vile vile hii biashara yetu haina uchawi hta uwe uchochoro gani biashara lazima utusue na ufanye vizuri tu.

Mihogo sio asubuhi tu mihogo kazin kwetu itapatkana muda wote ofisi itakapokua wazi,ndizi kadhalika,kacholi kadhalika hatuanzi na nguvu ya soda speed hii hii tutaenda nayo hadi mwisho.

Mtaji wa hii biashara yetu kwa makadirio ya chini kbsa kwa mtu mwenye vyombo vyote ni kama 300,000 na kwa mtu aasie na vyombo maana yake gharama itapanda zaidi lakini Ukiwa na 500,000 - 600,000 unaweza ukaianza hii biashara kibishi bishi mpk utakapoimarika kabisa.

Faida utakayoipata kwenye biashara hii kama upo sehemu nzuri umelenga na ukaiweka biashara kama mimi ninavyoipigia picha huku kichwani kwangu kukunja faida ya 100,000k per day ni jambo la kawaida kbsa,ambapo ukitoa matumizi ukalipa wafanyakazi wako wewe kubaki na 40,000 - 50,000 ni jambo la kawaida sanaaaaaaaa.View attachment 1526867

Kuna watu wanasemaga hizi ni theory hazina uhalisia SAWA SAWA kbsa acha sisi wazee wa theory tuthiorike ila mfano wa biashara hii ya chips ipo Magomeni usalama na nyingine ipo K.koo Aggrey na likoma opposite na POSTAL BANK kuna chaliii ya R chuga iko pale inajua biashara mpk inaboa,akikupmia chipsi ya buku unaweza sema kateleza mkono jinsi anavyomwagia kwenye hiyo sahani.

Hela haweki kwenye epron Hela anatupia kwenye ndoo kubwa Jioni hesabu anayofunga,wewe na duka lako unaweza ukaipata kwa wiki nzima ila mtu anaikunja kwa siku 1.

Kama upo Dar na una mtaji Nakuhakikishia hii biashara ipo siku 1 utakuja toa ushuhuda.Usiache ifanya.Funga macho ifanye Hutojutia nakuhakikishia.

I dedicate this thread kwa watafutaji wote wasiochoka na wenye malengo na wasioridhika na biashara moja kiufupi kwa wapiganaji wote waliopo ndani ya JF amu MAMA nakuaminia sana sana,najua huchokagi wala hujawahi kuchoka,ongezea na hiii.
haya ndo madini tuyatakayo sasa
 
Back
Top Bottom