Uchaguzi 2020 Bernard Membe achukua fomu ya kugombea Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo

Leo tarehe 17 Julai 2020, Waziri wa Mambo ya Nje Mstaafu na Mwanachama wa ACT Wazalendo Ndugu Bernard Membe atazungumza na waandishi wa habari.

Ukumbi: Ofisi ya ACT Wazalendo Magomeni, Dar es salaam.

Muda: Saa 8.00 Mchana.

Waandishi wote mnakaribishwa.

Janeth Rithe, Naibu Katibu wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma, ACT Wazalendo.

17 Julai 2020.

=========

UPDATES

========

Waziri Mstaafu wa Mambo ya Nje Mstaafu Tanzania Bernard Membe mchana huu amechukua fomu ya kugombea Urais kupitia chama cha ACT WAZALENDO ikiwa ni siku moja tu baada ya kupokewa rasmi kwenye Chama hicho.

Bernard Kamilius Membe alizaliwa tarehe 9 Novemba, 1953, Rondo, Chiponda, katika Mkoa wa Lindi, akiwa ni mtoto wa pili kati wa watoto saba (7) waliozaliwa katika familia ya Mzee Kamillius Anthony Ntachile na Mama Cecilia John Membe. Kwa kabila, Bernard Membe ni Mmwera, na kama ilivyo desturi ya Wamwera, watoto hutumia jina la ukoo wa Mama. Hivyo watoto wote saba wa familia hii ya Mzee Kamillius wamekuwa wanatumia jina la upande wa mama yao, Cecilia, yaani Membe.

Siasa:
Ndugu Membe ametumikia nafasi mbalimbali ikiwemo Kamanda wa Vijana wa Mkoa wa Lindi, Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa, na Katibu wa Secretariat ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa. Mwaka 2000, aliingia Bungeni baada ya kuchaguliwa na wananchi wa jimbo la Mtama, kuwawakilisha katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Licha ya uchanga wake bungeni, akiwa kama mbunge wa kawaida (back bencher), Bernard Membe alikuwa mchangiaji mkubwa wa mijadala inayohusu Amani, Ulinzi na Usalama pamoja na Utawala Bora.

Mwaka 2005, Bernard Membe alichaguliwa tena na wananchi wa Jimbo la Mtama kuwawakilisha katika Bunge la Jamhuri ya Muungano. Tofauti na kipindi cha nyuma, Bernard Membe alianza muhula wa pili wa Ubunge, Januari 2006, kama ‘front bencher’ baada ya kuteuliwa na rais Jakaya Mrisho Kikwete kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani. Kufuatia mabadiliko ya baraza la Mawaziri mnamo mwezi Oktoba, 2006, Bernard Membe alihamishwa Wizara na kuwa Naibu Waziri katika Wizara ya Nishati na Madini – moja ya wizara ngumu na nyeti kwa Taifa.

Hata hivyo miezi michache baadae, yaani January 2007, rais Jakaya Mrisho Kikwete alimteua Bernard Membe kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa baada ya aliyakuwa anashikilia wadhifa huo - Dr Asha Rose Migiro - kuteuliwa na Katibu Mkuu Baraza la Umoja wa Kimataifa na kuwa Naibu Katibu mkuu wa baraza hilo. Bernard Membe amehudu katika nafasi hiyo ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa tangu 2007 hadi 2015, akiwa ni Mtanzania wa pili kushika wadhifa huo kwa miaka mingi mfululizo, akitanguliwa na Rais Kikwete ambaye alidumu katika Wizara hiyo kwa miaka 10 mfululizo.

Mafanikio:
Bernard Membe ameongoza Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kipindi ambacho Tanzania na dunia, kwa ujumla, ilikabiliwa na changamoto kubwa katika mambo mbalimbali yanahusiana na ulinzi na usalama, uchumi na ajira (hasa kwa vijana). Changamoto hizo zimepelekea hali ya amani kwa ujumla kutetereka katika maeneo mengi ya dunia.

Hata hivyo, chini ya uongozi wa Bernard Membe, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimatafa, Tanzania imeendelea kuwa mtetezi na mshirika mkubwa wa ulinzi na usalama ndani ya Ukanda wa Afrika na duniani. Tanzania imeshiriki kuleta amani katika nchi za Maziwa makuu yaani, DRC, Burundi na Malawi, lakini pia Tanzania imeshiriki katika utatuzi wa migogoro ya kisiasa katika nchi za Comoro, Madagasca, na Sudan ya Kusini. Aidha, Tanzania imekuwa mshiriki mzuri katika kuchangia vikosi vya kulinda amani katika mataifa ambayo yalipata machafuko kisiasa.

Zaidi, soma:

CCM yamfukuza uanachama Bernard Membe, Kinana apewa karipio kali huku Makamba akitoka salama

News Alert: - Bernard Membe apokelewa rasmi ACT–Wazalendo. Atoa ahadi kemkem endapo watashika madaraka

Uchaguzi 2020 - Bernard Kamilius Membe: Nitagombea Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo

Wasifu wa Bernard Kamilius Membe

Afadhali na yeye amepata nafasi ya kupokea kibegi hicho, huenda itamsaidia kuondoa msononeko wa akili. Lowasa alipata kubeba kibegi hicho kutokea CHADEMA na kuahidi mafuriko ambayo hayakutokea lakini sasa hivi hana msononeko tena. Baada ya uchaguzi, nadhani hatakuwa na msononeko wala kelele tena.
 
zitto karamba joker sisi red bregedia tunaumia sana katuzidi ujanja bwana zuberi
 
Wanajamvi.
Kwanza tuweke sawa vitu.
Hapo awali kugombea uraisi kwa upinzani hakujawahi kuwa kitu rahisi au chepesi sana,huwa ni maamuzi mazito ya kujikana nafsi yako na kubeba msalaba wako mwenyewe.

Wepesi huu ulianza kujengeka mwaka 2015 baada ya sisi wenyewe kujiaminisha kwamba hatuwezi kuing'oa MCC wenyewe ila mpaka MCC "wenyewe" waje watusaidie kuing'oa (wajing'oe wenyewe).

Inafikirisha sana leo mtu kuweza kuongelea uamuzi wake wa kuing'oa MCC kwa aya mbili tu,huku kiu yake ikiwa kuungana wapinzani na wamsimamishe yeye.

Kwamba "kaombwa" pale Mlimani city,kapanda Range rover yake,kurudi kwake "ushuani" kaenda kutafakari na mkewe usiku kucha halafu asubuhi amekubali kubeba hiyo dhamana ya machozi,jasho na damu ya kuing'oa MCC yenye umri wa kikongwe madarakani. Aisee

Kwa upande mwingine: TL (simpigii chapuo) mwisho wa mwezi anakuja. Atadakwa fasta kwa kisingizio cha kesi za kuungwa ungwa. Usiku huo wa kuja TL "Elites" hawatalala na atadakwa hapo hapo uwanjani.
Maskini kaamua kujikana TL.Hayupo upande wao,hashiriki meza yao,hana urafiki nao na shilingi yao kaikataa. Usiku huo "wa kudakwa kwa TL,kwa kuwa ni mwisho wa mwezi "jasusi mbobezi" na "Kijana wa Mwandiga" wao watakuwa "ushuani" Masaki au Oysterbay wamelala na wake zao,wana amani tele moyoni huku wakisubiri kutimiza mpango wao oktoba 2020 na wapewe chao.

Mkutano wao haukuvamiwa,kubanwa kibali wala kuingiliwa na makamanda hapo Mlimani city. Walikula na kunywa huku wakigonga glasi na wala hela ya kampeni kwao haikuwa ajenda. Chama ambacho hakipo katika paycheck ya ruzuku hakiumizi kichwa kumzungusha Mgombea wake wa uraisi nchi kubwa kama Tanzania! Hela anakuja nayo "Mbobezi" ha ha ha.

Mpango wa siku nyingi
"Elites" kama alivyoada wao mwisho wa uchaguzi ndio mwanzo wa kuandaa uchaguzi mwingine.

Mbobezi ni trap na lengo lao ni kupunguza kura za CDM na kuitoa katika "key opposition",misheni ya muda mrefu sana na mratibu ni ZK.

Kama ilivyokuwa 2015,imepangwa chama dola washindane wao kwa wao huku tukipiga kelele na kuwashangilia.

Mbobezi akimaliza uchaguzi huu,MCC watamrudishia uanachama "kimasihara" kama walivyomfukuza "kimasihara".

ZK mpango wake ni kugombea 2025 ambapo atakuwa ametimiza lengo la kuimaliza CDM kama chama kikuu cha upinzani bara na CUF kufutika visiwani.

ZK anahitaji ruzuku bara na visiwani kuelekea 2025.

Mbobezi yeye yupo kazini,"Elites" walitengeneza na kwa makusudi amepewa yeye atakeleze huo "Mpango".

Kila kitu atapata Mbobezi,mabango,bendera,chopa,posho,magari na atafika kila kijiji hapa bongo kujinadi. Kwa siku 60 za kampeni hawatapungukiwa hata mafuta achilia mbali mabango. Kama 2015 kwa EL vijana walitundika bendera za CDM "Made-in-China" kwenye miti.

Wacha picha iendelee bwana.

Wasaalam

"Ukiwa na subra,utaona mwisho wa kila kitu.

"Upepo ukivuma sana,uchi wa kuku huonekana"
 
Ccm Mwisho Wenu Umekaribia...


Nchi Yetu Sote...


Na Mwaka Huu Mtaelewa kwa nini Kaka Man Aliimba Kama Noma na Iwe Noma.
 
The second incidence, the repeated blunder done with our juvinile opposition parties
 
Hi kuna tofauti gani kati ya kugombea "URAIS" na kugombea "KITI CHA RAIS"?

1595043101107.png

1595043140037.png

1595043606585.png





=============================================================================





1595043175810.png

1595043216422.png

1595043802465.png
 
Kipindi chake Tanzania iliyumba kimahusiano na Rwanda,Malawi na ilifanya uvamizi haramu huko comoro!
 
Okay tujibizane kwa hoja.

Sheria zina reference point ama grounds. Sheria zote zimetungwa baada ya kuchambua jema na baya "Morals".

Morals karibu zote tulizonazo zilikuepo kabla hata ya kuzaliwa (pia kabla ya wananchi wote waliopo hai leo).

Pia tunaweza vutana kwa hoja milele nani mwanzilishi wa Morals kati ya Mungu au mwanadamu tusimalize leo.
Eeenh mkuu 'Alpha 13'.

Wewe ungekuwa mwanafunzi wangu unapata yai hapo hapo!

Unatoka kwenye mada unapiga zako kusikohusika kabisa na mada.
 
Usimfanye mwalimu akuone wewe hufundishiki.

Huwezi kusoma majibizano yalipoanzia ukajua umetoka nje ya somo? Sasa unataka ulishwe kabisa?
Some lilikua wananchi vs sheria. Mwenzangu alitegemea niwatetee wananchi, nilipochangua upande wa sheria akajanikosoa "wananchi ndio watunga sheria kupitia wawakilishi". Nikamjibu sheria zinatungwa kutoka kwenye morals "elimu ya mema na mabaya" ambayo ilikuepo kabla ya wananchi wote tuliopo sasa.

Ili kupunguza mvutano nikaenda hatua moja mbele kuonyesha chimbuko la elimu hii ya mema na mabaya mizizi yake ipo kwa Mungu.

Point yangu ni hii; sheria ndio muongozo, viongozi inawapasa wazisimamie pia wawe mfano kwa kuzitii ili wananchi wote tuzifuate.
 
Kwa upande mwingine: TL (simpigii chapuo) mwisho wa mwezi anakuja. Atadakwa fasta kwa kisingizio cha kesi za kuungwa ungwa. Usiku huo wa kuja TL "Elites" hawatalala na atadakwa hapo hapo uwanjani.
Maskini kaamua kujikana TL.Hayupo upande wao,hashiriki meza yao,hana urafiki nao na shilingi yao kaikataa. Usiku huo "wa kudakwa kwa TL,kwa kuwa ni mwisho wa mwezi "jasusi mbobezi" na "Kijana wa Mwandiga" wao watakuwa "ushuani" Masaki au Oysterbay wamelala na wake zao,wana amani tele moyoni huku wakisubiri kutimiza mpango wao oktoba 2020 na wapewe chao.
Mtatunga sana hizi hadithi zisizo na miguu wala vichwa.

Tundu Lissu, atakuja hapa kama shujaa anayekuja kuikomboa nchi toka utumwani.

Hakuna shujaa aliyeogopa kujitoa maisha yake kuikomboa nchi yake.

Kuwekwa ndani sio mwisho wa mapambano, ni mwanzo tu wa mapambano hayo.

Kwa hiyo msiitumie vitisho vya Lissu kuwekwa ndani kama kinga yenu ya kuendelea kuwakandamiza wananchi wa taifa hili. Lissu ni sehemu tu ya mapambano ambayo hamuwezi kuyazima sasa.
 
Some lilikua wananchi vs sheria. Mwenzangu alitegemea niwatetee wananchi, nilipochangua upande wa sheria akajanikosoa "wananchi ndio watunga sheria kupitia wawakilishi". Nikamjibu sheria zinatungwa kutoka kwenye morals "elimu ya mema na mabaya" ambayo ilikuepo kabla ya wananchi wote tuliopo sasa.

Ili kupunguza mvutano nikaenda hatua moja mbele kuonyesha chimbuko la elimu hii ya mema na mabaya mizizi yake ipo kwa Mungu.

Point yangu ni hii; sheria ndio muongozo, viongozi inawapasa wazisimamie pia wawe mfano kwa kuzitii ili wananchi wote tuzifuate.
Basi ngoja niseme sipo kwenye 'mood' wa kuku'engage' kwa sasa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom