Benki ya CRDB kuwazawadia Sh. Milioni 15.4 ya Ada ya Shule wateja kupitia Akaunti ya Junior Jumbo

Blasio Kachuchu

Senior Member
Sep 7, 2016
153
111



Kwa upande wake Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Buza, Mary Joshua alisema wazazi wengi wamekuwa wakipata changamoto katika kulipa ada za Watoto kutokana na wengi kutokuwa na utamaduni wa kuweka akiba kwa ajili ya watoto. Hali hiyo imepelekea watoto wengi kuchelewa kurudi shule kuendelea na masomo au kujiunga na shule kwa wanafunzi wapya kutokana na kukosa mahitaji ya msingi ikiwamo ada.

“Tuna wahimiza wazazi/ walezi kuwafungulia watoto akaunti ya Junior Jumbo na kuanza kuweka akiba kwa ajili ya watoto kidogo kidogo. Akaunti hii inafunguliwa kwa vigezo nafuu sana, haina makato yoyote na hutoa faida ya riba kwa mteja,” amesema Bi. Mary Joshua huku akisisitiza kuwa Benki ya CRDB imejipanga kutoa elimu kwa wazazi ili kuwasaidia kuishi ndoto za watoto wao kwa kuwawezesha kupata elimu bora.

Meneja huyo alitoa rai pia kwa wazazi kutumia elimu inayotolewa na Benki ya CRDB kuwawekea akiba watoto wao kwani itasaidia sana kuweka msingi bora katika elimu. “Huu ni msimu wa sikukuu wengi wetu huwa tunafanya matumizi bila ya kujali January tunatakiwa kulipa ada pamoja na gharama nyengine za shule za watoto. Tunawahimiza kuweka akiba kwa ajili ya watoto kupitia akaunti ya Junior Jumbo,” aliongezea.
 
Back
Top Bottom