Masokotz
JF-Expert Member
- Nov 26, 2018
- 3,495
- 5,531
Nimepokea kwa masikitiko sana taarifa za kifo cha Rais Mstaafu wa Awamu ya tatu Ndugu Benjamin Mkapa. Kifo chake kimegusa moyo wangu na ninaamini kabisa kwamba kimegusa mioyo ya wengi sana.
Binafsi nimemfahamu Marehemu Mzee Mkapa kwa muda mfupi sana na katika kipindi kifupi nilichomfahmu amenijenga sana hasa katika misingi ya uongozi, maendeleo na ujenzi wa jamii. Mzee Mkapa katika uhai wake amekuwa ni mtu aliyeishi kwa kusema, kufanya na kusimamia kile alicho amini kwa maslahi mapana ya nchi.
Mbobezi huyu wa Diplomasia na siasa za Utandawazi ni mmoja wa waasisi wa Mabadiliko mengi sana katika Taifa letu. Amejijenge heshima nchini na nje ya dunia kutokana na umahiri wake wa kutetea kile alicho amini na kukisimamia.
Mzee Mkapa alikuwa ni mtu wa misimamo lakini mwenye kiwango kikubwa cha unyenyekevu. Hakuogopa kuonekana mbaya hasa pale ambapo aliamini kwamba kile alichosimamia ni sahihi na ni kwa maslahi mapana ya nchi. Alikuwa na ujasiri wa kukemea na kushauri pale inapobidi.
Mzee Mkapa ni Muasisi wa Tanzania mpya ambayo bado inajengwa. Alisimamia mageuzi makubwa sana katika uchumi wetu ikiwamo sekta ya fedha, uchumi na uwekezaji. Aliasisi sera ya ubinafsishaji na kuisimamia kwa udhabiti kwa kadiri ya uwezo wake. Alikuwa ni muumini wa Utandawazi na aliheshimika duniani kwa misimamo na mitazamo yake.
Mzee Mkapa ameendelea kuwa mshauri na mtetezi wa maslahi mapana ya nchi yetu na kwa hakika aliishi maisha ya mfano kwa uzalendo na utumishi.
PUMZIKA KWA AMANI MZEE WETU BEN MKAPA
Binafsi nimemfahamu Marehemu Mzee Mkapa kwa muda mfupi sana na katika kipindi kifupi nilichomfahmu amenijenga sana hasa katika misingi ya uongozi, maendeleo na ujenzi wa jamii. Mzee Mkapa katika uhai wake amekuwa ni mtu aliyeishi kwa kusema, kufanya na kusimamia kile alicho amini kwa maslahi mapana ya nchi.
Mbobezi huyu wa Diplomasia na siasa za Utandawazi ni mmoja wa waasisi wa Mabadiliko mengi sana katika Taifa letu. Amejijenge heshima nchini na nje ya dunia kutokana na umahiri wake wa kutetea kile alicho amini na kukisimamia.
Mzee Mkapa alikuwa ni mtu wa misimamo lakini mwenye kiwango kikubwa cha unyenyekevu. Hakuogopa kuonekana mbaya hasa pale ambapo aliamini kwamba kile alichosimamia ni sahihi na ni kwa maslahi mapana ya nchi. Alikuwa na ujasiri wa kukemea na kushauri pale inapobidi.
Mzee Mkapa ni Muasisi wa Tanzania mpya ambayo bado inajengwa. Alisimamia mageuzi makubwa sana katika uchumi wetu ikiwamo sekta ya fedha, uchumi na uwekezaji. Aliasisi sera ya ubinafsishaji na kuisimamia kwa udhabiti kwa kadiri ya uwezo wake. Alikuwa ni muumini wa Utandawazi na aliheshimika duniani kwa misimamo na mitazamo yake.
Mzee Mkapa ameendelea kuwa mshauri na mtetezi wa maslahi mapana ya nchi yetu na kwa hakika aliishi maisha ya mfano kwa uzalendo na utumishi.
PUMZIKA KWA AMANI MZEE WETU BEN MKAPA