Bendera ya- Tanzania Kupeperushwa nusu mlingoti

Tangu jana kuna habari inanitatiza kwamba Tanzania yamlilia Gaddafi, nashindwa kuelewa hivi huyu Membe akitoa ya moyoni mwake kuhusu kifo cha Gaddafi anawakilisha watanzania wote? Hivi huyo Gaddafi ametusaidia nini watanzania mpaka tumlilie. Huyu Membe na viongozi waseme wao ndio wanamlialia. Mbona hao walibya zaidi ya Elfu 50, walio uliwa kwa amri yake sio binadamu, na wale watanzania walio uliwa na wanajeshi wa Gaddafi pale Kagera akimsaidia Dictator mwenzake Idd Amini vipi au viongozi wetu wamesahau au hawakujua wala kusikia. Jamani viongozi wetu waache unafiki.

Huyu Membe naye tayari ameshakuwa Gamba,achilia mbali Joka la Mdimu
 
Mwafrika yeyote anayesherehekea kifo cha Gaddafi atakuwa mwendawazimu.

Pole sana mkuu, Kitanda usichokilalia hujui kunguni wake. Huo ni msemo wa kiswahili uliojikamilisha kwa maana yake. Kwa hiyo wale walioko Libya wenye nchi yao waliokuwa wanashangilia ni wendawazimu? Wewe ndio mwenye uchungu zaidi na Libya kuliko wao? Wewe ndiye unyeyajua mazuri ya Gaddafi kuliko Walibya wenyewe. Ninyi ndio wale mliokuwa mnatuaminisha kwamba Igunga is half London, imeendelea sana!! Ndio mnaosema Libya chini ya Gaddafi hakuna umaskini!!! Crap. Fanyeni utafiti kabla
 
Ndo maana watu hawaheshimu bendera ya Taifa. Enzi zetu ulikuwa unapiata penye bendera ukasikia filimbi unasimama wima hadi ipandishwe au ishushwe. Sasa kama mambo ni kama haya (kama ni kweli) bendera ni useless sory to say
 
Kufuatia kifo cha Dictator Gaddafi serikali kupitia Waziri Membe itapeperusha bendera ya nchi nusu mlingoti. Hili jambo linanichanganya kidogo, ni kwa heshima gani aliyostahili Gaddafi kupewa hadi bendera ipepee nusu milngoti? Dunia nzima inajua kwamba Gaddafi alikuwa Dictator amehusika na mauaji ya watu kama siyo halaiki tena kwa kiburi tu.

Gaddafi huyo huyo alishirikiana na Dictator wa Uganda Amini kuvamia nchi yetu na Watanzania wengi waliuawa, sasa hapa kuna umuhimu gani wa serikali ya Tanzania kupeperusha bendera nusu mlingoti? Mbona wakati IDD AMINI alipokufa Tanzania hatukupeperusha bendera nusu mlingoti?

Inamaana ile misaada yake ya kujenga Miskit ndiyo imetufanya tuchukue maamuzi hayo? Kwa maana nyingine ni kwamba hata IDD AMINI kabla hajafa angejenga shule au Kanisa hapa Tanzania, siku ya kifo chake ingepeperusha bendera nusu mlingoti?

Kama ni suala la IMANI lingeachiwa viongozi wa dini ndiyo waeleze msimamo wao kuhusu uzuri na ubaya wa Gaddafi.

Gaddafi huyo huyo alikuwa ni mshirika wa Gaidi OSAMA BIN Laden, inakuwaje tunawashangilia watu hatari kama hawa. Tunachokiona hapa siyo sera za nchi bali ni SIASA KWA AJILI ya 2015, sasa huu ndiyo ujinga wa serikali yetu.

Serikali kukataa kuwatambua waasi inamaana inafanya maandalizi kwenda Libya kuwafurusha serikali ya mpito ya Lbya. Tujiulize tena au tumuulize Waziri membe nini kauli yake kuhusu MAZISHI ya GADDAFI kufanyika BAHARINI kama ilivyokuwa kwa OSAMA BINLaden???

Watanzania tunaliona hili kuwa maombolezo hayo ni maalumu kwa MAFISADI na Wenyeuchu wa Madaraka ( Wachakachuaji na wezi wa KURA)na wala hayawakilishi Watanzania wenye nia njema.

hata kama alikuwa dictator hakustahili kifo kile.
 
JF siku izi unaweza kuleta story yoyote hakuna hata wa kuuliza "source please?" ?
si ndo hapo mkuu, yaani nimefungua kwa haraka huu uzi then nakutana na vitu havina hata source, na watu siku hizi wanachangia tu hata ukikuruopuka na kuandika kitu..!
Very sad indeed
 
kwa nini sisi tuwe na uchungu zaidi ya wa Libya ambao wengi wamekufa? Isitoshe yeye kaua ndugu zetu kule Kagera. Na kama kweli alipenda Uislamu na alijenga Misikiti Tanzania, je hakujua kuwa Kagera au jeshi la Tanzania lina waislamu? Na kwa nini vilevile awaue wa Libya ambao huenda ni ailimia 99 akija kuwa ni waislamu?
Yaani sisi wa Tanzania naona kama ni ulimbukeni, tunajali sana waarabu kuliko sisi wenyewe. Al Bashir kaua waafrika tena waislamu kule Darfur lakini hatujaandamana wala kulaani kitendo hicho, zaidi nafikiri ni inferiority yetu ya kudhani sisi waafrika tunahaki ya kufa kuliko ngozi tofauti na sisi. Sasa kufa kwa huyu mmoja ambae amdlta madhara mengi kuliko faida inatufanya tusononeke namna hiii!!!! mbona sifahamu kitu hapa???
Kama alikuwa ni kipenzi cha waafrika ni kwa nini alishabikia Nigeria igawanywe kuwa nchi mbili, ya Kikristo kusini na ya wa Islamu Kaskazini??? Sasa hiyo dream ingekuwaje?
Kuna kotesheni za Gadafi ningetaka kuziweka
Col Gaddafi on Africa


2007: "Libya is an African country. May Allah help the Arabs and keep them away from us. We don't want anything to do with them."

2009: "I am an international leader, the dean of the Arab rulers, the king of kings of Africa and the imam of Muslims, and my international status does not allow me to descend to a lower level," at an Arab League summit.
 
Kwa hiyo mtu ukisoma history tu ndio tiketi ya kukubali kilakitu?

mchango wa qaddafi kwa africa ni mkubwa sana .. amgalia investments alizofanya kusini mwa jangwa la sahara! .. naona watu wanarukia msikiti tu ! ... i hate to say this word but msifikiri kwa kutumia masaburi.. qaddafi was man enough kutetea rasili mali za africa kwa ujumla! kila mtu ana uzuri wake na ubaya wake aliyoufanyia africa kwa ujumla ni mengi
 
Great thinkers mmeacha kujadili hoja za maana mnakuwa kama akina Ritz na FFoxy ? Who is /was Gadaffi kwa Tanzania ? Mtanzania wa sasa ana shida kubwa sana anaweza kupoteza muda na kuawa kwa Gaddafi? Membe ni kiwewe kimemshika msaada wa pesa hakuna na labda kuona nguvu ya Umma imeshinda matamshi yake ya kijinga ya pickup .Atapatapa mwacheni .
 
I dont get it, it means Gaddafi's earlier crimes against humanity have been forgiven? If we want to have better Tanzania we must analyze things critically before we announce anything.
 
Hizo Dola za Ghadaffi zitawatoa Macho; alikuwa anawaibia wananchi wake kuwapa waafrika sasa nusu mlingoti itakuwa ni kujidhalilsha angalia huo ubalozi wa Libya hapo Dar hawata weka nusu mlingoti

Yaani Nyerere angekuwa hai sijui angesemaje
 
Huyu membe aache kujishauwa na mauaji ya Kadafi nilitegemea atakuomalia mauaji ya ndugu zetu Albino ati Kadafi kauliwa kikatili wewe Gamba tu na hata hapo huyo Rais wako ipo siku atakuwa kama Kadafi.Lakini hata hivyo simshangai Membe kwa kuwa huenda kapewa vijidola wakati aakienda huko Libya thus why anamlilia kwa kuwa hatapata tena viji euro,huna issue wewe na serikali yako ya Magamba
 
Acheni umbumbumbu nyie....gadafi ni shujaa..gadafi ni dume dunia inajua na kila mtu anajua....fatilieni mambo na historia ya dunia.someni historia na misimamo ya kanal muamar al gadafi.
 
Sina uhakika kama habari hiyo ni ya kweli,lakini sitashangaa kama serikali yetu itafanya hivyo ingawa itakuwa sawa na kukumbuka shuka wakati kumekucha! Ukifuatilia historia utagundua gaddafi alikuwa ni kiongozi jasiri na shupavu. Ni misimamo yake imara ndio iliyomponza. Waafrika tunatumika sana na nchi za magharibi na Marekani. Tu wanafiki na tunakubali kuzisaliti nchi zetu kwa gharama ndogo sana. Tusipokuwa makini tutarudishwa tena zama za ukoloni.
 
Hongera Membe na serikali kwa ujumla. Gadaf alikuwa ni mmoja wa viongozi imara sana Afrika, wanaongozwa na misimamo yao imara, si wale wafata upepo.

Afrika nzima inapaswa kumlilia Gadaf, mungu ailaze mahali peponi.
nimekubali alikuwa kiongoz shupavu
lkn nakataa bendera yetu kuwa nusu mlingoti kwa sababu ya kifo chake cha kujitakia.
 
Back
Top Bottom