Bendera ya- Tanzania Kupeperushwa nusu mlingoti

Hii habari haina ukweli. Mtoa mada nahisi kakurupuka. Wangempa msaada wa kijeshi ili asife. Ni ujinga mtupu wa hawa jamaa zetu akina membe.
 
Tuambieni kama bendera ya Libya nayo imeshushwa nusu mlingoti, kama sivyo ina maana tz inamheshimu na kumpenda zaidi gadaffi kuliko waloibya wenyewe? Halafu nimegundua magamba wote ndo wanaomsujudu huyu jamaa, kisa eti alitaka kuanzisha umoja wa afrika. Wanataka afrika iwe noja wakati tanganyika na z'bar tu ni mgogolo.
 
Hivi Ofisi za ubalozi wa Libya nchini nao wamepeperusha bendera nusu mlingoti? itakuwa ni AIBU na FEDHEHA kubwa sana kwetu kama wenye nchi waliofikwa na msiba bendera zao zipo juu kabisa na akina Membe wanahubiri ndivyo sivyo.

Well, huyo ni Membe bana. Kuna mbunge mmoja aliwahi kusema ndani ya bunge kwamba huyu bwana ni ''Joka la Kibisa'' (?)
 
Kama wanahamu ya kushusha bendera nusu mlingoti si washushe ya CCM? Wakishusha ya ccm wala hakuna atakae uliza maswali.
Kama wataona hiyo bendera ya ccm pekee ikipeperushwa nusu mlingoti haitoshi, washushe na ya Bakwata (kama wanayo) maana huyu jamaa mchango wake mkubwa katika nchi hii ni ujenzi wa misikiti.
 
kama gaddaf alitaka kuunganisha africa nini kimeharibika?si kikwete yupo na wanasema anaheshimika kimataifa?basi aunde huo umoja wa africa kama kweli rais wenu ana nguvu ya hoja.mia
 
Mi nafikiri huyu Marehemu anamuhusu Membe kibinafsi zaidi kuliko Tanzania kama nchi,
Kuna mambo waliahidiana wenyewe so mipango imevurugika ndio Joka la Mdimu amehuzunika.
Sasa Joka la Mdimu asitake kuingiza personal interest zake katika masuala ya kitaifa
 
Kufuatia kifo cha Dictator Gaddafi serikali kupitia Waziri Membe itapeperusha bendera ya nchi nusu mlingoti. Hili jambo linanichanganya kidogo, ni kwa heshima gani aliyostahili Gaddafi kupewa hadi bendera ipepee nusu milngoti? Dunia nzima inajua kwamba Gaddafi alikuwa Dictator amehusika na mauaji ya watu kama siyo halaiki tena kwa kiburi tu.

Gaddafi huyo huyo alishirikiana na Dictator wa Uganda Amini kuvamia nchi yetu na Watanzania wengi waliuawa, sasa hapa kuna umuhimu gani wa serikali ya Tanzania kupeperusha bendera nusu mlingoti? Mbona wakati IDD AMINI alipokufa Tanzania hatukupeperusha bendera nusu mlingoti?

Inamaana ile misaada yake ya kujenga Miskit ndiyo imetufanya tuchukue maamuzi hayo? Kwa maana nyingine ni kwamba hata IDD AMINI kabla hajafa angejenga shule au Kanisa hapa Tanzania, siku ya kifo chake ingepeperusha bendera nusu mlingoti?

Kama ni suala la IMANI lingeachiwa viongozi wa dini ndiyo waeleze msimamo wao kuhusu uzuri na ubaya wa Gaddafi.

Gaddafi huyo huyo alikuwa ni mshirika wa Gaidi OSAMA BIN Laden, inakuwaje tunawashangilia watu hatari kama hawa. Tunachokiona hapa siyo sera za nchi bali ni SIASA KWA AJILI ya 2015, sasa huu ndiyo ujinga wa serikali yetu.

Serikali kukataa kuwatambua waasi inamaana inafanya maandalizi kwenda Libya kuwafurusha serikali ya mpito ya Lbya. Tujiulize tena au tumuulize Waziri membe nini kauli yake kuhusu MAZISHI ya GADDAFI kufanyika BAHARINI kama ilivyokuwa kwa OSAMA BINLaden???

Watanzania tunaliona hili kuwa maombolezo hayo ni maalumu kwa MAFISADI na Wenyeuchu wa Madaraka ( Wachakachuaji na wezi wa KURA)na wala hayawakilishi Watanzania wenye nia njema.
Mirembe panakufaa sana tu.
 
Wengi hatumui Gaddafi na wengi inaelekea wameanza kumsikia wakat huu wa vita wakilishwa sumu na mataifa ya magharibi, somen historia vizuri na kuna siri hamuijui kuhusu serikali, kaen kimya na achen wamlilie
 
Hivi Ofisi za ubalozi wa Libya nchini nao wamepeperusha bendera nusu mlingoti? itakuwa ni AIBU na FEDHEHA kubwa sana kwetu kama wenye nchi waliofikwa na msiba bendera zao zipo juu kabisa na akina Membe wanahubiri ndivyo sivyo.

Well, huyo ni Membe bana. Kuna mbunge mmoja aliwahi kusema ndani ya bunge kwamba huyu bwana ni ''Joka la Kibisa'' (?)
mkuu wewe huwezi kufikiria hata kidogo? waasi wachache wakisaidiwa na mabeberu ndo wenye amri na ndo waliomuua Gaddafi sasa wewe unafikiri raia wa libya wanaujanja hapo? wamebaki kuumia kimoyomoyo tu. Kiukweli Mawazo ya Membe yamewakilisha mawazo ya wanyonge wa Libya ambao ni wengi. Hongera Membe kwa hilo.
 
Kama wanahamu ya kushusha bendera nusu mlingoti si washushe ya CCM? Wakishusha ya ccm wala hakuna atakae uliza maswali.

Maana kupeperusha bendera ya taifa nusu mlingoti ni UCHURO atakufa kiongozi wa juu kabisa hapa njini ili muenjoy hizo 1/2 mlingoti. Tunajikomba kuwa na majonzi kuliko walibya wenyewe!
 
Kufuatia kifo cha Dictator Gaddafi serikali kupitia Waziri Membe itapeperusha bendera ya nchi nusu mlingoti. .

Mkuu, sina uhakika kama kweli waziri Membe kayasema hayo, lakini kama ni kweli basi ni aibu. Ni aibu kwa sababu dunia nzima inajua kwamba Gadafi alikuwa dictator. Alitawala kwa mkono wa chuma. Hakuruhusu watu wenye mawazo tofauti na ya kwake. Aidha jana asabuhi pia nilimsikia waziri Membe akisema ati Watanzania hatuna kawaida ya kushangilia kifo cha mtu!!???. Nikajiuliza anasema kufurahisha au ndiyo sera ya nchi? Kama ni kweli, je kipindi kile Tanzania tunapigana vita na Idd Amini wa Uganda, kama asingetoroka tungefanikiwa kumkamata na kumuua tusingesherehekea? Sikupata jawabu. Kama kawaida ya wa TZ, majibu rahisi kwa maswali magumu.
 
tanzania ni miongoni mwa nchi 17 zilizopinga NTC kutambuliwa na UN kwa hhiyo membe lazima asimamie msimamo wake.
 
Mwafrika yeyote anayesherehekea kifo cha Gaddafi atakuwa mwendawazimu.
 
Hakuna mtu anayefurahia kifo, hata kama aliyekufa ni adui yako ila waLibya wengi wanafurahia kifo cha Gadaffi. Kuna familia nyingi sasa hivi ni yatima kwa sababu ya marehemu Gaddafi na wana haki ya kusherehekea kifo chake.
 
Back
Top Bottom