Hapo ulipodai maza kashauriwa vibaya mie nakupinga. Kama hawezi kufanya maamuzi binafsi bila kujali ushauri aliopewa na washauri wake kwa maslahi ya Watanzania basi kuna tatizo kubwa sana.
Nchi kama haina pesa aanze kulala mbele na mishahara na marupurupu ya Wabunge vyote ni vikubwa sana. Kuna Wabunge haramu 19 kila mwezi wanalipwa malipo haramu ya mabilioni ambayo hawastahili.
Nimeona mlipuko wa ajabu wa mikutano ya watendaji wa serikali siku za hvi karibuni. Mikutano hii, inafanyika kwenye kumbi za kulipia, kinyume na miezi michache kadhaa iliyopita. Safari zimeongezeka kwa kasi.
Ninaona wafanyakazi wa Wizara ya fedha wanaiba mabilioni ya fedha, wakati huo huo serikali haina fedha.
Wabunge wanalipwa kama wageni waliotoka sayari Mars, na bado wanapiga debe waongezewe malipo.
Kama kweli serikali haina fedha, hizi za mambo haya zinatoka wapi? Mtu akifikiria kwamba tuna watoa maamuzi wabinafsi wasiofaa na wasiojali maslahi ya umma wala maumivu ya watu wengine atakufa anakosea? Hivi kweli serikali kama kweli inajali, inashindwaje kuongeza wigo wa walipa kodi, kwa kufufua makampuni ya serikali yenye uwezo wa kuongeza uwezo wanyonge ili walipe kodi nzuri kama Pride Africa, lilokuwa limezagaa kila kona watu wakipata huduma za fedha kwa shangwe, wakiboresha maisha na kulipa kodi? Ni kwlei kwamba hakuna mtu mwenye ubunifu na ufahamu wa njia za kuongeza mapato kwa serikali, badala yake wanaongeza bei za mafuta ili hao walala hoi wazidi kufa na familia zao?
Mama anaposhauriwa, ni lazima achukue shauri kama zilivyo hata kama ni dhahiri kuna harufu ya madhara na yeye ni mchumi?
Ninadhani anahitaji msaidizi wa uchambuzi. Vinginevyo, tunaweza kuenda vibaya kwa shauri zenye mrengo wa ubinafsi na kutokujali maisha ya wanyonge.