Hii topic mpaka hapa nilikuwa sijaelewa chochote angalau nimepata mwanga. Nina swali... hii spidi ya kukopa nje sana na kununua sana nje na kuuza nje rasilimali madini na twiga tuu inaipeleka wapi shilingi yetu?
Always ss tunauza sana RAW MATERIALS wakati tunanunua sana zile Final Product. Bei ya Malighafi iko chini ukilinganisha na bidhaa iliyokamilika, hivyo basi sisi tunaingiza kiasi kidogo cha pesa za kigeni kupitia bidhaa na tunatumia kiasi kikubwa sana cha pesa katika kununua final product.
Hapa itabidi tuamue ama tutumie sana vitu vyetu wenyewe local product ili kubalance manunuzi au Tuendelee na kukopa ili kupata fedha hizo za kigeni zaidi kupata bidhaa kutoka nje.
Kuhusu mikopo, kuna baadhi ya miradi ni bora ukope ili kufinance kuliko kutumia fedha za ndani, hapa tunaweza kutumia njia mbili, mikopo ya muda mrefu (riba kubwa) au tuingie ubia na mashirika ya ndani au nje ili kufinance miradi na tugawane mapato for some years. Hii njia ya pili inatumika sana Ulaya ili kuleta maendeleo kwa haraka. Mfano, daraja la kigamboni ni la ubia kati ya Serikali na NSSF.
USHAURI.
Lazima tutafute leseni au ubia na makampuni ya nje ili yaweke viwanda hapa kwetu ili kuzuia manunuzi makubwa ya nje. Mfano, tunaweza ingia ubia na SAMSUNG, SONNY, TOYOTA, MAZDA NK waweke viwanda vyao hapa ili tuwe hub ya Afrika mashariki na kati katika bidhaa hizo nk.
Hatua hii inahitaji zaidi uthubutu na hali ya uhakika katika Sera, mipango, usalama, miundombinu nk katika kufanikisha hili.
Huwezi kuendelea bila kuwa na viwanda vikubwa au malighafi yenye uhitaji zaidi duniani.
Ikumbukwe madini sio bidhaa muhimu kwa mwanadamu hivyo sio ya kutegemea saaaana, labda SHABA ambayo hutumia sehemu nyingi zaidi.