Bei za mafuta Afrika Kusini (SA) zashuka

Bei za mafuta Afrika Kusini (SA) zashuka

SNAP J

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2013
Posts
7,117
Reaction score
8,096
Wakati watanzania bado tukilia na bei mpya za mafuta zilizoanza kutumika rasmi kuanzia Agosti 3 2022, nchini South Africa mambo ni tofauti kabisa.

Wizara ya madini na nishati nchini humo imetangaza auheni ya bei mpya za mafuta ambayo zimeanza kutumika rasmi tarehe 3 Agosti.(petroli na diseli ndio zimeshuka:tizama jedwali chini[emoji116]).

Wizara hiyo imezitaja sababu kuu za kushuka kwa gharama ya bidhaa hiyo nchini humo kuwa ni:

Sababu kuu zinazochangia kushuka kwa bei ya mafuta nchini SA ni:

1). Mahitaji madogo ya mafuta ghafi (crude oil) kwa sababu ya wasiwasi wa mdororo wa kiuchumi,

2). Bei za mafuta South Africa (SA) zashuka,

3). Kuibuka tena kwa Uviko-19 (COVID-19) nchini Uchina,

4). Uamuzi wa nchi wanachama wa OPEC (jumuiya la Nchi Zinazouza Petroli duniani) na nchi Wanachama Wasiokuwa wa OPEC kuongeza uzalishaji wa mafuta.

Hali kadhalika, wizara imesema bei ya mafuta SA ingeweza kushuka ziadi endapo kama kusingekuwa na vikwazo vya usafirshaji wa mafuta.

Endeleeni kudanganywa kuwa anaupiga mwingi.

IMG_20220803_211322.jpeg
 
Mbona hizo bei hazina tofauti ni Tanzania? Au wewe kwakuwa umeambiwa zimepungua ndio umekurupuka tu??

Exchange rate ni RAND 1= 139.22 TZS
 
Kwahiyo unafananisha rand 25 ya south na 3500 ya bongo,? Unajua rand 25 SA inanunua nini na 3500 bongo unafanyia nini? Pathetic Fool!!
Exactly mkuu kuna mazuzu humu yaani mpaka unakereka,sisi politicians wetu walitumezesha vitu gani, all countries around us ,bei zimekwenda chini only us, na bado kuna mazuzu humu wanaona ni sawa, na wanapiga kelele why Mr.Mbowe hawatetei!!,it's craze kutegemea wengine wakupiganie wewe umejificha na ID fake humu.
 
Siku zijazo hili jukwaa kuwe na qualifications za uanachama wallahi nchi hii watu Mazezeta na vibwengo kabisa Ujumbe upo very clear, Nchi hii Kwa Sasa ni aibu tupu serikali haipo stable period.
 
Back
Top Bottom