Bei ya trekta ya kulimia. Iwe mpya au mtumba

Bei ya trekta ya kulimia. Iwe mpya au mtumba

Donkey

JF-Expert Member
Joined
Dec 17, 2010
Posts
1,499
Reaction score
1,585
Wapi nitapata trekta ya kulimia iwe mtumba au mpya kwa bei nafuu. Pia, naomba ushauri ni aina gani ni bora
 
mkuu tractor ni nzuri karib zote sema ka unapiga kilimo kikubwa usiguse matractor ya kihindi au mpakistani, mengine wee okota na kapigie kazi tuu, mie najua yaliyo mengi bongo ni massey furguson na john deer ila yote yapo vizuri , ubungo karibu na darajani kuna jaamaa anauza used, ilala sokoni pale kuna yard jamaa anauza, so sehemu ni nyingi pia leo nimetoka ongea na mtu anauz alake MF 255
 
Halafu update MF 385 acha tu Aiseee lazima unuke pesa!!! Nashangaa DSM MTU ana Massey anazolea taka!??
haha haaa hesabu 50,000/= ila wakati mwingine sishangai maana najua management huko porin ni tabu ukizingatia wengi wamiliki wanataka kukaa mjini
 
Ngoja nifafanue kidogo kuhusu Tractor kati ya Masey,Ford na john deer..
Masey ni tractor nzuri ila kwa baadhi ya namba 135,165,270,290 na 375 hizi spare zake zipo za kumwaga na kwa series inayoendelea hapo spare zake mpaka kuagiza na pia hizi masey sio kwa ajili ya kulimia ardhi ngumu kama ya Ruvu au Dodoma kuna maeneo yenye ardhi ngumu ambayo inahitaji Ford series kuanzia 500 mpaka 600 au John Deer kubwa kwa uimara wa Ford ndio maana unaona hata Mafinga wanatumia kuvutia magogo mazito na kwa muda mrefu sio MF..
Kwa kulimia MF spare zake za kumwaga na bei ipo chini sio kama Ford au John deer...
 
165 kwenye mashamba ya mpunga Mbalali inaweza kweli mkuu na ni 2WD?
2WD itakwama kila mara kwenye tope huko inayotakiwa na hasa maeneo ya mashamba ya mpunga ni New Holland hili ni tractor bora sana linaweza kulima kwa Massa mengi kuliko matrector mengine shida linauzwa bei hata lililotumika kuliko brand zingine...Sema upate lenyewe maana kopi zake kutoka Pakistan na kwingineko yapo sasa hivi...
 
Ngoja nifafanue kidogo kuhusu Tractor kati ya Masey,Ford na john deer..
Masey ni tractor nzuri ila kwa baadhi ya namba 135,165,270,290 na 375 hizi spare zake zipo za kumwaga na kwa series inayoendelea hapo spare zake mpaka kuagiza na pia hizi masey sio kwa ajili ya kulimia ardhi ngumu kama ya Ruvu au Dodoma kuna maeneo yenye ardhi ngumu ambayo inahitaji Ford series kuanzia 500 mpaka 600 au John Deer kubwa kwa uimara wa Ford ndio maana unaona hata Mafinga wanatumia kuvutia magogo mazito na kwa muda mrefu sio MF..
Kwa kulimia MF spare zake za kumwaga na bei ipo chini sio kama Ford au John deer...
mkuu naunga mkono, ila ford spare part zake ni kichaa japo ile trekta imetengenezwaaa
 
Mkuu kwa tunaojua siri ya Massey Ferguson itamfaaa sana,hasa 165
mkuu hiyo wengine waiita mbuni ka ni mashamba makubwa au anapata tenda kubwa hua inakufa mapema injini alafu haitengenezeki ikatukia, labda ubadilishe injini uweke nyingine labda ya 185, 178, au 290 n.k ukifanyahivyo utakuwa umemaliza tabu yake
 
2WD itakwama kila mara kwenye tope huko inayotakiwa na hasa maeneo ya mashamba ya mpunga ni New Holland hili ni tractor bora sana linaweza kulima kwa Massa mengi kuliko matrector mengine shida linauzwa bei hata lililotumika kuliko brand zingine...Sema upate lenyewe maana kopi zake kutoka Pakistan na kwingineko yapo sasa hivi...
mkuu 2WD kwenye mashamba ya mpunga ni tabu. ila kwa bei za kawaida unaweza pata 4WD massey furguson kama MF290 na series nyingine ambazo kwa mtu mmoja mmoja zinanunulika, hayo ma new holland mtu wa kipato cha kawaida hawezi nunua
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom