Beating the Drum on One Side: Confusing the People on Both Sides

Beating the Drum on One Side: Confusing the People on Both Sides

Nadhani hapo kwenye bold pekee palitosha Mohamed Said kuto jibu hoja kutoka matini chanzi. Kwa sababu sikumbuki kama amewahi kutoa utafiti unaohusu hapo penye bold ambapo hapatuhusu. Mimi nakuomba unisaidie kujibu hoja ya 71waislamu+29wakristo=100.
Soma hii bayana unatukana na neno MAU MAU.

Na Mohamed SaidKwa mara ya kwanza Tanzania ilishuhudia kuandikwa kwa historia ya mmoja wa viongozi wakuu wake kupitia kitabu Simba wa Vita Katika Historia ya Tanzania Rashidi Mfaume Kawawa kilichoandikwa na Dk. John M. J. Magotti. Sidhani kama katika historia ya Tanzania kuna kumbukumbu ya kuandikwa kwa kitabu kinachohusu maisha ya kingozi yoyote achilia mbali kufanyika kwa sherehe ya kukizindua kitabu hicho Ikulu ikiongozwa na rais mwenyewe. Kwa hakika sherehe ilifana sana na tukakisubiri kwa hamu kitabu madukani ili tupate kunufaika na kumbukumbu za Mzee Kawawa.Msomaji anaweza kukisoma kitabu chote chenye kurasa 127 kwa muda wa saa moja akawa kakimaliza chote na atakapokiweka chini akawa hakubakia na chochote cha maana katika fikra yake.

Kwa nini iwe msomaji asibaki na kumbukumbu yoyote ya kiongozi mkubwa kama Mzee Kawawa mtu aliyeshuhudia kwa macho yake mwenyewe harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika na si hivyo tu yeye mwenyewe ni mmoja wa wale waliopigania uhuru wa Tanganyika na kushika nyadhifa kubwa za uongozi chini ya Mwalimu Julius Nyerere. Kwa kawaida vitabu vya maisha ya viongozi hasa wapigania uhuru huwa vina mambo mengi sana ambayo kwa muda mrefu huwa siri, hayafahamiki hadi hapo kitabu kitakapoandikwa ama kwa mkono wake kiongozi mwenyewe au kuandikwa na muandishi. Mifano ipo mingi.

Kitabu kama Mahatma Gandhi klichoandikwa na Robert Payne au Long Walk to Freedom alichoandika Nelson Mandela mwenyewe au Seeds of Freedom alichoandika Bildad Kaggia hakika unapomaliza kusoma vitabu hivi lazima urudi nyuma kufungua kurasa hapa na pale kuzisoma upya zile sehemu zinasosisimua.Huwezi kupata haya katika kitabu cha Mzee Kawawa. Huwezi kuyapata haya kwa kuwa mwandishi hakuandika kitu. Hakuandika kitu si kama Mzee Kawawa hana historia ya kusisimua na kuwa hana mengi ambayo wengi hawayajui katika maisha yake, nadhani mwandishi hakuwezakuja na jipya labda kwa sababu hakufanya utafiti wa kutosha kuweza kuandika kitabu kinachomuhusu simba wa vita aneunguruma. Kuna msemo wa Kiswahili usemao Aungurumapo simba mcheza ni nani? Kwa hakika simba wa vita hakuunguruma kabisa katika kitabu hiki. Sijui lawama zielekezwe wapi.Mimi simjui Mzee Rashidi Kawawa kwa kiwango cha kusema naweza kunyanyua kalamu na kufanya pitio la kitabu kilichoandikwa kuhusu yeye.

Nathubutu kuandika kuhusu kitabu chake kutokana na kumjua kwangu mimi nikiwa kama mwandishi na mtafiti ambae katika kutafiti kwangu nimekutana na jina la Mzee Kawawa hapa na pale katika nyaraka zilizo katika hifadhi ya ukoo wa akina Sykes. Nitatumia uzoefu wangu huu kueleza yale niliyoyaona katika nyaraka hizi na ninayojua kuhusu Mzee Kawawa na kufanya tathmini kwa yale niliyoyasoma katika kitabu cha Magotti.Miaka kama ishirini iliyopita nikiwa kijana mdogo nilipata hamu ya kuandika historia ya kudai uhuru wa Tanganyika. Sikuona mtu wa kumuendea isipokuwa Ally Sykes. Nilipomueleza kuwa nia yangu ni kuandika kitabu kuhusu marehemu kaka yake Abdulwahid Sykes (1924- 1968) Ally Sykes alinambia kuwa atanipa nyaraka zake zote nizipitie kisha ndiyo nakaenae chini kwa mahojiano ya ana kwa ana. Katika nyaraka alizonikabidhi ndani yake nilikuta barua ya mkono aliyoandika Rashid Kawawa mwaka 1952 kutoka Bukoba akimletea Ally Sykes aliekuwa Dar es Salaam. Barua hii ya Mzee Kawawa kwa Ally Sykes ilikuwa ikimfahamisha Ally Sykes hali ya siasa Kanda ya Ziwa.

Hii barua hadi leo ipo katika nyaraka za akina Sykes. Nilipokaa na Ally Sykes kutaka maelezo ya barua ile aliyoandikiwa na Kawawa, Ally Sykes alinipa kisa hiki:Mwaka 1951 nilichaguliwa kuwa katibu mkuu wa Tanganyika African Government Servants Association (TAGSA). Chama hiki kiliundwa mwaka wa 1927 kwa lengo la kuendeleza maelewano mazuri baina ya serikali ya Malkia na sisi watumishi Waafrika. Rashid Kawawa alikuwa mwana kamati. Mimi nilichaguliwa pamoja na Thomas Marealle kama rais wa TAGSA. Katiba ya TAGSA iliamuru uchaguzi wa kila mwaka, na mimin nilirudishwa madarakani kama katibu mara nne hadi Oktoba, 1954 nilipojiuzulu baada ya kuhamishwa kwenda Korogwe kama adhabu kwa kuwa miongoni mwa wale wanachama 17 waliounda TANU. Watu kadhaa walishika urais. Stephen Mhando na Dr Wilbard Mwanjisi wote hao waliwahi kuchaguliwa kuwa marais wa TAGSA.

Miongoni mwa wanachama watendaji wa TAGSA walikuwa Dr Michael Lugazia na Rashid Kawawa ambao alichaguliwa kuwa katibu baada ya mimi kujiuzulu. Kupitia TAGSA, Kawawa alichaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa Tanganyika Federation of Labour (TFL).Ujumbe wa Umoja wa Mataifa ulipokuja kuzuru Tanganyika Agosti, 1951 kwa mara ya tatu, vyama vyote viwili, TAA na TAGSA, viliwakilisha malalamiko kwa ujumbe huo. TAGSA iliwakilisha malalamiko yake kuhusu ubaguzi katika utumishi serikalini kwa mujibu wa kupanga mishahara kufuatana na rangi ya ngozi. Mshahara wa Mwafrika ulikuwa wa chini zaidi kuliko ule aliokuwa akipokea Mzungu au Muasia kwa kazi hiyo hiyo.

Kwa mfano Mwandishi wa hati mkato Mzungu alikuwa akipata mshahara mkubwa kuliko Mwafrika aliyekuwa na shahada au digrii kutoka chuo Kikuu cha Makerere. TAGSA vilevile tulilalamika kuhusu kuajiri makarani wa kutoka India na hali walikuwepo Waafrika kutoka Afrika ya Mashariki na Nyasaland ambao wangeweza kujaza nafasi hizo kwa urahisi.Vyama vyetu hivi viwili TAA na TAGSA viliwakilisha malalamiko haya tukifahamu fika kwamba Uingereza ilikuwa ikiitawala Tanganyika chini ya vifungu nambari 76 na 77 vya Umoja wa Mataifa ambavyo viliwekwa ili kuendeleza maendeleo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii ya nchi zilizokuwa chini ya udhamini. Kama mdhamini Uingereza ilitakiwa kuhimiza na kuheshimu haki za binadamu na uhuru wa kwa wote bila kubagua kwa misingi yajinsia, lugha au dini. Lakini Uingereza ilikuwa ikipuuza vifungu hivi bila aibu.

TAGSA tuliwakilisha malalamiko haya ili Umoja wa Mataifa ujue matatizo halisi ya ukoloni nchini Tanganyika.Mimi nikiwa katibu wa TAGSA nilifuatilia serikalini masuala yaliyoainishwa ndani ya malalamiko yetu. Suala lililokuwa likituhangaisha sana wakati ule ilikuwa uajiri wa Wahindi kutoka India, jambo ambalo niliieleza serikali halikuwa na faida, maadam kulikuwako na Waafrika ndani ya nchi ambao wangeweza kujaza nafasi zile. Jambo hili lilikuwa likisababisha manugíuniko makubwa miongoni mwa Waafrika.

Hakuna majibu maridhawa yaliyopatikana kutoka kwa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa. Barua tulizoandika serikalini juu ya masuala hayo zilipuzwa na Chief Secretary, Bruce Hutt. Katika kufuatilia malalamiko haya, Niliandika barua moja kali sana na kwa mara ya kwanza bila kutafuna maneno niliuliza uhalali wa Waingereza kututawala Waafrika wa Tanganyika. Nillimwambia Katibu Mkuu kuwa kwa kuwa serikali imeshindwa kupata ufumbuzi kwa matatizo ya Waafrika, Uingereza lazima ijitoe Tanganyikana Umoja wa Mataifa utawale Tanganyika. Barua hiyo ilimkasirisha Katibu Mkuu na siku chache baadaye nilipokea barua kutoka serikalini iliyokuwa imejaa vitisho, dharau, stihizai na makemeo. Nikajibiwa kuwa hakuwa na suala la Umoja wa Mataifa kutekeleza utawala wa moja kwa moja Tanganyika.Dkt Mwanjisi alikuwa amegusa suala nyeti sana kwa kuzungumzia matatizo ya ubaguzi wa rangi uliokuwa ukitukabili Waafrika wa . Kawawa, kama mjumbe wa kamati, akaniandikia barua akanitahadharisha nisichapishe ile hotuba ya Dkt Mwanjisi katika jarida la TAGSA bila idhini ya kamati ya utendaji. Kufuatia majibishano haya kati ya TAGSA na serikali, Dkt Mwanjisi kama alivyofanyiwa Dk Kyaruzi kabla yake, akahamishwa kutoka hospitali ya Sewa Haji mjini Dar es Salaam hadi Kingolwira Prison Hospital karibu na Morogoro. Kawawa na yeye akapewa uhamisho kwenda Bukoba na mimi nikapewa uhamisho kwenda Mtwara.


Dk Mwanjisi na Kawawa walikubali uhamisho wao na wakaondoka Dar es Salaam. Mimi nilikataa uhamisho na nikabakia Dar es Salaam kupinga uhamisho wangu.Alipokuwa Bukoba ndipo Kawawa akamwandikia Ally Sykes barua ile ya mwaka 1952 akimweleza hali ya siasa kama alivyoikuta Kanda ya Ziwa. Huyu ndiye Kawawa niliyemjua mimi kupitia nyaraka na mahojiano na Ally Sykes. Kwa kweli inasikitisha kuwa Dk Magotti hakupata fursa ya kuziangalia nyaraka hizi muhimu sana katika siyo historia ya Kawawa bali katika historia ya kuundwa kwa TANU na kudai uhuru wa Tanganyika. Endapo angepata nafasi ya kuziona hizi nyaraka zingempelekea katika kuwajua wazalendo wengine waliotajwa mle ndani kama Dk. Kyaruzi, Dk. Wilbard Mwanjisi ambao Kawawa alikuwanao katika harakati za TAGSA. Katika majina hayo angeweza kudodosa mengi kutoka kwa Mzee Kawawa na hivyo kuandika yale ambayo hayafahamiki kwa wengi. Hii imgekifanya kitabu kiwe cha maana.Mathalan Kawawa angeeleza mtafaruku kati ya Mwalimu Nyerere na Dk. Mwanjisi nini chanzo chake na nini ikajakuwa matokeo yake. Halikadhalika angempa fursa Mzee Kawawa kumuhadithia mchango wa Dk. Michael Lugazia katika kuasisi kwa TANU hasa kipindi kile cha 1953 wakati TAA ilipokuwa inatayarisha rasimu ya katiba ya TANU. Kwa ufupi ni kuwa Dk Lugazi alikuwa akijaribu kuamsha ari ya TAA Bukoba ari iliyokufa kutokana na kufungwa kwa kiongozi wa TAA Bukoba Ali Migeyo. Kisa cha Ali Migeyo ni moja ya visa vinavyosikitisha sana katika historia yaTanganyika kwani aliwekwa kizuizini na Mwalimu Nyerere kamaalivyofungwa na Waingereza. Haiwezekani kuwa Kawawa asiwe na habari na kile kilichopelekea mpigania uhuru hodari kama Ali Migeyo aishie jela tena wakati nchi ikiwa huru. Migeyo alifungwa na wakoloni kwa kuwahamasisha Watanganyika kudai uhuru labda Mzee Kawawa angeulizwa angeeleza ni nini kilitokea wakaamua kumfunga Migeyo kamawalivyomfunga Waingereza.

Kitabu kimegusia kazi alofanya Kawawa kama mtumishi wa serikali ya kikoloni katika kambi za raia wa Kenya walioshukukiwa kuwa ni Mau Mau. Katika hawa wafungwa walikuwawepo wananchama wa TANU ingawa hawa walikuwa Wakenya. Maarufu katika hawa alikuwa Dome Okochi Budohi (ambae kadi yake ya TANU ilikuwa na 6) na Patrick Aoko. Budohi alicheza senema pamoja na Kawawa iliyoitwa Wageni Wema. Kawawa na Budohi walikuwa wakifahamiana vizuri sana kwa sababu wote walikuwa wasanii. Budohi alikuwa mmojawapo katika bendi ya vijana wa mjini iliyojulikana kama Skylarks. Bendi hii baadaye ilibadilisha jina na kuitwa Blackbirds. Matangazo ya radio yalipoanza Tanganyika, Blackbirds midundo ya Blackbirds ilikuwa haikosekani kusikika radioni katika Sauti ya Dar es Salaam. Kawawa kama walivyo vijama wote wa Dar es Salaam wa wakati ule alikuwa mmmoja wa wapenzi wa bendi hii na alikuwa hakosekani Ukumbi wa Arnatouglo bendi hii ikitumbuiza katika ile miaka ya 1950. Ilikuwa katika ule upigaji muziki wa Budohi ndipo alipoungana na Kawawa katika kutengenezwa kwa senama hiyo ya Wageni Wema ambayo mwandishi kaitaja lakini aliishia hapo tu.Budohi na Aoko ni kati ya wafungwa wa0 "MAU MAU" waliokuwa Handeni ambako Kawawa alikuwa na jukumu la kuwaangalia. Budohi ndiyo alikuwa mtu wa kati baina ya TAA na KAU na kuanzia hali ya hatari ilipotangazwaKenya mwaka 1952 Budohi na Aoko wakawa katika jicho kali la makachero. Makachero hawa Waafrika wanafahamika na wengine walikuja kufanya kazi hiyohiyo katika Tanganyika huru. Hiki ndicho kipindi ambacho Kaimu Rais wa TAA na Katibu wa TAA Abdulwahid Sykes alipokutana na Kenyatta Nairobi. Wakati Wakenya hawa wanafungwa Tanganyika, viongozi wa KAU akina Bildad Kaggia, Jomo Kenyatta, Kungu Karumba, Achieng Oneko, Paul Ngei na Fred Kubai walikuwa wamekamatwa Kenya.

Kawawa ni mmoja kati ya viongozi hawa na ingependeza sana kama kupitia kwake tungeelezwa jinsi KAU na TAA ilivyokuwa ikishirikiana kwani haiwezekani kuwa Budohi na Kawawa uswahiba wao ukaishia kwenye kucheza senema tu.
 
Last edited by a moderator:
Mohamed Said
Sijui kama unaona jinsi mijadala ya kifikra inavyogeuga kuwa mijadala ya kashfa na matusi
Nilidhani ungeongoza katika kujibu hoja za Hirji ili tupate pande zote mbili za shilingi!

Kinyume chake tunaona picha na matusi.

Ningeshauri upitie hoja za Hirji ili kulitendea haki jamvi. Inavyoonekana nyuzi zinazokuhusu zinaambatana na matusi, sijui kama ungependa unasibishwe na hilo.

Umepata jibu kwanini wale uliosema 'wenzetu' wanakimbia jamvi? maana kuna tofauti kati ya jamvi na amvi! oops!

Ni ushauri tu
Nguruvi3.

Kama kuna matusi yeyote basi ni wajibu wetu kama wana JF kuwasaidia Mods kubonyeza kitufe cha abuse Mods wafanye kazi yao.
 
Last edited by a moderator:
nimekuuliza swali hujajibu nawe unauliza swali!

umenikumbusha swali langu kwako kule jukwaa la dini kuhusu "mtume Muhamad yuko ahera au jehanam" hadi kesho hutolijibu.

hapa napo nimekuuliza kuhusu utafiti wa Mohamed Said
1. Umefanyikia mikoa gani?

2. Sampling method ipi?

3. Sampling technique ipi?

4. Data analysis ilikuwaje?

5.How was Analysis of Variance done?

6. How was data interpreted?

HATUBADILI HISTORIA YA NCHI kwa utafiti wa Buguruni pekee na samples za misikitini pekee

Kasome post namba 314 nimekujibu na nimekuwekea reference zote zilizotumika kwenye tafiti ya Paper hii inayoongelewa hapa.

Hivi hizo Shule huwa mnaenda kusomea ujinga?
 
Mohamed Said
Sijui kama unaona jinsi mijadala ya kifikra inavyogeuga kuwa mijadala ya kashfa na matusi
Nilidhani ungeongoza katika kujibu hoja za Hirji ili tupate pande zote mbili za shilingi!

Kinyume chake tunaona picha na matusi.

Ningeshauri upitie hoja za Hirji ili kulitendea haki jamvi. Inavyoonekana nyuzi zinazokuhusu zinaambatana na matusi, sijui kama ungependa unasibishwe na hilo.

Umepata jibu kwanini wale uliosema 'wenzetu' wanakimbia jamvi? maana kuna tofauti kati ya jamvi na amvi! oops!

Ni ushauri tu

Prof Hirji ni msomi lakini ndugu yetu Mohd Said ni muislam mlalamikaji.hajibu hoja za prof ...anahitaji msaada na kwa bahati mbaya hakuna wa kumjibia
 
faiza foxy.

nakuelewa.

cjaona wa kukujibu.

Utashindwaje kumuelewa wakati unatumia prism ya udini, huyo kigagula faiza foxy na wewe mngemjibu Prof kwa hoja ingekua vizuri zaidi, na sio kutafuta makosa madogo ya herufi, Hisia za kijahidina zitawaua

Nipo pembeni nakunywa Mirinda Apple, nawasubiri
 
Last edited by a moderator:
Mzee Mohamed Said ina maana ktk chimbu-chimbua hujawahi pata habari za Dkt.Mwanjisi maisha yake baada ya uhuru na namna taa yake ilivyozimika ghafla ktk Tanganyika huru? Kama unazo habari zake kwa uchache nitupie nipate kumfahamu japo kwa uchache maana Wazee wako wa Gerezani taarifa zao walau nimetosheka nazo.
 
Last edited by a moderator:
Prof Hirji ni msomi lakini ndugu yetu Mohd Said ni muislam mlalamikaji.hajibu hoja za prof ...anahitaji msaada na kwa bahati mbaya hakuna wa kumjibia

Kuna majibu katowa Al Alama Mohamed Said lakini naona kama kawaida yenu, macho mnayo lakini hayaoni.
 
Last edited by a moderator:
Mzee Mohamed Said ina maana ktk chimbu-chimbua hujawahi pata habari za Dkt.Mwanjisi maisha yake baada ya uhuru na namna taa yake ilivyozimika ghafla ktk Tanganyika huru? Kama unazo habari zake kwa uchache nitupie nipate kumfahamu japo kwa uchache maana Wazee wako wa Gerezani taarifa zao walau nimetosheka nazo.

Kandukamo1,
Dr. Wilbard Mwanjisi...

Sijui kama ndugu yangu kweli hujui habari zake ama unataka mimi nilitibue
sega la nyuki.

Nikizileta hapa kuna watu watasema namchukia mtu fulani kwa hiyo nataka
nikilete kisa hiki hapa ili aonekane mbaya.

Nazijua sana habari za Dr. Mwanjisi.

Alikuwa pamoja na mzee wangu katika Tanganyika African Government Servant
Association (TAGSA).

Wote walikuwa viongozi na wanachama wa TAA.

Nimesoma hadi maandishi yake aliyokuwa akiandika 1950 dhidi ya ukoloni.

Mufti Sheikh Hassan bin Amir wakati mwingine alikuwa akiletewa maswali ya mtego
ili akijibu ichukuliwe kuwa ndiyo fatwa.

Alikuwa akishalijua kama hili ni swali la mtego alikuwa hajibu ila anamshauri muulizaji
afanye utafiti wake mwenyewe atapata jibu.
 
Mzee Mohamed Said ina maana ktk chimbu-chimbua hujawahi pata habari za Dkt.Mwanjisi maisha yake baada ya uhuru na namna taa yake ilivyozimika ghafla ktk Tanganyika huru? Kama unazo habari zake kwa uchache nitupie nipate kumfahamu japo kwa uchache maana Wazee wako wa Gerezani taarifa zao walau nimetosheka nazo.
Pata darsa kiduchu hapa chini.

Mwaka wa 1951 wakati Dossa na wenzake wapo katika juhudi za kuipa uhai mpya TAA Dossa aliandikiwa barua na V.M. Nazerali aliyekuwa mjumbe wa Baraza la Kutunga Sheria akimuomba Dossa aunge mkono juhudi zake na za Ivor Byaldon na Brig. Scupham za kutaka kuunda chama cha siasa kitachowashirikisha watu wa rangi zote. Bayldon na Brig. Scupham walikuwa kama alivyokuwa Nazerali, wajumbe wa Baraza la Kutunga Sheria.-Wanasiasa wengine walioombwa kuunga mkono juhudi hizi walikuwa Chifu Kidaha Makwaia, Liwali Yustino Mponda wa Newala, Dr. Joseph Mutahangarwa, Chifu Abdieli Shangali wa Machame, Chifu Thomas Marealle wa Marangu, Chifu Adam Sapi Mkwawa, Chifu Harun Msabila Lugusha, Dr. William Mwanjisi, Abdulkarim Karimjee, Dr. Vedas Kyaruzi, Liwali Juma Mwindadi, H.K.Viran, Stephen Mhando, Ally Sykes na Abdulwahid Sykes. Dossa na wenzake waliikataa ghilba hii kwa kuwa lengo lao lilikuwa ni kuanzisha chama cha siasa cha Waafrika wa Tanganyika kwa minajili ya kudai uhuru.-Mwalimu Nyerere alipofika Dar es Salaam kwa mara ya kwanza mwaka wa 1952 kama mwalimu wa shule ya St. Francis' College, Pugu hakuna mtu aliyekuwa anamjua au kupata kusikia habari zake katika ulingo wa siasa. Kassela Bantu ambaye alikuwa akijuana na Nyerere kwa siku nyingi alimchukua Nyerere kwa Abdulwahid Sykes kumtambulisha. Wakati ule Abdulwahid alikuwa Rais wa TAA. Nyerere mara moja akajiunga na baraza la siasa lililokuwa likifanyika Mtaa wa Mbaruku nyumbani kwa Dossa. Ikawa kila Jumapili Nyerere anakuja kutoka Pugu kuja kumtembelea Dossa. Ilikuwa katika baraza hii ndipo Nyerere alipokutana na wanasiasa wengi wa wakati ule kama Ramadhani Mashado Plantan aliyekuwa anamiliki gazeti lililokuwa likijulikana kama Zuhra, John Rupia, Dunstan Omari, Zuberi Mtemvu na wanasiasa wengine. Fikra za Nyerere za kudai uhuru zilisikika kwa mara ya kwanza kupitia kalamu ya Mashado Plantan na gazeti lake la Zuhra lililokuwa likitoka kila siku ya Ijumaa. Fikra za Nyerere ziliingiza msisimko mpya katika baraza lile na haukuchukua muda mwaka 1953 uongozi wa ndani ukampendekeza agombee urais wa TAA.
 
Last edited by a moderator:
Kandukamo1,
Dr. Wilbard Mwanjisi...

Sijui kama ndugu yangu kweli hujui habari zake ama unataka mimi nilitibue
sega la nyuki.

Nikizileta hapa kuna watu watasema namchukia mtu fulani kwa hiyo nataka
nikilete kisa hiki hapa ili aonekane mbaya.

Nazijua sana habari za Dr. Mwanjisi.

Alikuwa pamoja na mzee wangu katika Tanganyika African Government Servant
Association (TAGSA).

Wote walikuwa viongozi na wanachama wa TAA.

Nimesoma hadi maandishi yake aliyokuwa akiandika 1950 dhidi ya ukoloni.

Mufti Sheikh Hassan bin Amir wakati mwingine alikuwa akiletewa maswali ya mtego
ili akijibu ichukuliwe kuwa ndiyo fatwa.

Alikuwa akishalijua kama hili ni swali la mtego alikuwa hajibu ila anamshauri muulizaji
afanye utafiti wake mwenyewe atapata jibu.
Basi kama itakua tabu kwa wana ukumbi waweza kuyaacha au ukanitumia kwa PM.
 
Mohamed Said
Sijui kama unaona jinsi mijadala ya kifikra inavyogeuga kuwa mijadala ya kashfa na matusi
Nilidhani ungeongoza katika kujibu hoja za Hirji ili tupate pande zote mbili za shilingi!

Kinyume chake tunaona picha na matusi.

Ningeshauri upitie hoja za Hirji ili kulitendea haki jamvi. Inavyoonekana nyuzi zinazokuhusu zinaambatana na matusi, sijui kama ungependa unasibishwe na hilo.

Umepata jibu kwanini wale uliosema 'wenzetu' wanakimbia jamvi? maana kuna tofauti kati ya jamvi na amvi! oops!

Ni ushauri tu
Nguruvi3,
Nakuongezea picha nyingine.
Picha hii alinipiga Mzee Shebe mwaka wa 1952/53.

Mzee Shebe alikuwa na studio yake Mtaa wa Livingstone na Kipata.
Baadae Mzee Shebe akaja kuwa mpiga picha wa TANU na Nyerere
wakati wa kudai uhuru.

20140129_133419.jpg


Nguruvi3,
Kadri tunavyokwenda In Sha Allah ndivyo utazidi kunifahamu vyema.
 
Basi kama itakua tabu kwa wana ukumbi waweza kuyaacha au ukanitumia kwa PM.

Kandukamo1,
Subiri itafika wakati In Sha Allah tutamgumza Dr. Mwanjisi.
Nduguye Roland Mwanjisi ameandika "paper," kuhusu kaka yake.

"Paper," hii alimpelekea mzee wangu mmoja baada ya yeye Roland kusoma
kitabu cha Abdul Sykes.

In Sha Allah iko siku nitakuwekeeni hapa.

Sasa mnaanza kunishangaza mbona ghafla watu wanataka kujua historia hii?
Ilhali hapa hapa wako walioita historia hii ni ngano za Mohamed Said?

Nini kimezidi?
 
Utashindwaje kumuelewa wakati unatumia prism ya udini, huyo kigagula faiza foxy na wewe mngemjibu Prof kwa hoja ingekua vizuri zaidi, na sio kutafuta makosa madogo ya herufi, Hisia za kijahidina zitawaua

Nipo pembeni nakunywa Mirinda Apple, nawasubiri

Name calling si katika mambo yanayoruhusiwa JF.

Naona hujaisoma hii mada na umekurupuka, pitia vizuri. Nimei-knock-out hoja ya Professor Hirji in one post, na sijapata majibu ya kupinga hilo mpaka sasa hivi, na kila nimuulizae anakwepa, labda wewe pitia ujibu niliyouliza.

Lakini nikasema kwa faida ya watu kama wewe, ingawa criticism ya Hirji nime i knock out, tutaendelea kuwapa darsa mfaidike na ndicho kinachendelea lakini mapungufu yaliyopo kutoka kwa Hirji hayafai hata kujadiliwa. Tujadili "hypothetically...data..."?

Hebu wewe jibu ukweli, Mau Mau walipigana na Wajerumani?
 
Kandukamo1,
Subiri itafika wakati In Sha Allah tutamgumza Dr. Mwanjisi.
Nduguye Roland Mwanjisi ameandika "paper," kuhusu kaka yake.

"Paper," hii alimpelekea mzee wangu mmoja baada ya yeye Roland kusoma
kitabu cha Abdul Sykes.

In Sha Allah iko siku nitakuwekeeni hapa.

Sasa mnaanza kunishangaza mbona ghafla watu wanataka kujua historia hii?
Ilhali hapa hapa wako walioita historia hii ni ngano za Mohamed Said?

Nini kimezidi?


Hivi dhumuni lako hasa la kufunyua haya ni nini?
 
Kandukamo1,
Subiri itafika wakati In Sha Allah tutamgumza Dr. Mwanjisi.
Nduguye Roland Mwanjisi ameandika "paper," kuhusu kaka yake.

"Paper," hii alimpelekea mzee wangu mmoja baada ya yeye Roland kusoma
kitabu cha Abdul Sykes.

In Sha Allah iko siku nitakuwekeeni hapa.

Sasa mnaanza kunishangaza mbona ghafla watu wanataka kujua historia hii?
Ilhali hapa hapa wako walioita historia hii ni ngano za Mohamed Said?

Nini kimezidi?

Inashangaza si kidogo.

Tukiwaomba waje na historia waijuwayo wao nasi tufaidike na elimu yao hawaji nayo, mara wanakuomba kujuwa kuhusu fulani na hiki na kile tena kwa kejeli na tashtiti za hapa na pale, ingawa hawana walijualo.

Nnakumbuka walisema siku za nyuma wataunda kikundi chao hao wajiitao Yericko Nyerere, Mzee Mwanakijiji, Nguruvi3, Mag3 na wengineo ili waje na historia kupinga historia uliyoiandika wewe. Chakushangaza! naona mpaka leo umoja huo haujaja na chochote, sana sana niliona wakati fulani ajiitae Mzee Mwanakijiji akiokotea yale yale yako (plagiarism) na kuyatoa kwenye gazeti kama vile ni yake. Nikaona tena ajiitae Yericko Nyerere akiokotea yale yale yako (plagiarism) akileta humu humu JF kama vile yake.

Leo pumba za Professor Hirji waliona kama zimehuisha uhai wao lakini afanaalek, Mau Mau kapigana na Mjerumani? data za kufikirika na kupika (kakiri mwenyewe, wala si yangu hayo). Kuwaonesha hayo mawili tu, hawana cha kujibu, mara oooh picha, mara oooh matusi. Wakaulizwa kifungo cha "report abuse" hawakioni? Kimyaaaaaaa.

Sasa wanataka kujuwa kuhusu Dr. Mwanjisi.

Nilisema humu, paper ya Hirji ni knocked out na sasa tutaendeleza mnakasha kwa faida ya wengi wetu kupata darsa, lakini si kwa kumjibu Hirji, hivi mtu ukae unajibu "hypothetically...data..." (data za kufikirika)?

Tupe darsa Al Alama Mohamed Said, hao wanaosema ngano ndiyo wanajazana humu kuchota ilmu, lakini kwa uhasid wao tu, hawataki kukubali, unafikiri wangekuwa hawafaidiki wangejazana humu?

Baniani mbaya kiatu chake dawa.

Wanasikitisha sana.
 
Hivi dhumuni lako hasa la kufunyua haya ni nini?

Lusungo,
Aliyeleta suala la Dr. Mwanjisi si mimi.
Soma post ya nyuma utaona hilo.

Mimi nimemjibu kuwa hapana haja ya kueleza habri zake.
Nahisi na wewe unakijua kisa cha huyu mzalendo.
 
kwa jinsi ninavyo fahamu dharau za mohamed said,mabandiko yanayo anzishwa na members wengine kwa lengo la kumkosoa,huwa hashiriki hata kama ID yake umekuwa tagged in,lakni hili la prof hirji yeye mwenyewe kaelekea kibra.yupo active ku refute kila post.hakika safari hii kashikwa pabaya.
 
Back
Top Bottom