BBC waianika Tanzania tena!

BBC waianika Tanzania tena!

Hata kwenye hivyi viwanda vikubwa nako hawa Osha huwa wanafuata mlungula tu, si vinginevyo
 
Hivi wewe ni journalist wa aina gani?hata common sense huna? Sasa kama kuna child labour mererani isesemwe? We Ulienda mererani ukakuta hakuna watoto?huu ukanjanja hadi lini?

Mkuu, tuna makanjanja wengi sana humu. Mwingine ambaye ni Bonafide genuine Kanjanja ni yule jamaa wa kipindi cha Kitimoto
 
msubiri naibu waziri Steven Masele aje akanushe na kuuombwa bwana Manyerere ujipime kama unafaa kuwa mhandishi wa habari
maana hii serikali yetu kazi yake ni kukanusha na kuwa na ndimi mbili za kigeugeu kama alivyowahi kusema mbunge mkosamali
 
We si uko huko mwanao wa kumzaa ushamuelekeza kwa maneno na vitendo jinsi ya kupeleka tindo na taarifa, ana uzoefu wa muda gani mpaka sasa????!!!!!


Mlete wa kwako kwasabb amekosa malezi ya baba na mama ndo ataweza. maana mnazaazaa tu na hamuwatunzi mnaishia kutelekeza familia na ndio hao wanaokuja huku hakuna mtoto mwenye malezi bora na maisha bora ambae mzazi wake anawajibika kikamilifu utegemee atakuja huku. wakwangu hawezi kuja huku kuja huku kwa maana mimi ni tajiri anapata kila kitu.
 
jiheshimu kama Deogratius Balile, anajua kuvaa na kuzungumza na pia yupo objective
 
Mlete wa kwako kwasabb amekosa malezi ya baba na mama ndo ataweza. maana mnazaazaa tu na hamuwatunzi mnaishia kutelekeza familia na ndio hao wanaokuja huku hakuna mtoto mwenye malezi bora na maisha bora ambae mzazi wake anawajibika kikamilifu utegemee atakuja huku. wakwangu hawezi kuja huku kuja huku kwa maana mimi ni tajiri anapata kila kitu.

Another set of sperm and ovum wasted!!!!!!!
 
kama suala ni child labour , hiyo inaweza hata kuanzia nyumbani kwako, check umri wa house-girl.
 
Nilitembelea Chunya, Makongorosi, Matundas, Itumbi, Mapogoro na sehemu nyingi za huko Chunya wanakochimba dhahabu.

Cha kushangaza nimekuta watoto wa shule ikifika break time wanaenda mtoni au migodi ya karibu na shule zzao ya kienyeji na kutafuta dhahabu.

Hao hata uwazuie vipi hawazuiliki washaonja raha ya pesa.

Ya huko Mererani siyajui.

Ni wakati muafaka, Serikali ijikite kuhakikisha hawa watoto wanasoma tena sehemu kama hizo za madini wawe wanaanza kufundshwa mambo ya madini kuanzia primary.

Si vyema kuwawacha wanatumika kutafuta pesa wakati ambao ilitakiwa wapate haki zao za msingi za kusoma na kucheza.
 
Haya sasa matusi! Suala la ajira mererani kwa watoto si kubwa wala la kulazimishwa. Kuna watoto nilibaini wamefiwa wazazi wote. Hao wanaingia pale kuchakuachakua kama ilivyo sehemu nyingine. Ninachokataa ni kile cha kuonesha kama child labour ya pale ni jambo lililobarikiwa na vyombo husika au na matajiri wa migodi.

Hivi umewaza nini mpaka ukaandika haya,uko sawa kabisa au labda umetumia kilevi! Wewe si mwandishi wa habari kitaaluma kabisa,mbona unanipa wakati mgumu kuamini kama maneno haya yanatoka kwa mtu anayejitambua,watoto wakifiwa na wazazi wao wanakuwa wakubwa au wanageuka wanyama hivo kuwaweka kwenye kundi la watoto wanaofanya kazi migodini ni kosa!

Umenisikitisha sana sana Manyerere sijajua unafanya yote haya kwa dhamira na malengo gani.
 
Matusi hayasaidii. Mimi nimesema nyoka hawazami. Wanaokoteza mabaki nje tu
Pale kuna vyama kama arema na tamida vinazuia watoto kuzama. Walioko nje ni kawaida kama ilivyo kwenye fukwe ambako kuna watoto wengi au ktk masoko.
Bado ni child labour na haihitaji kuwa wameajiriwa na mtu yeyote. Ile tu kuruhusiwa watoto kufanya kazi katika mazingira hayo ni kuvunja haki za watoto na kwa mantiki hiyo ni Serikali ya kulaumiwa.
 
kama suala ni child labour , hiyo inaweza hata kuanzia nyumbani kwako, check umri wa house-girl.

Yote hayaruhusiwi ila lazima kupata pa kuanzia na.unapoanza unaanzia kwenye hatari kubwa kama huko wanakopata adha na hatari ya afya!!!!!

Wa nyumbani anakosa haki ya kusoma ila atleast anakula vizuri, hatumii chemicals, hakai kwenye vumbi, anaelekezwa mazuri na mabaya, anakula, analala pazuri na salama ana uhakika wa matibabu!!!!!

SIO SAWA KWA VYOVYOTE VILE ila ana nafasi nzuri zaid ya huyo wa mgodini!!!!
 
The Boss, hujui kitu. Watoto wapo nje wanaokota tu. Hakuna anayeingia shimoni. Nimekaa miezi miwili pale sikuona mtoto "nyoka" akizama chini. Wanaozama ni wana-apollo.

Si jambo la siri kwamba watoto wanatumika sana kama nguvu kazi katika migodi wa wachimbaji wadogo hapa Tanzania. Merarani ni sehemu tu ya tatizo lakini ukitaka kuona jinsi watoto wanavyotaabika na kazi za uchimbaji tembelea machimbo ta dhahabu yaliyopo Nyarugusu (Geita), Nyakagwe na Nyangalata (Kahama). Haya machimbo yote yanaendeshwa na wachimbaji wadogo/kati ambapo watoto ndiyo nguvu kazi kwa ujira mdogo. Manyerere Jacton fanya study ya kutosha kabla ya kukanusha ukweli uliopo.
Kitendo cha watoto wadogo kujishughulisha kuokota mawe Mererani ni moja ya child labour. Kuna watu wamewaajiri watoto hao kuokota chenga na wanalipwa kwa siku. Si jukumu la watoto kuokota chenga migodini bali wanapaswa kuwa shule. Watoto wanafanya nini katika maeneo ya machimbo?
 
nini kifanyike nafikiri ndicho kitu cha msingi si kuzungumzia kuliko kubishana as child labour ipo au hamna
 
Nani kawaajiri?

Sio lazima wawe chini ya ajira ya kampuni ama mtu flani ndo ujue kuwa hiyo ni ajira kwa watoto. Hoja ya msingi hapa ni kwamba ajira kwa watoto ni kinyume cha sheria. Kama ni watoto wa Kitanzania na ambao wanatoka katika familia zao na kwenda katika eneo la migodi hayo ni makosa. Ikiwa wewe ni mwandishi wa habari na unakiri kwamba ulikwenda mererani na uliwashuhudia watoto wakiwa katika eneo la mgodi na hukuona kama ni tatizo eti kwa kuwa tu walikuwa wanaokota mabaki utakuwa na matatizo. Kama ungewakuta wanao katika eneo hilo ungelinyamaza eti kwa vile wanaokota mabaki? Ukweli ni kwamba hata hao Tanzaniteone taarifa hii inawaathiri kibiashara na wala sio kuwanufaisha. Hii ni kwa sababu hakuna mahali popote duniani unakoweza kupata Tanzanite isipokuwa Tanzania tu. Kwa hiyo itakapotokea madini hayo kususiwa na dunia, ni wote wanaohusika na Tanzanite ndio watakaoathirika pasipo kujua ni nani kasababisha. Muhimu hapa ni kuacha visingizio na badala yake kuchukua hatua stahiki. Ukiwa kama mwandishi,hupaswi kuchagua upande mmoja na kuutetea huku ukiulinda upande mwingine. Au mazoea hujenga tabia? Manake wanasisa wamewageuza waandishi wetu mchague upande wa kuwasemea,tabia hiyo sasa mnaihamishia hata katika masuala ya msingi ya kijamii... BADILIKA!
 
mi nadhani tuangalie nini kifanyike ili kuokoa au kusitisha ilo swala la child labour
 
Back
Top Bottom