BBC Swahili fanyieni kazi hili...

May Day

JF-Expert Member
May 18, 2018
6,162
8,820
Mimi ni miongoni mwa wasikilizaji wa redio mbalimbali hapa nchini, miongoni mwa hizo ni BBC SWAHILI kupitia washirika wao. Si kwamba wanachonikwaza wao hakitokei kwenye redio nyingine la hasha ila naangalia na ukubwa wa shirika husika.

Hakuna shaka kuwa sehemu kubwa ya Wasikilizaji wa Kiswahili wanapatikana Tanzania, sasa Mtangazaji anapoleta taarifa kutoka Rwanda, na kusema "bei imepanda kutoka faranga elfu moja mpaka elfu tatu" mimi Mtanzania hapo naelewa nini?, najuaje hiyo bei kweli ni kubwa kwa kulinganisha na bei ya nilipo?. Kwa nini mnapotaja pesa za nchi nyingine msimsaidie Msikilizaji wenu kuelewa...kwa mfano mngeweza kulinganisha na shilingi au dola ya Kimarekani ambayo walau inatumika kwa kila nchi ya EAC...ili nami nitafanya hisabati kujua huo ughali ukoje.

Au wakati mwingine Mnamuhoji, kwa mfano raia wa Jamuhuri ya Congo, raia ataunga unga kiswahili hapo alafu Mtangazaji (Lubunga Byaombe au mwingine) atapokea na kuendelea na matangazo kana kwamba kila kitu kilichoongelewa na Raia huyo kimeeleweka, na wakati mwingine huwa najua kabisa kuwa hata wao Watangazaji hawajamuelewa huyo Mzungumzaji.

Sasa huwa najiuliza ni kwa vipi hamuoni haja ya Msikilizaji wenu kuelewa kila taarifa mnayoitoa?.
 
Ni Kwaajili Ya Watu Wanaoongea/Kusikia Kiswahili Bila Kujari Iwapo Anashida Kuongea
Wengine Wanajifunza Kiswahili Sanifu Kupitia Radio
 
Kiswahili kinaongelewa EAST AFRICA YOTE...na Africa mashaariki kunanchi 5 sasa ikiwemo Ruanda na Burundi
Lakini hoja yangu si umeipata?...hata aliyepo Rwanda akiambiwa bei ya mafuta Tanzania imepanda kutoka shilingi 2000 mpaka 2500 huenda atatamani kujua kama kweli ni ghali...na huenda akatamani kulinganisha na bei iliyopo nchini kwake...hivyo Wanaotutaarifu (BBC) wanawajibika kuhakikisha kila Msikilizaji anaelewa kwa walau kulinganisha hizo bei na dola ya kimarekani kwa kuwa ni rahisi kwa Mwananchi yeyote kufanya ulinganifu wa dola na currency ya nchi alipo.

Mathalan wakisema kutoka shilingi 2000 ambayo ni sawa na dola moja hadi shilingi 3000 ambayo ni sawa na dola moja na nusu, Msikilizaji atafanya hisabati kujua ongezeko likoje na labda kushawishika kujua ni kwa nini bei hiyo ipo juu kuliko kwao au vice versa.
 
Au unapomsikiliza Raia wa ndani ndani wa Jamuhuri ya Congo Kiswahili anachokiungaunga sidhani kama hata kuna Mtu anaelewa.

Wapo baadhi yao wana afadhali na Mtu utaelewa hata kwa asilimia 70-80, ila wapo wasioeleweka kabisa na ndio nadhani Watangazaji wanawajibika kutoa ufafanuzi wa kilichoongelewa kama wanavyofanya kwa Muongeaji wa Kiingereza..au la wasirushe hewani Mzungumzaji asiyeeleweka kwa Msikilizaji.
 
Ukisikiliza Wasafi huwa unaelewa kila kitu boss?
Huku nilipo hata siwapati Wasafi. Ila pia Wasafi na BBC hawalingani ndio maana nimesema hapo juu kuwa si kwamba idhaa nyingine hazina hayo makosa bali tofauti ya hadhi inawahukumu zaidi BBC.

Tuna redio nyingi tu za kijamii huku mikoani zina changamoto lukuki hata hujui uanzie wapi kuwalaumu.
 
Mimi ni miongoni mwa wasikilizaji wa redio mbalimbali hapa nchini, miongoni mwa hizo ni BBC SWAHILI kupitia washirika wao. Si kwamba wanachonikwaza wao hakitokei kwenye redio nyingine la hasha ila naangalia na ukubwa wa shirika husika.

Hakuna shaka kuwa sehemu kubwa ya Wasikilizaji wa Kiswahili wanapatikana Tanzania, sasa Mtangazaji anapoleta taarifa kutoka Rwanda, na kusema "bei imepanda kutoka faranga elfu moja mpaka elfu tatu" mimi Mtanzania hapo naelewa nini, najuaje hiyo bei kweli ni kubwa kwa kulinganisha na bei ya nilipo?. Kwa nini mnapotaja pesa za nchi nyingine msimsaidie Msikilizaji wenu kuelewa...kwa mfano mngeweza kulinganisha na shilingi au dola ya Kimarekani ambayo walau inatumika kwa kila nchi ya EAC...ili nami nitafanya hisabati kujua huo ughali ukoje.

Au wakati mwingine Mnamuhoji, kwa mfano raia wa Jamuhuri ya Congo, raia ataunga unga kiswahili hapo alafu Mtangazaji (Lubunga Byaombe au mwingine) atapokea na kuendelea na matangazo kana kwamba kila kitu kilichoongelewa na Raia huyo kimeeleweka, na wakati mwingine huwa najua kabisa kuwa hata wao Watangazaji hawajamuelewa huyo Mzungumzaji.

Sasa huwa najiuliza ni kwa vipi hamuoni haja ya Msikilizaji wenu kuelewa kila taarifa mnayotupatia?.

Sidhani kama BBC Swahili watakuwa na muda wa si Kulifanyia Kazi hili unallitaka au hata pia Kuyasoma tu haya Maelezo yako. Huwa hawapangiwi!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom