Analogia Malenga
Platinum Member
- Feb 24, 2012
- 5,286
- 10,834
Jumatatu ya Juni 5,2023, BBC Swahili imetangaza kuanza msimu wake mpya wa matangazo ya runinga kutokea mjini Nairobi nchini Kenya badala ya London, Uingereza.Mitandaoni mjadala umekuwa ni kwanini studio hizo zisingehamishiwa Tanzania kutokana na uasili na idadi kubwa ya wazungumzaji wa lugha ya kiswahili.
Mwanahabari mtanzania Mubelwa Bandio, anayefanya kazi zake nchini Marekani kwa upande wake anasema mazingira ya kuwekeza na kufanya kazi za uanahabari nchini Tanzania ni magumu na yaliyoandamwa na urasimu mkubwa kulinganisha na jirani zetu Kenya.
Mwanahabari mtanzania Mubelwa Bandio, anayefanya kazi zake nchini Marekani kwa upande wake anasema mazingira ya kuwekeza na kufanya kazi za uanahabari nchini Tanzania ni magumu na yaliyoandamwa na urasimu mkubwa kulinganisha na jirani zetu Kenya.