Kwanini CIA inajadili waziwazi mambo mabaya iliyoitendea China?

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
VCG111450473202.jpeg


Taarifa zilizovujishwa na waliokuwa maofisa wa ujasusi nchini Marekani kwa gazeti la Wall Street (WSJ) zimewaacha watu wakiduwaa. Inadaiwa kuwa, mtandao wa Shirika la Upelelezi la Marekani (CIA) nchini China, ambao ulivunjwa kwa utaratibu maalum na Shirika la Upelelezi la China muongo mmoja uliopita, umekuwa ni vigumu kurejeshwa tena. CIA inadai kuwa, hivi sasa inajitahidi kujenga tena mtandao huo nchini China, na Mkurugenzi wa Shirika hilo, William Burns ameweka wazi kuwa, rasilimali ya bajeti iliyotengwa kwa ajili ya ujumbe wa China imeongezeka kwa zaidi ya mara mbili katika miaka mitatu iliyopita.

Kama inavyojulikana, Marekani imekuwa ikijihusisha na ufuatiliaji wa kina na ujasusi duniani kwa muda mrefu, na kujipatia jina la uhakika la ‘falme ya upelelezi.’ Vitendo hivyo, ambavyo kihalisi ni visivyofaa na vinakwenda kinyume na sheria ya kimataifa na hali ya kawaida ya kimsingi ya uhusiano wa kimataifa, haviwezi kukosa kufuatiliwa na jamii ya kimataifa. Lakini, wakati Wamarekani wanajadili vitendo hivyo waziwazi, hawaonekani kuwa na aina yoyote ya majuto wala aibu. Badala yake, kuna kile kinachoonekana kama hali ya ‘haki’, kana kwamba kuhusika na ujasusi ni heshima inayofurahiwa na Marekani. Hii si kwa sababu ya ‘nafasi nzuri kisaikolojia’ ya Marekani, bali ni matokeo ya umwamba na kukosa aibu ambayo yameendelea baada ya nadhari ya muda mrefu ya ‘upekee wa Marekani.’

Hata hivyo, wakati huohuo, inapaswa kufahamu kwa nini wanasiasa maarufu wa Marekani mara nyingi wanangukia katika aina ya mawazo madanganyifu, wakiamini kuwa, kati ya mambo mengine mengi, China daima inafanya upelelezi katika kambi za jeshi nchini Marekani, inasikiliza taarifa za siri, na kuiba nyaraka muhimu. Licha kuwa na nguvu bora ya kitaifa duniani, bado nchi hiyo inaonyesha hali kubwa ya kukosa usalama.

Waraka ulioandikwa na WSJ umeweka wazi mambo mengi. Kwanza, imeweka wazi matamshi ya CIA ya kujihusisha na vitendo vya ujasusi dhidi ya China, inawezekana hii ikawa ni katika jaribio la kuongeza thamani yake yenyewe na kutafuta kuungwa mkono Zaidi kifedha na Bunge la Marekani. Hata hivyo, hatua hii ni sawa na kujipiga risasi mguuni. Wakati Marekani inapiga kele na kulenga kile kinachodaiwa kuwa ‘wapelelezi kutoka China,’ mara zote inashindwa kutoa ushahidi halisi. Badala yake, inaanzisha kampeni za kuichafua China na kudai China kutoa ushahidi kuwa haina hatia. Mwelekeo huu umeonyesha kuwa, Marekani inatambua wazi kuwa madai yake ya ‘upelelezi’ hayana mashiko, lakini bila aibu inaendelea nayo kama vile ‘hakuna anayeweza kuwafanya lolote kuhusu hilo.’

Pili, waraka huo wa gazeti la Wall Street unathibitisha kuwa kazi ya kupambana na ujasusi ya nchini China ni ya ufanisi wa ngazi ya juu. Imeweza kuondoa abisa mtandao wa upelelezi wa Marekani nchini China na kuzuia mtandao huo kujengwa upya katika miaka 10 iliyopita. Haya ni mafanikio makubwa katika kupambana na ujasusi, na kuifanya Marekani kutetereka mbele ya kazi ya ulinzi dhidi ya ujasusi nchini China. Wakati China ilipofanyia marekebisho Sheria ya Kupambana na Ujasusi, ilikosolewa sana na maoni ya umma kutoka nchi za Magharibi. Lakini sasa inaonekana kama dhana nyuma ya ukosoaji huo ilikuwa ni kuishinikiza China kuondoa ulinzi wake na kuruhusu wapelelezi wengine kufanya shughuli zako kwa uhuru ndani ya mipaka ya China. Bahati nzuri ni kwamba, China haikuanguka katika mtego huu. China imeweza kujilinda na vitendo vya ujasusi hapo zamani, na pia itakuwa na uwezo wa kuzuia kuingia kwa siri kwa CIA nchini humo katika siku zijazo.

Tatu, waraka huo unatukumbusha kuwa, mfululizo wa kupambana na ujasusini lazima uimarishwe. Shirika la Ujasusi la Marekani limeonesha kwamba, kujenga tena mtandao wake wa upelelezi nchini China kwa sasa ndio lengo lake kuu na litaendelea kuwa hivyo katika siku za mbeleni. Mwaka 2021, kulikuwa na ripoti kwamba CIA imeanzisha idara maalum ya China, ikiwa ni idara pekee ya nchi moja katika Shirika hilo. Haya yote yanaweza kufanya hali ya China kupambana na ujasusi kuwa mbaya na ngumu Zaidi. Ni muhimu kusisitiza kuwa, mapambano dhidi ya ujasusi hayakinzani na sera ya China ya kufungua mlango zaidi kwa dunia, na mabadilishano ya kawaida ya kigeni hayataathiriwa wa kuvurugwa.

Baada ya kuwekwa wazi kwa kitendo cha Marekani kufanya ujasusi isivyo halali kwa wenza wake ikiwemo Korea Kusini, Japan na Ujerumani, nchi hizo hatimaye zilichagua kukubali kimya kimya fedheha hiyo, lakini China kamwe haiwezi kufanya hivyo!
 
Back
Top Bottom