Hili ni kwa nchi nzima mkuu UWT wameshikana na akina mama BAWACHA WANAWAZA VITI MAALUMUMkuu kwa nini naumia nilikwenda kijijini kwetu sehemu za Singida,kiukweli CDM inakubalika sana pale
na vuguvugu la mageuzi kwelikweli,ila tatizo nililoliona ni wanawake kutwa na vilemba vya CCM vichwani
nikaamua kufanya utafiti mdogo kwa nini akina mama wako nyuma kwenye mageuzi ,majibu yao ni karibu
yalifanana kuwa wao wanatembelewa na kujaliwa na akina mama wa CCM hawajaona mama wa CDM hivyo
wanadhani CDM inatakiwa kuwa kwa vijana na wanaume.Nilichogundua ni kuwa UWT wanajitahidi kuwabana
wanawake hasa vijijini wakijua ndio angalau wanaweza kupata kura zao.Viongozi Bawacha kama hamna wito
wa uongozi kaeni pembeni.