HS CODE
JF-Expert Member
- Jul 5, 2019
- 1,784
- 4,413
Wakuu! Naomba nitumie salamu zilizo zoeleka zaidi visiwani, “Hamjambo?”, “Mumesalimika?”.
Niende moja kwa moja kwenye mada. Pamoja na mateso yote wanayopitia waliotumia muda mwingi mashuleni ambao kwa sasa wamezagaa kila kona ya taifa hili, kiasi cha baadhi kuwatafsiri kama wamepoteza uelekeo, ndugu zangu aliyesoma kasoma.
Afadhali ya yeye anayeteseka muda huu, lakini matumaini ya kesho yake kubadilika ghafla ni makubwa.
Fikiria mtu ambaye ajira zote zinazotoka iwe ni taasisi nyeti au taasisi yoyote ya serikali au binafsi yeye hazimuhusu kwa sababu hajasoma.
Ni bora aliyesoma anaweza kufanya hata kazi za asiyesoma kuliko asiyesoma ambaye kazi za aliyesoma hazimuhusu.
Ni rahisi zaidi kwa aliyesoma kuishi maisha ya ahueni, yaani kati kwa kati sio chini wala sio juu kuliko asiyesoma, asiyesoma akipigika anapigika kweli.
Najua pande zote mbili zina sumu kali sana, na zinatafuta pakuzitemea. Nawakaribisha kwenye huu uzi, zitemeeni hapa. Bila kujali umesoma au hujasoma, unaweza kukaa upande wowote.
Ama namna gani, wewe unaonaje?
Asante.
MUHIMU
Kuendana na uzi huu, msomi ni mwenye elimu ya fani kwa angalau ngazi ya Cheti.
Niende moja kwa moja kwenye mada. Pamoja na mateso yote wanayopitia waliotumia muda mwingi mashuleni ambao kwa sasa wamezagaa kila kona ya taifa hili, kiasi cha baadhi kuwatafsiri kama wamepoteza uelekeo, ndugu zangu aliyesoma kasoma.
Afadhali ya yeye anayeteseka muda huu, lakini matumaini ya kesho yake kubadilika ghafla ni makubwa.
Fikiria mtu ambaye ajira zote zinazotoka iwe ni taasisi nyeti au taasisi yoyote ya serikali au binafsi yeye hazimuhusu kwa sababu hajasoma.
Ni bora aliyesoma anaweza kufanya hata kazi za asiyesoma kuliko asiyesoma ambaye kazi za aliyesoma hazimuhusu.
Ni rahisi zaidi kwa aliyesoma kuishi maisha ya ahueni, yaani kati kwa kati sio chini wala sio juu kuliko asiyesoma, asiyesoma akipigika anapigika kweli.
Najua pande zote mbili zina sumu kali sana, na zinatafuta pakuzitemea. Nawakaribisha kwenye huu uzi, zitemeeni hapa. Bila kujali umesoma au hujasoma, unaweza kukaa upande wowote.
Ama namna gani, wewe unaonaje?
Asante.
MUHIMU
Kuendana na uzi huu, msomi ni mwenye elimu ya fani kwa angalau ngazi ya Cheti.