Kweli kabisa, labda miaka mingi sana ijayo.Haitatokea tena kupatikana jembe kama Magufuli
Magufuli was the best EVER president R. I P . Upembuzi wa Kadogosa unaonesha mzee JPM alikuwa mfanyakazi c mwanasiasa wa porojo za majukwaa anayetaka haki za mashoga na haki za wafungwa waitwe wanafunziAliheshimu Demokrasia
Chaguzi zilikuwa za Haki na Huru
Wapinzani Walifanya Mikutano yao bila KAMATA kamata ya Polisi
Wabunge 19 Wasio kuwa na Chama Walivuliwa Ubunge Wao
Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
Mpaka leo timu Msoga nadhani wameanza kuelewa hasara tuliyopata kama taifa kwa kumpoteza Magufuli.Magufuli was the best EVER president R. I P . Upembuzi wa Kadogosa unaonesha mzee JPM alikuwa mfanyakazi c mwanasiasa wa porojo za majukwaa anayetaka haki za mashoga na haki za wafungwa waitwe wanafunzi
Mkuu karibu tena kule jukwaani, bado tunaliendeleza gurudumu. Wakenya wamesanda kabisaKitambo sana bro The best 007 tangu kipindi kile i think 2020 kwenye jukwa la battle Dar vs Nairobeee. Mimi tangu afe mwamba sikutokea tena pale jukwaani maana niliona hakuna cha kujivunia tena
Unaanzaje kumlinganisha Maghufuli na taka taka zilizopo sasa hv , wanamkosea heshima SanaMagufuli was the best EVER president R. I P . Upembuzi wa Kadogosa unaonesha mzee JPM alikuwa mfanyakazi c mwanasiasa wa porojo za majukwaa anayetaka haki za mashoga na haki za wafungwa waitwe wanafunzi
Nakumbuka time ile wenyewe walishakubali ile speed yetu kila siku wanaletewa multibillions projects, wao walibaki na white elephants projects zao , mpaka alipokufa magu nikawa nikipita kule roho inaniuma sanaMkuu karibu tena kule jukwaani, bado tunaliendeleza gurudumu. Wakenya wamesanda kabisa
Ni kweli speed imepungua ila bado tunawatesa na miradi ile ile aliyoanzisha mwamba.Nakumbuka time ile wenyewe walishakubali ile speed yetu kila siku wanaletewa multibillions projects, wao walibaki na white elephants projects zao , mpaka alipokufa magu nikawa nikipita kule roho inaniuma sana
Inashangaza sana.Unaanzaje kumlinganisha Maghufuli na taka taka zilizopo sasa hv , wanamkosea heshima Sana
Bro nina kumbukumbu zako since march 2021, kuna comment ulisema hiviNi kweli speed imepungua ila bado tunawatesa na miradi ile ile aliyoanzisha mwamba.
Umetisha sn mkuuBro nina kumbukumbu zako since march 2021, kuna comment ulisema hivi
" KATI YA WATU 10 WALIOKUA WANAMCHUKIA MAGUFULI,
-WATANO WANAMCHUKIA KWA MKUMBO.
Screenshot hyo hapo
- 3 HAWAJUI KWA NINI WANAMCHUKIA.
- 2 NI UPINZANI UCHWARA."
View attachment 2620828
We noma mwanangu kwa kutunza kumbukumbuNA HIZI NI QUOTE ZA BAADHI YA SPEECH ZISIZOSAHAULIKA ZA MAGUFULI ULIZIANDIKA KWENYE LILE JUKWAA NILIZISCREENSHOT MARCH 2021 NNAZO MPAKA LEO, The best 007
View attachment 2620832View attachment 2620830View attachment 2620831
Kalindeni.kaburiMpaka leo timu Msoga nadhani wameanza kuelewa hasara tuliyopata kama taifa kwa kumpoteza Magufuli.
Ukiona hunachakuonge wew tukanatu nayo ni pointHabari zenu wanajukwaa, baada ya kugundua kuwa mtu huyu imeshindikana kabisa kusahaulika ndani ya mioyo ya Watanzania na wasio Watanzania nimeona nianzishe uzi ambao utagusa pande zote yani wale wanaodhani alikuwa Rais bora na wale wanaodhani hakuwa Rais bora.
Ikumbukwe kwamba tangu amefariki mtu huyu imepita takribani miezi sita na siku kadhaa mpaka hapa ninapoandika huu uzi, sasa naomba wale Magufulians waseme kwanini wanadhani huyu alikuwa Rais bora kabisa kuwahi kutokea Tanzania na watoe sababu za kusema hivyo pia wale wanaodhani hakuwa Rais bora watoe sababu zao.
Ndugu zangu nimelazimika kuanzisha huu uzi kutokana na kile ninachokiona kwamba jina la Magufuli sasa limekuwa kama dini mana unapomponda tu kama pembeni yako kuna mfuasi wake basi hawezi kukuacha salama.
Hii imepelekea kutokea mikanganyiko na sintofahamu kwenye majukwaa mbalimbali inafikia kipindi unakuta mada haihusiani na Magufuli lakini uzi unaharibika kwa sababu ya u-Magufuli vs u-Anti Magufuli.
Sasa ndugu zangu tusiendelee kuharibu nyuzi za watu, kama una dukuduku lako kuhusiana na kiongozi huyu mashuhuri aliyewahi kuongoza Tanzania basi weka hapa dukuduku lako au maoni yako juu ya mwamba huyu yaweke hapa jamii ifahamu ni kwa namna gani kiongozi huyu alikuwa mzuri au mbaya.
Nianze na mimi binafsi msimamo wangu juu ya JPM, ni kwamba namuona kama Icon na benchmark ya viongozi waliopo na watakaokuja kwasababu zifuatazo
1. Muanzilishi wa Tanzania mpya. JPM alikuwa kiongozi mwenye uthubutu wa kuwakaripia viongozi wote walio chini yake kwa mamlaka aliyopewa kikatiba iwe ni viongozi wa kuteuliwa na yeye mwenyewe au wa kuchaguliwa basi viongozi walitii, ilikuwa ni utaratibu kwa viongozi wa Tanzania waliochini ya Rais kikatiba kujiamulia mambo watakavyo wao ikibidi hata kukaidi maagizo yanayotolewa na Rais, hii ilipelekea huko nyuma nchi yetu kupoteza muelekeo lakini chini ya JPM maagizo yakawa yanafuatwa na kasi ya utendaji ikawa kubwa kuwahi kutokea Tanzania.
2. Kiongozi mkweli daima. Mtu huyu alikuwa ni moja kati ya binadamu wachache wakweli, alikuwa mwanasiasa pekee asiyejuwa kuongopa, ilifika mahali akajiingiza kwenye mgogoro na wanasiasa wenzake ndani ya CCM kwakuwa wengi wao hawakuzoea ukweli, JPM akisema hili hapana basi juwa kwamba halitatokea au akisema hili linawezekana basi juwa hivyo, hakuwa mtu wa kupepesa macho, alikuwa na uwezo wa kuongea ukweli hadharani pasipo kuficha ficha kitu chochote, hii ikapelekea viongozi waliokuwa wanaendekeza siasa majitaka kumuogopa kwani mzee yule hakuwa akijali kama unatokea CCM au upinzani.
3. Msimamo mkali. Chini ya JPM tuliona Tanzania yenye msimamo na isiyoyumbishwa na mtu yeyote au taifa lolote lile liwe na uchumi mkubwa au mdogo, hii ikapelekea Tanzania kufahamika zaidi kimataifa na duniani kote.
4. Kiongozi mwenye maono. Hayati JPM alikuwa ni kiongozi mwenye maono, hili liko wazi kwani maono yake hasa kwenye nyanja za kiuchumi ndio zikapelekea nchi yetu kuingia uchumi wa kati kabla ya muda uliokusudiwa, hii ilitokana na maono na jitihada zake kuhakikisha nchi yetu inajitegemea kwa kuanzisha miradi iliyoonekana haiwezekani lakini chini ya uongozi wake ikawezekana, pia maono yake yalijidhihirisha hata kwenye ugonjwa ulioikumba dunia kwa sasa ugonjwa wa Corona, nchi nyingi duniani zimeanza kutumia theories alizozitoa Hayati JPM.
5. Kiongozi mwenye ushawishi. Hayati JPM alikuwa na karama ya ushawishi mbele ya jamii, alikuwa na uwezo wa kusema jambo fulani na jamii nzima ikakubaliana naye kwa asilimia kubwa, kiukweli kabisa hata leo hii JPM akiamka na akasema watanzania wachanje basi believe me dawa za kuchanja hazitatosha, hii ni kutokana na imani kubwa aliyojiwekea mbele ya jamii kwakuwa watanzania waliamini kwamba JPM ana upendo wa dhati kwa wananchi wake na hawezi kuwarubuni kwa namna yoyote ile.
6. Mtu wa Mungu. Licha ya mapungufu yake kibinaadamu lakini ni ukweli usiopingika kwamba JPM alikuwa ni mtu wa Mungu, siku zote za uongozi wake hakuacha kumtegemea Mungu na hili alilifanya hadharani kwa kumtaja Mungu popote alipoenda na watu wake wakaribu wanasema mzee yule ulikuwa ni utaratibu wake kumtanguliza Mungu mbele.
7. Kipenzi cha wengi. Ukiacha mitandao ambao kuna wachache wanaomsema vibaya Magufuli ni dhahiri shairi kwamba hayati alipendwa na wengi, hii ilijidhihirisha pale alipofariki, umati uliojitokeza haukuwahi kutokea na sidhani kama utatokea kwa siku za karibuni, sio kwamba walioenda kumuaga walienda kukejeli bali waliguswa haswa, vilio kila pembe ya waagaji na kila sehemu mwili ulipoenda, hii inathibitisha ni jinsi gani watanzania walimpenda kiongozi wao.
Yako mengi ya kumuelezea Magufuli lakini itoshe kwa haya niliyoyaandika kumuelezea, mengine niwaachie ninyi wenzangu karibuni.