Bashiru Vs Membe: CCM yatoa msimamo wake kuhusu suala hilo

Bashiru Vs Membe: CCM yatoa msimamo wake kuhusu suala hilo

Sasa mtu anaitwa na Katibu Mkuu wa Chama ambaye ndiye mtendaji Mkuu wa Chama, unamletea kibesi tena unamdharau kabisa wazi wazi na kupitia mitandaoni. Sasa inamaana wewe ndiye umekuwa bosi wake ama?

Hivi kama ni nyumbani kwako umetembelewa na wageni lakini bahati mbaya ukajampa na ukamsingizia mtoto wako kuwa amejamba lakini kenyewe kaanze kukushushua mbele ya wageni na kukana huku wakiku-point tena wewe, utavumilia hiyo hali.

Kwani wakati akina Kinana wanawaamrisha akina Lowassa wasifanye kampeni huku wakiwatishia kuwakata majina yao, walikuwa wanafanya hivyo kwa kuwa na ummarufu ama kwa kanuni za Chama? Mbona Lowassa alikuwa akitii bila kurudishia madongo yaliyokuwa yakitolewa na mtandao wa Membe ukiongozwa na akina Nape Nnauye na baadhi ya Viongozi wa UV-CCM?
 
CCM itatawala milele kwa namna hii ya upinzani kukataa mauno kwa kila ngoma inayopigwa na CCM....hapa ni mipango ya CCM kuwatoa wapinzani kwenye hoja ya URAIS 2020 na WAPINZANI walivyo MAZUZU wameacha kila kitu sasa wamepagi kushabikia (KUKATA MAUNO) ngoma wasiyoijua....
Hahahahaaaa
 
Upo sawa kabisa. Kuna watu kwa umahili wao hata kama uwapendi lakini ni maslahi ya Taifa.

Unamuacha Membe ana hang hang peke yake bila kazi za kumkeep bize unategemea nini.

Unamuacha Nape naye ana hang hang bila kazi yoyote unategemea nini.

Wanajipa kazi wenyewe na moto utaonekana.

(kwa mtazamo wangu japo simpendi NAPE ni kiungo mzuri na muhimu sana kati ya Chama na serikali amezunguka nchi nzima kwa ajiri ya Magufuli amazozana vikali na wapinzani mpaka Leo hii Upo madarakani).

Huwa napenda sana kukutana na Geniuses / Great Thinkers hapa Jamvini JamiiForums kama Wewe Mkuu. Upo vizuri na nimekukubali.
 
Chadema wako bize kumpotosha Membe kama walivyompotosha Lowasa.

Mahaba ya Chadema kwa Membe yanasitajaabisha , badala ya kumlilia Mbowe yupo gerezani wako bize kumlilia mwana ccm Membe!!!!
Haiyumkini utakuwa umelewa au umezidiwa na hali fulani isiyokuwa nzuri kiafya! Mkiparurana huko lumumba kisababishi ni cdm, Lowasa au Mbowe kwani ni watu stadi sana kwa kupiganisha! Na lazima awazalishe mtoto wa kiume huyo Membe! 2020 atakalia ikulu, sijui utajinyonga!
 
Tunapokaribia uchaguzi wa 2020 hakuna ubishi kuwa ndani ya CCM kuna makundi, kwa elewa wangu kuna kundi la Bernard Membe aliyekuwa mgombea 2015 vile vile bado kuna masalia ya kundi la Lowassa. Ingawa Magufuli naye anajitahidi kutengeneza kundi lake lkn bado changa halina nguvu ya kisiasa nguvu yake inategemea vyombo vya dola.

Wasioamini siasa za fitina ndani ya CCM hasa uchaguzi unapokaribia wamuulize, Salim Ahmed Salim, John Malecela, Mohamed Bilali, na Jakaya Kikwete.

Baada ya jina la Membe kuanza kusikika kuwania urais tayari fitina zimeanza kutengenezwa na mitandao imeanza kujengwa, hofu kubwa ya CCM ni ndani ya chama kuliko nje ya chama, inawezekana kabisa kwa mara ya kwanza rais Magufuli akapata mpinzani.

Rais Magufuli anajua jinsi alivyopita kwenye tundu la sindano wakati wa mchakato wa kura ya maoni, anajua fika nguvu ya Lowassa aliyokutana nayo, bila fitina za Mkapa nafikiri leo asingekuwa pale, ndiyo maana ameanza jitihada za kumuweka Lowassa karibu na himaya yake, anajua Lowassa ni kiungo muhimu kati yake na wanamtandao, ni muda tu tutaanza kuona vijana wa CCM mitandaoni na kwenye majukwaa wakimsafisha Lowassa.

Kwa upande mwingine mtandao wa Membe ni mpana, ukimtaja Membe umemtaja rais msataafu Jakaya Kikwete umemtaja Pius Msekwa, umemtaja Hawa Ghasia, umemtaja Kinana, Nape, Rostam Azizi. Membe ana marafiki wengi ndani na nje ya nchi, anao marafiki Falme za Kiarabu, Mabalozi wengi wa western countries ni washirika wake.

Membe siyo Lowassa kuwa ukimfanyia figisu kidogo tu atakubali yaishe. Kosa alilofanya Lowassa ambalo sidhani kama Membe atalifanya ni kuhama chama, najua Membe atapambana ndani ya chama kwa kutumia uzoefu wake, ujuzi wake, na diplomasia yake.

Membe hana papara ni mtu mkimya, mwana diplomasia mbobevu, mwana usalama aliyefanya kazi ya intelijensia ndani ya system kwa muda mrefu na amepanda sana vyeo ndani ya idara hiyo nyeti na hivyo anazijua siri nyingi za serikali na namna nzuri ya kufanya umafia.

Tukumbuke tu kuwa aliyemfix Lowassa hadi kuamua kuondoka CCM ni komred Membe na mtandao wake wa akina Kinana, Nape, kwa hiyo CCM ya akina Bashiru Ally ijiandae kisaikolojia, isidhani itapata mtelemko itakapokuwa ina dili na mbobezi wa fitina Mh. Bernard Membe.
 
Hii ndio jf!! Am proud of it.. Am proud of jf members and more so Am very proud of Gentamycine !! Huyu ndugu ni role model wangu sana hapa jamvini so ukiwa na mtu wa namna hii inatakiwa uwe very clean and more detailed kwenye nyuzi zake!! Kwani atakuaibisha kwa hoja zake kuntu na style yake ya uandishi!!

Naomba piá nami nichangie kidogo kwenye uzi huu ambao unagusa mahaba ya waliowengi ikiwemo mie!!

Kwanza mtoa hoja ka -analyse sana na vema juu ya jinsi uongozi wa sasa ulivyocheza game hili mara baada ya uchaguzi na hatimae serikl ikaundwa na kajaribu kuonyesha jinsi wachezaji ambao kwa vyovyote vile walishiriki kikamilifu ktk mechi ilê na hatimae timu yetu Mimi na mtoa mada kama stakua nakosea ilishnda!!! Kajaribu kuonyesha jinsi hawa wachezaji mahiri kabsa walivyosahaurika kwenye kupewa tuzo mara baada ya mechi ile..

Ni ukweli usiofichika popote palipo na watu hapakosi kuwa na neno,,, na kwa vyovyote vile Mh Magufuli alijua na anajua kabsa juu ya suala hili ,na kisiasa mwisho Wa uchaguzi A ni maandalizi ya uchaguzi B

Ndg naomba niseme hv ktk timu ya washauri wa magufuli hakuna popote walipokosea kwa maoni yangu,, kwani ktk vita au mpambano wowote hasa huu wa kisiasa watu na wataalamu wa mambo haya walishauri mfano wake ni kina Sun Tzu na kina Nicole Marchiavelian ambao waliwahi shauri hivi :

Mfano Sun Tzu kwenye kitabu chake cha ( THE ART OF WAR ) alisema hivi there are the best things to put in considerations when a leader wants to win a War kwamba ( Make your enemy believe that you are very far when you are actually very close to them But when you are very far make them believe that you are very close to them) ukiangalia principle hii utaelewa jinsi washauri WA JPM walivyoitumia vzr hii concept... Yaani huenda Membe anauhakika kabsa kwamba Magufuli yu mbali nae na sasa kaamua kujidhihirishia hilo kwa kufanya aanayoyafanya sasa na matokeo yake wote tumeanza na tutazd kuyaona na kiukweli JPM lazima ashinde vita yetu macho ,yaani hapa Magufuli kajifanya kuwa yuko mbali sana na membe kwani kamfanya na yeye ajijue hvyo kwa kushndwa kumteua na kwa dhana hii sasa Magufuli Vita kaishinda kwani badala ya kufikiria Membe afanye nini kucheza na akili za JPM yeye kaingia mazima mazima akidhani atashinda kumbe nooooooo!!! Na angetulia pengne Magufuli angetumia mbinu nyngne

Hebu tuangalie pia Nicole Marchiavelian alisema nn juu ya masuala ya uongozi hasa pale alipokuwa akiwashauri wafalme mbali mbali.
Huyu jamaa alikuja na principles kama

1 It's better to be feared than to be loved... Yaani hapa alichokifanya JPM kasema potelea mbali wacha wanichukie ila mie nachotaka a b c na matokeo yake Membe kakubali kwamba anamchukia na kwakua Magufuli analijua hilo kwqmba hataki kupendwa kinafiki ila bora umchukie ndo maana wameanza kuhaha wenyewe kama huyu sashv licha ya kumuona sashv kama mshnd ila sheria zitambana za CCM na kesho Magufuli atawin.

2 People Will inevitably lie to you, so it is therefore acceptable to lie them too... Hapa Kama Gentamycine the best analytic,, alivyoona yaani huenda hawa washauri kweeli walibugi kwa kumdanganya JPM sasa kwakua anajua namna ya kuruka kamba jamaa aliwakubalia ili tu kutuliza mambo ila alijua kabsa kwamba hapa yawezekana jamaa wanasema hv tu ili tu mambo yaende ila ntawadanganya na mie.... Na hiki ndicho kilichotokea.... Membe kamembeka kweli kweli pamoja na washauri kama kweeli walifanya hvyo as allvosema mtoa mada so mshindi ni JPM koz tukubali tukatae endapo membe ataendelea kujifanga kaota mabawa na uana diplomasia wake akumbuke yeye ni mdg mnooooo kwa chama so lolote litatokea

3 Trust no one, but make follow up and prove by yourself. Hapa Magufuli huenda aliambiwa hivi ama vile ila alitumia principle hizi akasema siamni mtu hadi nijiridhishe Mwenyewe na hapa kajiridhsha kwamba jamaa anataka hiki kweeli kama nilivoambiwa so sasa kaamua kutafuta suluhu kwani alivyotega vyote vimenasa.....

Kwahyo kwangu binafs naweza sema membe ataonekana mshnd kwenye mitandao siku izi mbili tatu ila ukweli ni kwmba hawezi akawin... Magufuli namuona kwa jicho Lang kama mtu ambayo ni digitalized kwenye masuala aya na yuko makini sana akiongozwa na timu yake na ukweli wawe makini sana maadui wake kwani matokeo yake watakuja kushndwa kwa aibu..... Mfano wake ni membe... So jamaa alimuacha ili aje amalize kqbsa nguvu yake kuliko kumpa cheo koz pengne angejijenga japo napenyewe kwa uwezo WA timu Magufuli sizani kqma ange wiiin

Shukrani sana niko tayari kukosolewa!!!!!!
 
Haiyumkini utakuwa umelewa au umezidiwa na hali fulani isiyokuwa nzuri kiafya! Mkiparurana huko lumumba kisababishi ni cdm, Lowasa au Mbowe kwani ni watu stadi sana kwa kupiganisha! Na lazima awazalishe mtoto wa kiume huyo Membe! 2020 atakalia ikulu, sijui utajinyonga!
Vipi ikiwa
Lowasa vs Membe
 
HIvi mambo ya katibu wa CCM na wanachama wake yanatuhusu nini sisi? Membe si mwanachama wa CCM? Kwani kaitwa Polisi? Kaitwa ofisini kwao, baadhi munazoza na kushangilia eti 2020 wapi huko. wana CDM, CUF, TLP waseme nini?
 
Yanasemwa mengi na yatasemwa mengi ila kama kuna Kosa kubwa ambalo Rais Dkt. Magufuli amelifanya ( na naamini hapa atakuwa alishauriwa vibaya na Watu wake ) ni kuweka mbali au kukaa mbali na ' Fundi wa Diplomasia ' Benard Membe na kwa maoni yangu huenda leo hii tunaona baadhi ya matatizo ya hapa na pale yanatokea hasa Kimataifa kwakuwa hana ' Mafundi ' kama akina Membe.

Hata kama huyu Mtu ( Membe ) aliamua Kuachana na Ubunge lakini Mimi kama GENTAMYCINE bado naamini kwamba Mheshimiwa Rais Magufuli kwa ' Mandate ' yake kama ' Executive ' bado alikuwa anaweza Kumtumia katika ' Baraza ' lake la Mawaziri au hata katika maeneo mengine hasa ya Kidiplomasia ambayo kwa Mimi naona kwamba hadi hivi leo bado tunafanya vibaya na mifano juu ya hili iko mingi tu.

Kwa Mtu mwenye ' exposure ' kubwa na ' iliyotukuka ' kabisa huku akiwa amewahi Kuhudumu katika moja ya Idara / Taasisi muhimu / nyeti Kiusalama katika nchi hii kama Mzee Benard Membe leo hii kumuacha awe tu hivi ' huru ' nadhani ' technically ' kabisa hapa kuna Kosa kubwa sana lilifanyika ama kwa Watu kutokujua au Mheshimiwa Rais Magufuli alilishwa ' Sumu ' za ' Kimajungu ' na Watu wake wa karibu ambao anawaamini nae ' Sumu ' ikamuingia vilivyo na matokeo yake ndiyo haya sasa.

Sehemu yoyote ile hasa kwa Watu wenye ' akili ' sawasawa pale ukishaona kuwa Mtu fulani bado ana ' Potential ' fulani katika nchi ambayo ina Tija ya Kimaendeleo basi yakupashwa uendelee Kumuamini na Kumtumia ila kama pia umeona mwenyewe kwa Vipimo vyako kuwa GENTAMYCINE ni ' Tishio ' Kwako basi njia pekee ya Kumuweza ni ' Kumjumuisha ' katika ' Utawala ' wako ili uweze Kumlevya Kimamlaka lakini pia Kumdhoofisha ' Kimbinu ' pasipo Yeye kujua lakini kumuacha awepo awepo tu ni hatari kubwa kama ambavyo tunaanza kuiona sasa.

Hata hivyo bado hatujachelewa na hasa hasa Rais Magufuli bado hajachelewa kwani Mimi GENTAMYCINE naamini tena kwa 100% kuwa Mzee Benard Membe anaweza kuwa ni ' msaada ' mkubwa mno wa Kiutawala Kwake ama kwa huu muda alioubakisha kwa muhula wale huu wa Kwanza au hata kwa muhula wake wa pili na mwisho. Asiwasikilize wale ' Wanafiki ' ambao wamemzunguka na ambao hata Yeye pia alishakiri mara nyingi tu kuwa walishawahi hadi kumwambia kuwa Katibu Mkuu wa sasa wa CCM Ndugu Bashiru Ally Kakurwa hafai lakini Yeye mwenyewe akajiridhisha nae na kuamua kufanya nae Kazi na tunaona anafanya vyema tu.

Yangu ni hayo tu ila Mzee Benard Membe bado ni ' Lulu ' kubwa katika ' Utawala ' huu asiachwe na apewe ' Majukumu '.

Nawasilisha.
Duh!! Wewe unamjua Membe kuliko mkuu wa nchi!! Unapata taarifa muhimu kuliko mkuu wa nchi!! Mh!! Maajabu haya!! Acha ujuaji mzee wa kutoka na kujaa mapovu!!!
 
Yanasemwa mengi na yatasemwa mengi ila kama kuna Kosa kubwa ambalo Rais Dkt. Magufuli amelifanya ( na naamini hapa atakuwa alishauriwa vibaya na Watu wake ) ni kuweka mbali au kukaa mbali na ' Fundi wa Diplomasia ' Benard Membe na kwa maoni yangu huenda leo hii tunaona baadhi ya matatizo ya hapa na pale yanatokea hasa Kimataifa kwakuwa hana ' Mafundi ' kama akina Membe.

Hata kama huyu Mtu ( Membe ) aliamua Kuachana na Ubunge lakini Mimi kama GENTAMYCINE bado naamini kwamba Mheshimiwa Rais Magufuli kwa ' Mandate ' yake kama ' Executive ' bado alikuwa anaweza Kumtumia katika ' Baraza ' lake la Mawaziri au hata katika maeneo mengine hasa ya Kidiplomasia ambayo kwa Mimi naona kwamba hadi hivi leo bado tunafanya vibaya na mifano juu ya hili iko mingi tu.

Kwa Mtu mwenye ' exposure ' kubwa na ' iliyotukuka ' kabisa huku akiwa amewahi Kuhudumu katika moja ya Idara / Taasisi muhimu / nyeti Kiusalama katika nchi hii kama Mzee Benard Membe leo hii kumuacha awe tu hivi ' huru ' nadhani ' technically ' kabisa hapa kuna Kosa kubwa sana lilifanyika ama kwa Watu kutokujua au Mheshimiwa Rais Magufuli alilishwa ' Sumu ' za ' Kimajungu ' na Watu wake wa karibu ambao anawaamini nae ' Sumu ' ikamuingia vilivyo na matokeo yake ndiyo haya sasa.

Sehemu yoyote ile hasa kwa Watu wenye ' akili ' sawasawa pale ukishaona kuwa Mtu fulani bado ana ' Potential ' fulani katika nchi ambayo ina Tija ya Kimaendeleo basi yakupashwa uendelee Kumuamini na Kumtumia ila kama pia umeona mwenyewe kwa Vipimo vyako kuwa GENTAMYCINE ni ' Tishio ' Kwako basi njia pekee ya Kumuweza ni ' Kumjumuisha ' katika ' Utawala ' wako ili uweze Kumlevya Kimamlaka lakini pia Kumdhoofisha ' Kimbinu ' pasipo Yeye kujua lakini kumuacha awepo awepo tu ni hatari kubwa kama ambavyo tunaanza kuiona sasa.

Hata hivyo bado hatujachelewa na hasa hasa Rais Magufuli bado hajachelewa kwani Mimi GENTAMYCINE naamini tena kwa 100% kuwa Mzee Benard Membe anaweza kuwa ni ' msaada ' mkubwa mno wa Kiutawala Kwake ama kwa huu muda alioubakisha kwa muhula wale huu wa Kwanza au hata kwa muhula wake wa pili na mwisho. Asiwasikilize wale ' Wanafiki ' ambao wamemzunguka na ambao hata Yeye pia alishakiri mara nyingi tu kuwa walishawahi hadi kumwambia kuwa Katibu Mkuu wa sasa wa CCM Ndugu Bashiru Ally Kakurwa hafai lakini Yeye mwenyewe akajiridhisha nae na kuamua kufanya nae Kazi na tunaona anafanya vyema tu.

Yangu ni hayo tu ila Mzee Benard Membe bado ni ' Lulu ' kubwa katika ' Utawala ' huu asiachwe na apewe ' Majukumu '.

Nawasilisha.
Kwa akili yako diplomasia anaijua kuliko walioisomea? Mahiga, vipi? Membe is a failure of his own ignorance.
 
CCM aliyoongoza Kikwete au Mkapa ilikuwa na watu makini wakiunda kundi wanunda kweli,

Mwenyekiti aliiogopa CCM yenye meno

Tusidanganyane na kufarijiana, hakuna mwenye Ubavu wa kumuyumbisha Magufuli , ambaye kaifanya CCM kibogoyo kama taasisi nyingine mfano Bunge,

Tuwe wakweli kwamba hofu aliyowajaza wanachama wa CCM hakuna hata kwenye uthubutu wa kuandaa mpango wa kumtoa kabla ya 2025 pia usishangae kwa CCM anayoiongoza anawapangia mpaka mgombea mwaka 2025-2035

CC Pascal Mayalla

Britannica
 
Nazani ata jiwe akija kusoma apa lazmia azimie kwa ofu
naijatwittersavages-20181125-0001.jpeg
 
Wanabodi.
Nimepitia account ya twitter ya Mh Membe aliyofungua 2012 ambayo ina mtiririko rasmi wa matukio yake(maana hakuna verified ) lakini sijaona hayo majibu.

Bernard Membe (@BernardMembe) | Twitter

Katika account hiyo mara ya mwisho kupost ni August 13 2015 alipo-retweet twitter ya Alvaro Rodriguez .

Twiiter account hiyo ina wafuasi 140,000(140K) na imeandika mara (ametweet)1,558 .

Katibu mkuu CCM hasije kuwa ananjibu mtu hasiyekuwepo,Membe hewa au kupitia account za wahuni au hiyo kauli imebuniwa na wajanja kuleta tension tu katika taifa na chama.

Je kwa nini vyombo vya habari vinaandika hiyo kauli bila kuwa na uthibitisho kama ni yake membe?

Sasa haya majibu hapo chini yameandikwa wapi? na kwenye account ipi?...chanzo chake ni wapi?..

''Kufuatia taarifa za kwenye mitandao jioni hii na messages nyingi zinazokuja kwangu, nimeamua kutoa ujumbe huu kwa wote wanaonitakia mema.

Usiku huu nimempelekea KM wa Chama chetu ndugu Bashiru ujumbe wa kukubali kumwona mara nitakaporejea kutoka Nje ya nchi.

Nimeshangazwa kidogo na utaratibu uliotumika kuniita, lakini kwa sababu ya ugeni kazini na kwa sababu ninamheshimu, nitakwenda kumwona Ofisini kwake.

Wote tunajua kuwa mwanzilishi wa tuhuma zote dhidi yangu tunazozisoma na kuzisikia kwenye vyombo cha habari na mitandaoni ni Cyprian Musiba.

Nimemwomba Katibu Mkuu Bashiru kuwa siku nitakayokwenda kumwona, Musiba awepo ili atoe ushahidi kwa sababu mtoa tuhuma ndiye mwenye wajibu wa kuthibitisha aliyoyasema. Mimi kama mtuhumiwa siwajibiki kufanya hivyo. Burden of proof ni ya Musiba. Mimi nitajibu mapigo atakapomaliza kutoa ushahidi mbele ya KM.

Aidha nimemwambia KM kuwa nilitegemea kuwa mara baada ya Mwanaharakati Uchwara kushusha tuhuma nzito kwa watu na viongozi wenye historia na heshima kwenye Chama Mimi nikiwemo, Musiba anayelalamikiwa na wengi kuwa ni mwongo, mzushi, mfitini na mtu asiye na heshima, angaliitwa Chama na TISS ili athibitishe madai yake, na aonywe kwa utovu wake wa nidhamu na kwa kuchafua majina ya viongozi.

Hilo halikufanyika na mwanaume kwa kutumwa na kujituma anaendelea kuchafua watu. Mimi niliamua na bado nitaendelea kukaa kimya kwa sababu Chama na vyombo vya Usalama ndiyo vilivyopaswa kumhoji Musiba.

Baada ya kujiridhisha kuwa aliyoyasema yana mshiko, basi kamati ya maadili ya chama ingalifanya kazi ya kuwaita wahusika kwa kanuni na taratibu za Chama chetu na kuwahoji!

Kutokufanya hivyo, nimemwambia KM ndiko kulikotufanya wengine tuanze kuamini kuwa sauti tunayoisikia ni yake Musiba, lakini akili si yake ni ya kupewa na waliomtuma, wanaomlipa na wanaomlinda. Tuhuma nitungiwe mimi, halafu nitakiwe kuzijibu!! Nikaamua kumpuuza na nitaendelea kufanya hivyo. Kumjibu Musiba ni kumpa heshima asiyostahili.

Mpaka hapo nitakapokutana na KM wa Chama chetu na Musiba, tuvute subira! Nawapenda na kuwashukuruni wote mliotaka niseme neno. BM. "
 
Kuna watu wakipenda kitu wao ni kusifia tu.Hivi Tanzania nzima ni Membe tu ni potential?Kwamba ilikua ni lzm Membe awe included ktk utawala huu na kuachwa ni kosa kubwa sana.
Tatizo unawaza slowslow kama mwendo wa konokono

Nilichomuelewa Genta kama Membe angekuwepo kwenye wadhifa wowote hata ya ubalozi UN huenda huu upinzani na challenge kuelekea uchaguzi 2020 Mh Rais asingeupata na pia angempatia wadhifa angeua ego ya huyu membe ambaye ana timu kubwa tu huko ccm tiss kugombea urais na pia angeweza kuuliwa kisiasa kama muhongo na nchemba alivyofanywa


Fikiria mbali ndugu
 
Kada wa CCM na aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe aliyekuwa mtia nia wa urais kupitia CCM mwaka 2015, akiwa anahojiwa na ITV, mwaka 2013 alidai kwamba, yeye ana maadui 11 na kwamba ikifika mwaka 2016, wataihama Nchi.

Membe aliitoa kauli hiyo akiwa Waziri wa Mambo ya Nje na kwa nafasi yake hiyo, isiyomhusisha na masuala ya ndani ya Nchi, tulitegemea ndiye Waziri wa kwanza ambaye atakuwa na maadui wachache sana nchini, achilia mbali kutokuwa nao kabisa kwani Wizara yake ina-deal zaidi na masuala ya nje ya Nchi.

Hata bungeni, Wizara ya Mambo ya Nje, ni mojawapo ya Wizara chache sana nchini ambazo huwa hazikumbani na maswali magumu bungeni na hupitishwa haraka haraka bila ugumu wowote kutoka kwa Wabunge. Ni kama ilivyo pia kwa Wizara ya Ulinzi.

Sasa, swali linakuja: Kwa kazi gani alizozifanya Bernard Membe katika uwaziri ubunge na wake toka mwaka 2000 hadi 2013, ambao ulimsababishia yeye kuwa na maadui wa mpaka kuweza kutajwa hadi kwenye Tv? Basi hata angekuwa adui 1, maadui yaani wote hao hadi11? Basi napo ungemalizana nao humu humu ndani, yaani unataka hadi wakimbilie Kenya? Ni adhabu gani uliwapangia kuwafanyia hadi uwatake wakimbilie Kenya - ulitaka kuwaua?

Kaulii hiyo ya Membe aliyoitoa kwa umma wa Watanzania ilitaka umma umuone Membe ni strong kuliko Kikwete aliyeonekana dhaifu ama? Je, hao aliowataja ni maadui wa Taifa ama ni maadui wa Membe?

Kwa statement hiyo ya Membe, nini cha kumshauri Rais Magufuli dhidi ya Membe? Na yeye Rais amfukuzie mbali ama?

Je Rais Magufuli amtake Membe kama "anaguna anyooshe mikono ajifanye kama anajukuna?

Je, Membe ndiye anayesifiwa kwa utendaji wa Sera za Mambo ya nje? Soma hapo chini.

Mh Bernard Membe, Ulishafuta kauli hii Kuhusu Rajoelina - JamiiForums

Bernard Membe: Nina maadui 11, ikifika 2016 watakimbilia Kenya! - JamiiForums
Hahahaa....... Kuupanda mchongoma kushuka ndio ngoma nakuona unavyohangaika mkuu!
 
Back
Top Bottom