Bashiru Vs Membe: CCM yatoa msimamo wake kuhusu suala hilo

Bashiru Vs Membe: CCM yatoa msimamo wake kuhusu suala hilo

Mahaba ya Chadema kwa Membe yanasitajaabisha , badala ya kumlilia Mbowe yupo gerezani wako bize kumlilia mwana ccm Membe!!!!

Kila baada ya saa moja kuna mwana Chadema anaanzisha nyuzi ya kumpromote Membe badala Mbowe.

Baada ya Mbowe kufungwa jela vijana wake wote anaowalipa kumtetea mtandaoni wamekacha kumtetea na sasa wameanza kutumia bando aliliowalipa kumtetea Membe.

Katika hali ya kawaida vijana wa Chadema na magazeti yalitakiwa yawe bize kuongelea kufungwa kwa Mbowe lakini sasa hamna chombo cha habari wala gazeti linaloandika habari za mwenyekiti ,

Bavicha na Chadema kwa ujumla macho yao yote ni kwa mwana ccm Membe!!
😀😀😀😀😀
 
Bavicha akili zao wanazojua wenyewe

Uvccm makalio yao wanayajua wenyewe
MBWIGA.jpg
 
Hayo maelezo mengine mengi ni chini yanachosha tu ila kichwa tu cha habari kinajitosheleza kbs kuwa Mh. Rais alibugi au tuseme kuna kachuki kauchaguzi uliopita wa timu A na B kutokana na mparangano wakati wa kuwania nafasi hii adhimu.
Kuna uwezekano pia mkuu alipima maji kama huyu nguli wa kidiplomasia anaweza kupokea na kutekeleza zile zinazoitwa amri toka juu, wakapata mashaka na kumuacha.
Huenda pia kulikuwa na hofu kuwa huyu jamaa ni mashuhuri duniana kidiplomasia na ana akili nyingi na mbinu kwahiyo ni hatari kwa akili kidogo wakaona isiwe tabu wakamtosa.
Inawezekana pia walimhofia kwakuwa timu yake ndani ya chama na serikali ingalipo na inanguvu kwahiyo kumpatia nafasi ndani ya serikali yake ni kuimarisha/kutia nguvu zaidi timu yake na kuhatarisha/kudhoofisha utendaji wa serikali ya awamu hii kama itatokea wangetofautiana ktk maamuzi flaniflani ndani ya serikali. Hofu ya timu JK kuendelea kuwepo serikalini pia inaweza kuwa sababu za kumtosa.
 
Kwahiyo mnataka chadema wakavamie magereza wamkomboe Mbowe!, waandamane kwa kitu kilichopo mahakamani?

Ccm ni mzigo kabisa, hamjaribu kutumia hata 0.2 ya ubongo kufukiri.

Mbafu!
 
Naona unachanganya mambo, kuwa na taarifa sahihi na kuchukua maamuzi sahihi ni mambo mawili tofauti. Kwani hao wanaovuta sigara ni kwamba hawana taarifa sahihi kwamba zina madhara?
Hahahahahah sijui umeandika nini.
 
Chadema wako bize kumpotosha Membe kama walivyompotosha Lowasa.

Mahaba ya Chadema kwa Membe yanasitajaabisha , badala ya kumlilia Mbowe yupo gerezani wako bize kumlilia mwana ccm Membe!!!!

Apotoshwe kwani yeye mtoto mdogo? Hayo mambo yenu wenyewe CCM yamalizeni wenyewe. keshawashika kende mnabaki kulia lia.
 
Kwani keshkokutwa hawezi kupewa dhamana!?oohh maskini amekwisha
 
Pamoja na yote hayo 2020 magufuli ccm hana chake mchuano utakuwa lissu(cdm) na Membe(ccm)
 
Tatizo lake kubwa toka alipoingia madarakani alijua na aliamini kuwa ili aweze kuwa na amani ktk uongozi wake ni kuwamaliza Wapinzani kwa kuvisakama vyama vya siasa. Muda wake mwingi yeye na wapambe wake walikuwa wakifikiri dawa ya Wapinzani hasa CUF na CHADEMA kwani ktk imani yake wasingekuwepo basi wale wapinzani wake kama kina Benard Membe wanhekosa pa kukimbilia pale ambapo angetaka kuwamalizia kisiasa huko huko ccm.

Sasa muda umekwisha Vyama vile bado vipo ila maadui wamekuwa wengi na wanaoungwa mkono ndani ya chama chake mwenyewe.

Suala la Benard kubadili msimamo wakeni ngumu kwa sasa kwani walishamdhiaki kwa muda mrefu na sasa ameshaonyesha uwezo wake ktk kulisuka jeshi lake hasa Kidiplomasia.

Haya tunayoyaanika ni madogo sana kwa yanayoendelea ndani ya chama cha mapinduzi. Ni suala la muda tu huu moshi wa sasa utakuwa ni moto mkubwa na hakutakuwa na wakuuzima.

Kama angeachana na vyama vya upinzani wafanye shughuli za halali za kisiasa hakika ccm isinhefika hapa kwani uhuru wakujieleza ungekuwa wazi na hata hili la Benard Membe angeling'amua mapema. Sasa yeye kila kukicha yeye na viongozi wa upinzani kiasi kwamba hataki kuwaona hata uraiani wakitafuta riziki kwajili ya familia zao.
Jamaa kajifanya mjanja na kusahau kwamba;mjanja hajinyoi.
Tuone chamelon amnyonyoe atie akili
 
Na misukule mwaka huu inaipambwa kwa kila rangi. Membe hata ule uwaziri wa mambo ya nje alikuwa hafai. Alibebwa tu kwenye ule utawala ulikuwa umejaa vilaza kama kina Masha, Ngeleja nk

Asante kwa Kuchangia siku njema!
 
Yanasemwa mengi na yatasemwa mengi ila kama kuna Kosa kubwa ambalo Rais Dkt. Magufuli amelifanya ( na naamini hapa atakuwa alishauriwa vibaya na Watu wake ) ni kuweka mbali au kukaa mbali na ' Fundi wa Diplomasia ' Benard Membe na kwa maoni yangu huenda leo hii tunaona baadhi ya matatizo ya hapa na pale yanatokea hasa Kimataifa kwakuwa hana ' Mafundi ' kama akina Membe.

Hata kama huyu Mtu ( Membe ) aliamua Kuachana na Ubunge lakini Mimi kama GENTAMYCINE bado naamini kwamba Mheshimiwa Rais Magufuli kwa ' Mandate ' yake kama ' Executive ' bado alikuwa anaweza Kumtumia katika ' Baraza ' lake la Mawaziri au hata katika maeneo mengine hasa ya Kidiplomasia ambayo kwa Mimi naona kwamba hadi hivi leo bado tunafanya vibaya na mifano juu ya hili iko mingi tu.

Kwa Mtu mwenye ' exposure ' kubwa na ' iliyotukuka ' kabisa huku akiwa amewahi Kuhudumu katika moja ya Idara / Taasisi muhimu / nyeti Kiusalama katika nchi hii kama Mzee Benard Membe leo hii kumuacha awe tu hivi ' huru ' nadhani ' technically ' kabisa hapa kuna Kosa kubwa sana lilifanyika ama kwa Watu kutokujua au Mheshimiwa Rais Magufuli alilishwa ' Sumu ' za ' Kimajungu ' na Watu wake wa karibu ambao anawaamini nae ' Sumu ' ikamuingia vilivyo na matokeo yake ndiyo haya sasa.

Sehemu yoyote ile hasa kwa Watu wenye ' akili ' sawasawa pale ukishaona kuwa Mtu fulani bado ana ' Potential ' fulani katika nchi ambayo ina Tija ya Kimaendeleo basi yakupashwa uendelee Kumuamini na Kumtumia ila kama pia umeona mwenyewe kwa Vipimo vyako kuwa GENTAMYCINE ni ' Tishio ' Kwako basi njia pekee ya Kumuweza ni ' Kumjumuisha ' katika ' Utawala ' wako ili uweze Kumlevya Kimamlaka lakini pia Kumdhoofisha ' Kimbinu ' pasipo Yeye kujua lakini kumuacha awepo awepo tu ni hatari kubwa kama ambavyo tunaanza kuiona sasa.

Hata hivyo bado hatujachelewa na hasa hasa Rais Magufuli bado hajachelewa kwani Mimi GENTAMYCINE naamini tena kwa 100% kuwa Mzee Benard Membe anaweza kuwa ni ' msaada ' mkubwa mno wa Kiutawala Kwake ama kwa huu muda alioubakisha kwa muhula wale huu wa Kwanza au hata kwa muhula wake wa pili na mwisho. Asiwasikilize wale ' Wanafiki ' ambao wamemzunguka na ambao hata Yeye pia alishakiri mara nyingi tu kuwa walishawahi hadi kumwambia kuwa Katibu Mkuu wa sasa wa CCM Ndugu Bashiru Ally Kakurwa hafai lakini Yeye mwenyewe akajiridhisha nae na kuamua kufanya nae Kazi na tunaona anafanya vyema tu.

Yangu ni hayo tu ila Mzee Benard Membe bado ni ' Lulu ' kubwa katika ' Utawala ' huu asiachwe na apewe ' Majukumu '.

Nawasilisha.
hivi kwani Membe si mwanachama wa kawaida tu upande ule
 
Kada wa CCM na aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe aliyekuwa mtia nia wa urais kupitia CCM mwaka 2015, akiwa anahojiwa na ITV, mwaka 2013 alidai kwamba, yeye ana maadui 11 na kwamba ikifika mwaka 2016, wataihama Nchi.

Membe aliitoa kauli hiyo akiwa Waziri wa Mambo ya Nje na kwa nafasi yake hiyo, isiyomhusisha na masuala ya ndani ya Nchi, tulitegemea ndiye Waziri wa kwanza ambaye atakuwa na maadui wachache sana nchini, achilia mbali kutokuwa nao kabisa kwani Wizara yake ina-deal zaidi na masuala ya nje ya Nchi.

Hata bungeni, Wizara ya Mambo ya Nje, ni mojawapo ya Wizara chache sana nchini ambazo huwa hazikumbani na maswali magumu bungeni na hupitishwa haraka haraka bila ugumu wowote kutoka kwa Wabunge. Ni kama ilivyo pia kwa Wizara ya Ulinzi.

Sasa, swali linakuja: Kwa kazi gani alizozifanya Bernard Membe katika uwaziri ubunge na wake toka mwaka 2000 hadi 2013, ambao ulimsababishia yeye kuwa na maadui wa mpaka kuweza kutajwa hadi kwenye Tv? Basi hata angekuwa adui 1, maadui yaani wote hao hadi11? Basi napo ungemalizana nao humu humu ndani, yaani unataka hadi wakimbilie Kenya? Ni adhabu gani uliwapangia kuwafanyia hadi uwatake wakimbilie Kenya - ulitaka kuwaua?

Kaulii hiyo ya Membe aliyoitoa kwa umma wa Watanzania ilitaka umma umuone Membe ni strong kuliko Kikwete aliyeonekana dhaifu ama? Je, hao aliowataja ni maadui wa Taifa ama ni maadui wa Membe?

Kwa statement hiyo ya Membe, nini cha kumshauri Rais Magufuli dhidi ya Membe? Na yeye Rais amfukuzie mbali ama?

Je Rais Magufuli amtake Membe kama "anaguna anyooshe mikono ajifanye kama anajukuna?

Je, Membe ndiye anayesifiwa kwa utendaji wa Sera za Mambo ya nje? Soma hapo chini.

Mh Bernard Membe, Ulishafuta kauli hii Kuhusu Rajoelina - JamiiForums

Bernard Membe: Nina maadui 11, ikifika 2016 watakimbilia Kenya! - JamiiForums
 
Rais Dk. John Pombe Magufuli, hana kinyongo chochote na Viongozi wenzake ndani ya CCM na ndani ya Serikali na ndani ya Dola lakini wao wanamhujumu kwa nia zao mbaya. Wengi walipewa nafasi huko nyuma walishindwa ku-deliver, amekuja mwenzao wanaanza kumuonea wivu.

Magufuli pitia hiki Kitabu cha The Prince cha Karne ya 16 kutoka kwa gwiji la Kitaliano, Niccolo Machiavelli, upate ushauri namna ya ku-deal na adversaries wako.

Machiavelli's The Prince
 
Back
Top Bottom