Episode 1: Ikaripotiwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM, Dr. Bashiru Ally Kakurwa amemuita, kupitia vyombo vya habari aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Benard Camilius Membe kuzungumza naye juu ya tuhuma dhidi ya Membe ya kuanza kusaka kura za Urais za mwaka 2020.
Episode 2: Ikaripotiwa kuwa Membe, kupitia mitandao ya kijamii, akamjibu Dr. Bashiru. Pamoja na mambo mengine, Membe aliyaweka wazi mambo makubwa yafuatayo. Mosi, alikubali wito wa Katibu Mkuu wake na kuahidi kwenda kumuona atakaporejea nchini kwakuwa kwasasa yuko nje ya nchi. Pili, Membe aliomba 'muunda tuhuma' Cyprian Musiba awepo ili ajibu tuhuma zake. Tatu, Membe alikosoa namna alivyoitwa na Katibu Mkuu na kusema kuwa Katibu Mkuu ni mgeni kwenye uongozi wa chama.
Episode 3: Katibu Mkuu wa CCM Dr. Bashiru Ally Kakurwa hakusema ndiyo au hapana kuhusu ombi la Membe la uwepo wa Musiba katika kukutana kwao ili Membe asikie tuhuma zake na kuzijibu.
Episode 4: Ikaripotiwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM Dr. Bashiru Ally Kakurwa amemjibu Membe kuhusu ugeni wake ndani ya CCM kwa kusema kuwa yeye Katibu Mkuu ni mgeni kwenye Team Lowassa na Team Membe lakini si mgeni CCM na taratibu zake.
Episode 5: Imeandikwa na gazeti la leo la Mwananchi kuwa mkongwe wa siasa na uongozi wa hapa nchini, Mzee Pius Msekwa amemkosoa Katibu Mkuu wa CCM hasa katika namna alivyomuita Membe. Msekwa amesema kuwa ni afadhali Katibu Mkuu angetumia barua au simu kumuita lakini si njia iliyotumika.
Episode 6: Dr. Bashiru na Membe wanakaribia kuonana. Wameshajibizana, kukosolewa na kuungwa mkono na watu mbalimbali ndani ya chama chao na hata nje ya chama chao cha Mapinduzi. Wote ni binaadamu wenye hisia za kufurahi na kuchukia. Watatazamana na kuzungumza vipi kiutulivu watakapokutana kwa uwepo wa yaliyotokea baina yao?
Political Forecast: CCM inamuandaa mgombea wa Urais wa 'kumsimamisha' upinzani mwaka 2020!
Episode 1: Ikaripotiwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM, Dr. Bashiru Ally Kakurwa amemuita, kupitia vyombo vya habari aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Benard Camilius Membe kuzungumza naye juu ya tuhuma dhidi ya Membe ya kuanza kusaka kura za Urais za mwaka 2020.
Episode 2: Ikaripotiwa kuwa Membe, kupitia mitandao ya kijamii, akamjibu Dr. Bashiru. Pamoja na mambo mengine, Membe aliyaweka wazi mambo makubwa yafuatayo. Mosi, alikubali wito wa Katibu Mkuu wake na kuahidi kwenda kumuona atakaporejea nchini kwakuwa kwasasa yuko nje ya nchi. Pili, Membe aliomba 'muunda tuhuma' Cyprian Musiba awepo ili ajibu tuhuma zake. Tatu, Membe alikosoa namna alivyoitwa na Katibu Mkuu na kusema kuwa Katibu Mkuu ni mgeni kwenye uongozi wa chama.
Episode 3: Katibu Mkuu wa CCM Dr. Bashiru Ally Kakurwa hakusema ndiyo au hapana kuhusu ombi la Membe la uwepo wa Musiba katika kukutana kwao ili Membe asikie tuhuma zake na kuzijibu.
Episode 4: Ikaripotiwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM Dr. Bashiru Ally Kakurwa amemjibu Membe kuhusu ugeni wake ndani ya CCM kwa kusema kuwa yeye Katibu Mkuu ni mgeni kwenye Team Lowassa na Team Membe lakini si mgeni CCM na taratibu zake.
Episode 5: Imeandikwa na gazeti la leo la Mwananchi kuwa mkongwe wa siasa na uongozi wa hapa nchini, Mzee Pius Msekwa amemkosoa Katibu Mkuu wa CCM hasa katika namna alivyomuita Membe. Msekwa amesema kuwa ni afadhali Katibu Mkuu angetumia barua au simu kumuita lakini si njia iliyotumika.
Episode 6: Dr. Bashiru na Membe wanakaribia kuonana. Wameshajibizana, kukosolewa na kuungwa mkono na watu mbalimbali ndani ya chama chao na hata nje ya chama chao cha Mapinduzi. Wote ni binaadamu wenye hisia za kufurahi na kuchukia. Watatazamana na kuzungumza vipi kiutulivu watakapokutana kwa uwepo wa yaliyotokea baina yao?
Political Forecast: CCM inamuandaa mgombea wa Urais wa 'kumsimamisha' upinzani mwaka 2020!
Yanasemwa mengi na yatasemwa mengi ila kama kuna Kosa kubwa ambalo Rais Dkt. Magufuli amelifanya ( na naamini hapa atakuwa alishauriwa vibaya na Watu wake ) ni kuweka mbali au kukaa mbali na ' Fundi wa Diplomasia ' Benard Membe na kwa maoni yangu huenda leo hii tunaona baadhi ya matatizo ya hapa na pale yanatokea hasa Kimataifa kwakuwa hana ' Mafundi ' kama akina Membe.
Nimekuelewa vyema ... uko sahihi. Kiongozi ni lazima atafakari kwanza kabla ya kutoa tamko lolote. Matamshi ya kiongozi yanapoleta mtafaruku hayatatufikisha popote.Kwa taarifa yako hata angekaa naye karibu huyo Membe ndio angefundishwa hiyo diplomasia. Ogopa mtu aliyekuja na mbinu ya kwamba kama una korosho na huna shamba hizo korosho utazila, lakini hatuoni wanaouza magari wakionyesha viwanda walipotengenezea hayo magari, na wanaochoma mahindi humu mjini hawaonyeshi mashamba walipoyalimia. Kipa wa ile timu yako ndio anazingua.
2020 twende na MembeYanasemwa mengi na yatasemwa mengi ila kama kuna Kosa kubwa ambalo Rais Dkt. Magufuli amelifanya ( na naamini hapa atakuwa alishauriwa vibaya na Watu wake ) ni kuweka mbali au kukaa mbali na ' Fundi wa Diplomasia ' Benard Membe na kwa maoni yangu huenda leo hii tunaona baadhi ya matatizo ya hapa na pale yanatokea hasa Kimataifa kwakuwa hana ' Mafundi ' kama akina Membe.
Hata kama huyu Mtu ( Membe ) aliamua Kuachana na Ubunge lakini Mimi kama GENTAMYCINE bado naamini kwamba Mheshimiwa Rais Magufuli kwa ' Mandate ' yake kama ' Executive ' bado alikuwa anaweza Kumtumia katika ' Baraza ' lake la Mawaziri au hata katika maeneo mengine hasa ya Kidiplomasia ambayo kwa Mimi naona kwamba hadi hivi leo bado tunafanya vibaya na mifano juu ya hili iko mingi tu.
Kwa Mtu mwenye ' exposure ' kubwa na ' iliyotukuka ' kabisa huku akiwa amewahi Kuhudumu katika moja ya Idara / Taasisi muhimu / nyeti Kiusalama katika nchi hii kama Mzee Benard Membe leo hii kumuacha awe tu hivi ' huru ' nadhani ' technically ' kabisa hapa kuna Kosa kubwa sana lilifanyika ama kwa Watu kutokujua au Mheshimiwa Rais Magufuli alilishwa ' Sumu ' za ' Kimajungu ' na Watu wake wa karibu ambao anawaamini nae ' Sumu ' ikamuingia vilivyo na matokeo yake ndiyo haya sasa.
Sehemu yoyote ile hasa kwa Watu wenye ' akili ' sawasawa pale ukishaona kuwa Mtu fulani bado ana ' Potential ' fulani katika nchi ambayo ina Tija ya Kimaendeleo basi yakupashwa uendelee Kumuamini na Kumtumia ila kama pia umeona mwenyewe kwa Vipimo vyako kuwa GENTAMYCINE ni ' Tishio ' Kwako basi njia pekee ya Kumuweza ni ' Kumjumuisha ' katika ' Utawala ' wako ili uweze Kumlevya Kimamlaka lakini pia Kumdhoofisha ' Kimbinu ' pasipo Yeye kujua lakini kumuacha awepo awepo tu ni hatari kubwa kama ambavyo tunaanza kuiona sasa.
Hata hivyo bado hatujachelewa na hasa hasa Rais Magufuli bado hajachelewa kwani Mimi GENTAMYCINE naamini tena kwa 100% kuwa Mzee Benard Membe anaweza kuwa ni ' msaada ' mkubwa mno wa Kiutawala Kwake ama kwa huu muda alioubakisha kwa muhula wale huu wa Kwanza au hata kwa muhula wake wa pili na mwisho. Asiwasikilize wale ' Wanafiki ' ambao wamemzunguka na ambao hata Yeye pia alishakiri mara nyingi tu kuwa walishawahi hadi kumwambia kuwa Katibu Mkuu wa sasa wa CCM Ndugu Bashiru Ally Kakurwa hafai lakini Yeye mwenyewe akajiridhisha nae na kuamua kufanya nae Kazi na tunaona anafanya vyema tu.
Yangu ni hayo tu ila Mzee Benard Membe bado ni ' Lulu ' kubwa katika ' Utawala ' huu asiachwe na apewe ' Majukumu '.
Nawasilisha.
Si mchezoWatatazamana kwa macho na kusikilizana kwa masikio yao, BTW
Dr Bashiru kashaharibu anatafuta huruma ya wenzake na Polepole kaanza kumsaidia