Kada wa CCM na aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe aliyekuwa mtia nia wa urais kupitia CCM mwaka 2015, akiwa anahojiwa na ITV, mwaka 2013 alidai kwamba, yeye ana maadui 11 na kwamba ikifika mwaka 2016, wataihama Nchi.
Membe aliitoa kauli hiyo akiwa Waziri wa Mambo ya Nje na kwa nafasi yake hiyo, isiyomhusisha na masuala ya ndani ya Nchi, tulitegemea ndiye Waziri wa kwanza ambaye atakuwa na maadui wachache sana nchini, achilia mbali kutokuwa nao kabisa kwani Wizara yake ina-deal zaidi na masuala ya nje ya Nchi.
Hata bungeni, Wizara ya Mambo ya Nje, ni mojawapo ya Wizara chache sana nchini ambazo huwa hazikumbani na maswali magumu bungeni na hupitishwa haraka haraka bila ugumu wowote kutoka kwa Wabunge. Ni kama ilivyo pia kwa Wizara ya Ulinzi.
Sasa, swali linakuja: Kwa kazi gani alizozifanya Bernard Membe katika uwaziri ubunge na wake toka mwaka 2000 hadi 2013, ambao ulimsababishia yeye kuwa na maadui wa mpaka kuweza
kutajwa hadi kwenye Tv? Basi hata angekuwa
adui 1, maadui yaani wote hao hadi11? Basi napo ungemalizana nao humu humu ndani, yaani unataka
hadi wakimbilie Kenya? Ni adhabu gani uliwapangia kuwafanyia hadi uwatake wakimbilie Kenya - ulitaka kuwaua?
Kaulii hiyo ya Membe aliyoitoa kwa umma wa Watanzania ilitaka umma umuone Membe ni strong kuliko Kikwete aliyeonekana dhaifu ama? Je, hao aliowataja ni maadui wa Taifa ama ni maadui wa Membe?
Kwa statement hiyo ya Membe, nini cha kumshauri Rais Magufuli dhidi ya Membe? Na yeye Rais amfukuzie mbali ama?
Je Rais Magufuli amtake Membe kama "anaguna anyooshe mikono ajifanye kama anajukuna?
Je, Membe ndiye anayesifiwa kwa utendaji wa Sera za Mambo ya nje? Soma hapo chini.
Mh Bernard Membe, Ulishafuta kauli hii Kuhusu Rajoelina - JamiiForums
Bernard Membe: Nina maadui 11, ikifika 2016 watakimbilia Kenya! - JamiiForums